Ndugu wana Jamii na wapenzi wa mpira nchini.
Kwako TFF.
Nawasilisha utetezi wangu kwako kuwahusu wateja wangu Yanga na wachezaji wake watano uliowapa adhabu hivi karibuni. Yanga anahusika kwa vile umemnyima haki ya kuwafanyisha kazi waajiriwa wake halali kwa vipindi mbali mbali.
Utetezi wa 1: Ukubwa wa adhabu
Bila kujali kama wamefanya kosa au la napenda nawasilisha utetezi kuwa adhabu uliowapa ni kubwa sana na inaonyesha kuwa na agenda nje ya kosa lenyewe. Kwa kawaida unapotaka kumhukumu mtu yeyote aliye fanya kosa, lazima utumie sheria, kanuni zilizopo bila kusahau hukumu ulizokwisha pitisha kwa wengine waliofanya makosa kama hayo. Napinga ukubwa wa adhabu kwa wachezaji wa Yanga kwa kutumia hoja ya hukumu ulizowahi kupitisha kama ifuatavyo:
1. Katika mchezo dhidi ya Simba na Oljoro JKT mchezaji Patrick Mafisango alimsukuma mwamuzi Isihaka Shirikisho baada ya kumuonesha kadi nyekundu mchezaji mwenzake Haruna Moshi. Kamati yako iliamuadhibu Mafisango kwa kuamuru simba imwandikie barua ya onyo kali kwa kitendo chake hicho ambacho kinafanana sana na hiki cha wateja wangu. Source:Mafisango Aonywa, Simba Yapigwa Faini . Au tuseme ni kwa vile ulikosa ushahidi wa video kutoka redio clouds ukimuonyesha mafisango akikimbia kutoka mbali sana kama alivyofanya mchezaji wa Yanga, na kuja kumsukuma mwamuzi?
2: KIPA Juma Kaseja wa timu ya Simba alionyesha utovu wa nidhamu cha kugoma kupeana mkono na aliyekuwa mgeni rasmi katika mechi ya Simba na Yanga iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Kamati yako ilimuadhibu kwa kumfungia mechi tatu na faini ya shs 500,000. Ndio tuseme Refa ni zaidi ya mgeni rasmi?
3. Mchezaji Aziz Sibo wa African Lyon alifungiwa kutocheza mechi tatu na faini ya sh 500,000 kwa kosa la kumtandika kichwa mchezaji wa Polisi ya Dodoma
source:TFF yatoa adhabu kwa watovu wa nidhamu
Kesi kama hizi ziko nyingi ambazo kumbukumbu zake unazo. Kwa hoja hii naomba utengue uamzi wako wa kuwafungia wachezaji wa Yanga zaidi ya mechi tatu.
Utetezi wa 2: Kuwanyima nafasi ya Kujitetea
Ni kitendo cha haki kumsikiliza mtuhumiwa kabla ya kumpa adhabu. Kitendo hiki sio tu kinatoa haki bali pia uwezesha wenye mamlaka kugundua tatizo la ndani ambalo ni kiini cha tatizo lililotokea. Kwa vile wateja wangu hawakupata haki hiyo naomba utengue hukumu yako mara moja.
Hii ni sawa na kesi iliyokuwa inawahusu Rage na Sendeu kwa kitendo chao kilichodhaniwa ni kuhujumu mechi. Pamoja na kwamba walisikika redioni wakieleza nia ya kugomea mchezo bado kamati ya Tibaigana iliwataka walete maelezo ya kujitetea kabla ya kuwahukumu.
Source:Tibaigana kuwahoji Rage, Sendeu
Utetezi wa 3: Uhalali wa Kamati iliyotoa hukumu.
Kamati iliyotoa hukumu ni kamati ya ligi ambayo hata kama inayo mamlaka bado ina wajumbe ambao wana Conflict of Interest katika hili swala, mfano Nyange Kaburu ambaye ni makamu mwenyekiti wa Simba, timu pinzani na wateja wangu. Kwa hili pia naomba adhabu itenguliwe mara moja.
Utetezi wa 4: Kutompa adhabu refa.
Refa wa mchezo huo alionekana wazi kushindwa kumudu mchezo na hivyo kusababisha fujo. Mfano alimpa Niyonzima kadi kwa kosa la kumtukana, kosa ambalo ni lakufikirika zaidi na kanuni zinamtaka refa kuweka kosa hilo kwenye ripoti ili mchezaji husika achunguzwe. Refa pia alishindwa kumpa mchezaji wa Yanga, Mwasika kadi nyekundu pamoja na kumbughuzi wakati wa mchezo. Refa alishindwa kuwaadhibu wachezaji wa Yanga kwa rafu mbaya walizo kuwa wanafanya. Refa alishindwa kumpa kadi Tegete kwa kosa la kuingia uwanjani. Refa alishindwa kuwahusisha waamzi wenzake ili kuweza kufanya maamzi yasiyo na shaka n.k.
Mfano wa kesi kama hii upo, na kamati hiyo hiyo ilishawahi kuwafungia waamuzi Peter Mujaya wa Mwanza aliyechezesha mechi namba 101 kati ya JKT Ruvu Stars kwa miezi 12 kwa kushindwa kumudu mchezo, kumuondoa Isihaka katika orodha ya waamuzi kwa kushindwa kumuadhibu Mafisango ambaye alimsukuma baada ya kumuonesha kadi nyekundu Haruna Moshi wa Simba.
Ndio kusema Mu-israel Mkongo alimudu mchezo? aliwaadhibu wote waliohusika na rafu mbaya?....
Source: Waamuzi, Kamishna Waondolewa VPL
Utetezi wa 5: Ushahidi uliotumika
TFF wanadai waliweza kubaini waliofanya fujo kwa kutumia ushahidi wa video ulioonyeshwa na TV hususa ni CloudsTV ambayo ililipigia debe sana swala hilo. Katika technologia ya leo chochote kinaweza kufanyika ikiwemo ku-edit picha na video ili kujenga hoja ya jambo ambalo mwandishi wa habari anataka watazamaji waelewe. TFF inapaswa kutumia video ambazo hazija editiwa na ambazo zinatoka kwenye source ambayo haiponyeshi mgongano wa kimaslahi hata chembe kama ilivyo CloudsTV ambayo mtangazaji wake wa kipindi ni kiongozi wa Simba.
Utetezi wa 6: TFF kupuuza malalamiko ya Yanga kuhusu kuongwa kwa Refa
Wateja wangu waliwaletea malalamiko kuwa wana wasiwasi na refa wa mchezo huo ambaye anaonekana kama ameongwa na timu ya Azam ili atoe maamuzi ambayo sio sahihi. La kushangaza TFF hamkuchukua hatua yoyote na kusababisha mchezo kuvurugika. Mfano ni case ya Arsenal na Barcelona ambapo mwamuzi aliyetazamiwa kuchezesha mechi kati yao ya UCL alionekana mitaani huko kwao amevalia fulana ya Barcelona. UEFA ilisikia malalamiko hayo na kumuondoa huyo mwamzi mara moja. Najua kwa kufanya hivi kunaweza kusababisha kila timu kulalamikia mwamzi, lakini kwa kuiga wenzetu, TFF inaweza kumuondoa refa anayelalamikiwa na kuomba mlalamikaji alete ushahidi, na endapo akishindwa basi achukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kulimwa faini.
Kwa utetezi huu naomba wateja wangu waondolewe adhabu mara moja na Mwamuzi afungiwe maisha kujihusisha na mchezo tunaoupenda wa mpira wa miguu. Naomba niseme wazi kuwa hata mimi sifurahi vitendo vya kupigana uwanjani, lakini nachelea kusema kuwa TFF ndio inachochea kwa kufanya Timu na wachezaji kuona kuwa hakuna anayewasikiliza pindi wanapotoa malalamiko yao kuhusu marefa.
Napenda pia kuwaomba TFF waanzishe uchunguzi kuhusu AZAM maana imelalamikiwa na timu zaidi ya 5 kwa vitendo vyao vya kuwashawishi marefa kutoa maamuzi mabaya.
Nawasilisha utetezi.
Wakili wa Kujitolea
Kwako TFF.
Nawasilisha utetezi wangu kwako kuwahusu wateja wangu Yanga na wachezaji wake watano uliowapa adhabu hivi karibuni. Yanga anahusika kwa vile umemnyima haki ya kuwafanyisha kazi waajiriwa wake halali kwa vipindi mbali mbali.
Utetezi wa 1: Ukubwa wa adhabu
Bila kujali kama wamefanya kosa au la napenda nawasilisha utetezi kuwa adhabu uliowapa ni kubwa sana na inaonyesha kuwa na agenda nje ya kosa lenyewe. Kwa kawaida unapotaka kumhukumu mtu yeyote aliye fanya kosa, lazima utumie sheria, kanuni zilizopo bila kusahau hukumu ulizokwisha pitisha kwa wengine waliofanya makosa kama hayo. Napinga ukubwa wa adhabu kwa wachezaji wa Yanga kwa kutumia hoja ya hukumu ulizowahi kupitisha kama ifuatavyo:
1. Katika mchezo dhidi ya Simba na Oljoro JKT mchezaji Patrick Mafisango alimsukuma mwamuzi Isihaka Shirikisho baada ya kumuonesha kadi nyekundu mchezaji mwenzake Haruna Moshi. Kamati yako iliamuadhibu Mafisango kwa kuamuru simba imwandikie barua ya onyo kali kwa kitendo chake hicho ambacho kinafanana sana na hiki cha wateja wangu. Source:Mafisango Aonywa, Simba Yapigwa Faini . Au tuseme ni kwa vile ulikosa ushahidi wa video kutoka redio clouds ukimuonyesha mafisango akikimbia kutoka mbali sana kama alivyofanya mchezaji wa Yanga, na kuja kumsukuma mwamuzi?
2: KIPA Juma Kaseja wa timu ya Simba alionyesha utovu wa nidhamu cha kugoma kupeana mkono na aliyekuwa mgeni rasmi katika mechi ya Simba na Yanga iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Kamati yako ilimuadhibu kwa kumfungia mechi tatu na faini ya shs 500,000. Ndio tuseme Refa ni zaidi ya mgeni rasmi?
3. Mchezaji Aziz Sibo wa African Lyon alifungiwa kutocheza mechi tatu na faini ya sh 500,000 kwa kosa la kumtandika kichwa mchezaji wa Polisi ya Dodoma
source:TFF yatoa adhabu kwa watovu wa nidhamu
Kesi kama hizi ziko nyingi ambazo kumbukumbu zake unazo. Kwa hoja hii naomba utengue uamzi wako wa kuwafungia wachezaji wa Yanga zaidi ya mechi tatu.
Utetezi wa 2: Kuwanyima nafasi ya Kujitetea
Ni kitendo cha haki kumsikiliza mtuhumiwa kabla ya kumpa adhabu. Kitendo hiki sio tu kinatoa haki bali pia uwezesha wenye mamlaka kugundua tatizo la ndani ambalo ni kiini cha tatizo lililotokea. Kwa vile wateja wangu hawakupata haki hiyo naomba utengue hukumu yako mara moja.
Hii ni sawa na kesi iliyokuwa inawahusu Rage na Sendeu kwa kitendo chao kilichodhaniwa ni kuhujumu mechi. Pamoja na kwamba walisikika redioni wakieleza nia ya kugomea mchezo bado kamati ya Tibaigana iliwataka walete maelezo ya kujitetea kabla ya kuwahukumu.
Source:Tibaigana kuwahoji Rage, Sendeu
Utetezi wa 3: Uhalali wa Kamati iliyotoa hukumu.
Kamati iliyotoa hukumu ni kamati ya ligi ambayo hata kama inayo mamlaka bado ina wajumbe ambao wana Conflict of Interest katika hili swala, mfano Nyange Kaburu ambaye ni makamu mwenyekiti wa Simba, timu pinzani na wateja wangu. Kwa hili pia naomba adhabu itenguliwe mara moja.
Utetezi wa 4: Kutompa adhabu refa.
Refa wa mchezo huo alionekana wazi kushindwa kumudu mchezo na hivyo kusababisha fujo. Mfano alimpa Niyonzima kadi kwa kosa la kumtukana, kosa ambalo ni lakufikirika zaidi na kanuni zinamtaka refa kuweka kosa hilo kwenye ripoti ili mchezaji husika achunguzwe. Refa pia alishindwa kumpa mchezaji wa Yanga, Mwasika kadi nyekundu pamoja na kumbughuzi wakati wa mchezo. Refa alishindwa kuwaadhibu wachezaji wa Yanga kwa rafu mbaya walizo kuwa wanafanya. Refa alishindwa kumpa kadi Tegete kwa kosa la kuingia uwanjani. Refa alishindwa kuwahusisha waamzi wenzake ili kuweza kufanya maamzi yasiyo na shaka n.k.
Mfano wa kesi kama hii upo, na kamati hiyo hiyo ilishawahi kuwafungia waamuzi Peter Mujaya wa Mwanza aliyechezesha mechi namba 101 kati ya JKT Ruvu Stars kwa miezi 12 kwa kushindwa kumudu mchezo, kumuondoa Isihaka katika orodha ya waamuzi kwa kushindwa kumuadhibu Mafisango ambaye alimsukuma baada ya kumuonesha kadi nyekundu Haruna Moshi wa Simba.
Ndio kusema Mu-israel Mkongo alimudu mchezo? aliwaadhibu wote waliohusika na rafu mbaya?....
Source: Waamuzi, Kamishna Waondolewa VPL
Utetezi wa 5: Ushahidi uliotumika
TFF wanadai waliweza kubaini waliofanya fujo kwa kutumia ushahidi wa video ulioonyeshwa na TV hususa ni CloudsTV ambayo ililipigia debe sana swala hilo. Katika technologia ya leo chochote kinaweza kufanyika ikiwemo ku-edit picha na video ili kujenga hoja ya jambo ambalo mwandishi wa habari anataka watazamaji waelewe. TFF inapaswa kutumia video ambazo hazija editiwa na ambazo zinatoka kwenye source ambayo haiponyeshi mgongano wa kimaslahi hata chembe kama ilivyo CloudsTV ambayo mtangazaji wake wa kipindi ni kiongozi wa Simba.
Utetezi wa 6: TFF kupuuza malalamiko ya Yanga kuhusu kuongwa kwa Refa
Wateja wangu waliwaletea malalamiko kuwa wana wasiwasi na refa wa mchezo huo ambaye anaonekana kama ameongwa na timu ya Azam ili atoe maamuzi ambayo sio sahihi. La kushangaza TFF hamkuchukua hatua yoyote na kusababisha mchezo kuvurugika. Mfano ni case ya Arsenal na Barcelona ambapo mwamuzi aliyetazamiwa kuchezesha mechi kati yao ya UCL alionekana mitaani huko kwao amevalia fulana ya Barcelona. UEFA ilisikia malalamiko hayo na kumuondoa huyo mwamzi mara moja. Najua kwa kufanya hivi kunaweza kusababisha kila timu kulalamikia mwamzi, lakini kwa kuiga wenzetu, TFF inaweza kumuondoa refa anayelalamikiwa na kuomba mlalamikaji alete ushahidi, na endapo akishindwa basi achukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kulimwa faini.
Kwa utetezi huu naomba wateja wangu waondolewe adhabu mara moja na Mwamuzi afungiwe maisha kujihusisha na mchezo tunaoupenda wa mpira wa miguu. Naomba niseme wazi kuwa hata mimi sifurahi vitendo vya kupigana uwanjani, lakini nachelea kusema kuwa TFF ndio inachochea kwa kufanya Timu na wachezaji kuona kuwa hakuna anayewasikiliza pindi wanapotoa malalamiko yao kuhusu marefa.
Napenda pia kuwaomba TFF waanzishe uchunguzi kuhusu AZAM maana imelalamikiwa na timu zaidi ya 5 kwa vitendo vyao vya kuwashawishi marefa kutoa maamuzi mabaya.
Nawasilisha utetezi.
Wakili wa Kujitolea