Utetezi wa Sabaya kuwa alifanya uhalifu kwa amri ya mamlaka iliyomteua ni sababu kubwa kwa nini Tanzania tunahitaji mabadiliko ya Katiba

Utetezi wa Sabaya kuwa alifanya uhalifu kwa amri ya mamlaka iliyomteua ni sababu kubwa kwa nini Tanzania tunahitaji mabadiliko ya Katiba

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Naamini kwa dhati kabisa kile alichosema Sabaya, kwamba matendo ya kihalifu aliyofanya Arusha ilikuwa maagizo toka mamlaka iliyomteua na alipaswa kutii. Sabaya ameenda mbali, akasema haikuwa mara ya kwanza kupewa maagizo kama hayo.

Na ni wazi kwamba Sabaya kama Mkuu wa Wilaya nje ya Arusha, asingekuwa na uthubutu wa kwenda kutenda mambo kama hayo nje ya mkoa wake. Kwa hiyo lazima kujiamini huko kulitokana na kufanya mambo kwa amri ya Raisi.

Jambo la msingi ni kwamba, ni wangapi waliagizwa kufanya matendo kama haya ya Sabaya na mamlaka zilizowateua? Na je, kuna walioamrishwa kuua raia? Kupotea kwa baadhi ya Watanzania kama kina Ben Saanane na wengineo, ni dalili tosha kwamba inawezekana kuna wengine kama Sabaya waliagizwa kuvunja haki za binadamu na mamlaka za juu zilizowateua, na hata kupoteza haki za watu kuishi.

Tukirudi nyuma kidogo, twapaswa kujiuliza, kwa nini hii mamlaka ya juu ilitoa amri kwa watu kama Sabaya ikijua wazi amri hizo zilikiuka haki za binadamu na hata kuwakosesha watu haki ya kuishi? Ni wazi tatizo liko kwenye Katiba yetu ambapo mamlaka hii ya juu ilitambua haiwezi kamwe kushitakiwa hata ingefanya jambo gani!

Sasa turudi kwa Raisi wetu wa sasa Samia na chama chake CCM. Hawaoni kwamba huu ni upungufu mkubwa sana katika Katiba yetu, kuwa na mamlaka ya juu ambayo yana uhuru wa kutoa maagizo ya kuvunja haki za binadamu na hata kuua kwa kiburi tu cha kujua mamlaka ya juu haiwezi kuwajibishwa kisheria kwa lolote?

Inatutia wasiwasi basi sababu za msingi kwa nini Raisi Samia na CCM wanapinga kwa nguvu zote mabadiliko ya Katiba. Hivi tuingie shaka kwamba Raisi Samia hataki Katiba mpya kwa sababu na yeye angependa kuwa na uwezo wa kutoa maagizo kama aliyopewa Sabaya na wengineo ambao mambo ya kutisha waliyofanya bado hayajawekwa wazi, ili yeye na wengine katika CCM kama Spika, Mwanasheria Mkuu nk wasije wakawajibishwa kisheria hapo baadae?

Kwa msingi huu, utetezi wa Sabaya kwamba alifanya aliyofanya kwa sababu yalikuwa ni maagizo toka mamlaka iliyomteua ni kengelea yenye sauti kubwa kwamba Katiba ya Tanzania ni lazima ifanyiwe mabadiliko.
 
Naunga mkono hoja! Nipo tayari kuchangia kiasi cha fedha ili tu ile Rasimu ya Jaji Warioba ipitishwe kwa marekebisho machache, na kuwa Katiba Mpya ya Wananchi.

Porojo za kujenga uchumi kwanza, tumechoka kuzisikia.
 
wenye waliompa mwongozo wa kujitetea hivyo sio mafala...mpaka kukamatwa kwake hao viongozi walikuwa wapi kuzuia asikamatwe? Unajuaje pengine amewasiliana nao lakini ushirikiano ukawa sifuri? Vitu ni vingi sana mpaka huyu jamaa kufikia kujitetea hivyo..tusubiri meza ishapinduliwa...[emoji3166]
 
wenye waliompa mwongozo wa kujitetea hivyo sio mafala...mpaka kukamatwa kwake hao viongozi walikuwa wapi kuzuia asikamatwe? Unajuaje pengine amewasiliana nao lakini ushirikiano ukawa sifuri? Vitu ni vingi sana mpaka huyu jamaa kufikia kujitetea hivyo..tusubiri meza ishapinduliwa...[emoji3166]

Majasusi huwa hawasaidianagi? Ama wao ni kuchekelea mwenzao anaponyolewa huku wakitia maji.
 
Nchi hii mtu anaanzisha operesheni za kishenzi usalama wa taifa upo, IGP na Jeshi lake wapo.

Unajiuliza unashangaa hupati majibu.
 
wenye waliompa mwongozo wa kujitetea hivyo sio mafala...mpaka kukamatwa kwake hao viongozi walikuwa wapi kuzuia asikamatwe? Unajuaje pengine amewasiliana nao lakini ushirikiano ukawa sifuri? Vitu ni vingi sana mpaka huyu jamaa kufikia kujitetea hivyo..tusubiri meza ishapinduliwa...[emoji3166]
Hata mimi nilikuwa nawaza hivyo. Baada ya kuona wamemtelekeza ikabidi ajilipue tu. Lakini amewahi sana maana hata msoto bado hajapata.
 
Viongozi wa ccm na wanachama wa ccm waliopo JamiiForums akili zao zimefanana sanaaaa.


Lunatic [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Umuhimu wa Katiba Mpya unazidi kujithibitisha.
 
Lakini kwa akili za kawaida yule alietoa maelekezo na yule alieopokea maelekezo unadhani wataheshimu katiba mpya hata kama itawazuia kufanya maovu?
Kwani hata katika katiba ya Msekwa (katiba ya sasa)walioyafanya hayavumiliki.
Na hata pale walipobadirisha sheria ya kutoshitakiwa ni batili kwa kuwa ni binadamu hawawezi kuwa juu ya sheria,ndio sababu wote tumeambia tupige chanjo ya Covid-19 kwani we are human beings not angels.
 
wenye waliompa mwongozo wa kujitetea hivyo sio mafala...mpaka kukamatwa kwake hao viongozi walikuwa wapi kuzuia asikamatwe? Unajuaje pengine amewasiliana nao lakini ushirikiano ukawa sifuri? Vitu ni vingi sana mpaka huyu jamaa kufikia kujitetea hivyo..tusubiri meza ishapinduliwa...[emoji3166]
Hivi kwanini Sabaya alilia sana pale Dom kuuga mwili wa JPM. Aliangua kilio zaidi ya watoto wa Mwendazake.

Kwani kuna jipya katika mambo anayoyaongea? Tokea Tanzania imeanza ni wakuu wa wilaya wangapi au viongozi waliokwisha tekeleza operations za kutosha kabisa na hawajawahi kuingia katika traps hizo?

Yaani unataka kunambia Rais SSH ni mjinga sana kiasi hicho katika wakuu wa wilaya wote Tanzania amsimamishe yeye tu na kuagiza uchunguzi?
 
Kama huu uzi umeandika bila shinikizo lolote basi wewe ni miongoni mwa watu ambao hawajaelewa utetezi wa sabaya kwa sababu zifuatazo:
-Hajakiri kufanya uhalifu isipokuwa kasema dhumuni la kufika kwake dukani pale ni kumkamata mmiliki wa duka lile kama alivyoagizwa na wakuu wake japo hawakumkuta.
-Kumbuka pia sabaya kasema yule mtuhumiwa mwingine yeye hamtambui kwa sababu hakuwa miongoni mwa wale wanne ambao yeye aliongozana nao.
 
Hivi kwanini Sabaya alilia sana pale Dom kuuga mwili wa JPM. Aliangua kilio zaidi ya watoto wa Mwendazake.

Kwani kuna jipya katika mambo anayoyaongea? Tokea Tanzania imeanza ni wakuu wa wilaya wangapi au viongozi waliokwisha tekeleza operations za kutosha kabisa na hawajawahi kuingia katika traps hizo?

Yaani unataka kunambia Rais SSH ni mjinga sana kiasi hicho katika wakuu wa wilaya wote Tanzania amsimamishe yeye tu na kuagiza uchunguzi?

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Mkuu kwa utetezi alioutoa sabaya jana umetengeneza mwanya wa mashahidi wengine kuongezeka na naomba uniamini kwamba sabaya ataachiwa huru hivi karibuni.
 
Naamini kwa dhati kabisa kile alichosema Sabaya, kwamba matendo ya kihalifu aliyofanya Arusha ilikuwa maagizo toka mamlaka iliyomteua na alipaswa kutii. Sabaya ameenda mbali, akasema haikuwa mara ya kwanza kupewa maagizo kama hayo.

Na ni wazi kwamba Sabaya kama Mkuu wa Wilaya nje ya Arusha, asingekuwa na uthubutu wa kwenda kutenda mambo kama hayo nje ya mkoa wake. Kwa hiyo lazima kujiamini huko kulitokana na kufanya mambo kwa amri ya Raisi.

Jambo la msingi ni kwamba, ni wangapi waliagizwa kufanya matendo kama haya ya Sabaya na mamlaka zilizowateua? Na je, kuna walioamrishwa kuua raia? Kupotea kwa baadhi ya Watanzania kama kina Ben Saanane na wengineo, ni dalili tosha kwamba inawezekana kuna wengine kama Sabaya waliagizwa kuvunja haki za binadamu na mamlaka za juu zilizowateua, na hata kupoteza haki za watu kuishi.

Tukirudi nyuma kidogo, twapaswa kujiuliza, kwa nini hii mamlaka ya juu ilitoa amri kwa watu kama Sabaya ikijua wazi amri hizo zilikiuka haki za binadamu na hata kuwakosesha watu haki ya kuishi? Ni wazi tatizo liko kwenye Katiba yetu ambapo mamlaka hii ya juu ilitambua haiwezi kamwe kushitakiwa hata ingefanya jambo gani!

Sasa turudi kwa Raisi wetu wa sasa Samia na chama chake CCM. Hawaoni kwamba huu ni upungufu mkubwa sana katika Katiba yetu, kuwa na mamlaka ya juu ambayo yana uhuru wa kutoa maagizo ya kuvunja haki za binadamu na hata kuua kwa kiburi tu cha kujua mamlaka ya juu haiwezi kuwajibishwa kisheria kwa lolote?

Inatutia wasiwasi basi sababu za msingi kwa nini Raisi Samia na CCM wanapinga kwa nguvu zote mabadiliko ya Katiba. Hivi tuingie shaka kwamba Raisi Samia hataki Katiba mpya kwa sababu na yeye angependa kuwa na uwezo wa kutoa maagizo kama aliyopewa Sabaya na wengineo ambao mambo ya kutisha waliyofanya bado hayajawekwa wazi, ili yeye na wengine katika CCM kama Spika, Mwanasheria Mkuu nk wasije wakawajibishwa kisheria hapo baadae?

Kwa msingi huu, utetezi wa Sabaya kwamba alifanya aliyofanya kwa sababu yalikuwa ni maagizo toka mamlaka iliyomteua ni kengelea yenye sauti kubwa kwamba Katiba ya Tanzania ni lazima ifanyiwe mabadiliko.
Vip kuna mwingine?
 
Naamini kwa dhati kabisa kile alichosema Sabaya, kwamba matendo ya kihalifu aliyofanya Arusha ilikuwa maagizo toka mamlaka iliyomteua na alipaswa kutii. Sabaya ameenda mbali, akasema haikuwa mara ya kwanza kupewa maagizo kama hayo.

Na ni wazi kwamba Sabaya kama Mkuu wa Wilaya nje ya Arusha, asingekuwa na uthubutu wa kwenda kutenda mambo kama hayo nje ya mkoa wake. Kwa hiyo lazima kujiamini huko kulitokana na kufanya mambo kwa amri ya Raisi.

Jambo la msingi ni kwamba, ni wangapi waliagizwa kufanya matendo kama haya ya Sabaya na mamlaka zilizowateua? Na je, kuna walioamrishwa kuua raia? Kupotea kwa baadhi ya Watanzania kama kina Ben Saanane na wengineo, ni dalili tosha kwamba inawezekana kuna wengine kama Sabaya waliagizwa kuvunja haki za binadamu na mamlaka za juu zilizowateua, na hata kupoteza haki za watu kuishi.

Tukirudi nyuma kidogo, twapaswa kujiuliza, kwa nini hii mamlaka ya juu ilitoa amri kwa watu kama Sabaya ikijua wazi amri hizo zilikiuka haki za binadamu na hata kuwakosesha watu haki ya kuishi? Ni wazi tatizo liko kwenye Katiba yetu ambapo mamlaka hii ya juu ilitambua haiwezi kamwe kushitakiwa hata ingefanya jambo gani!

Sasa turudi kwa Raisi wetu wa sasa Samia na chama chake CCM. Hawaoni kwamba huu ni upungufu mkubwa sana katika Katiba yetu, kuwa na mamlaka ya juu ambayo yana uhuru wa kutoa maagizo ya kuvunja haki za binadamu na hata kuua kwa kiburi tu cha kujua mamlaka ya juu haiwezi kuwajibishwa kisheria kwa lolote?

Inatutia wasiwasi basi sababu za msingi kwa nini Raisi Samia na CCM wanapinga kwa nguvu zote mabadiliko ya Katiba. Hivi tuingie shaka kwamba Raisi Samia hataki Katiba mpya kwa sababu na yeye angependa kuwa na uwezo wa kutoa maagizo kama aliyopewa Sabaya na wengineo ambao mambo ya kutisha waliyofanya bado hayajawekwa wazi, ili yeye na wengine katika CCM kama Spika, Mwanasheria Mkuu nk wasije wakawajibishwa kisheria hapo baadae?

Kwa msingi huu, utetezi wa Sabaya kwamba alifanya aliyofanya kwa sababu yalikuwa ni maagizo toka mamlaka iliyomteua ni kengelea yenye sauti kubwa kwamba Katiba ya Tanzania ni lazima ifanyiwe mabadiliko.
JamiiForums1485051612.jpg
 
Back
Top Bottom