Uteuzi wa Job Masima kuwa Balozi Israel ni ishara ya Rais Magufuli kuinoa na kuiimarisha TISS

Uteuzi wa Job Masima kuwa Balozi Israel ni ishara ya Rais Magufuli kuinoa na kuiimarisha TISS

ni muda sasa umepita tokea tupate uhuru, nchi za wenzetu ikiwemo china waliwatumia wanausalama wao kujiimarisha kiuchumi lakini kama hawa Tiss hawapo chini ya chama kilichopo madarakani ni lipi walilolifanya kutuimarisha kiuchumi?

Hapana, labda hujafuatilia jinsi China ilivyochukua maamuzi magumu kufikia hapo ilipo leo.

Ni chama cha kikomunisti cha China ndicho chanzo na kichocheo cha China uionayo leo.
 
Ungeipenda nchi yako unavyosema usingelaumu kwa hiyo style. Typically wewe ni antagonist na hata ufanyiwe nini utalalamika tu kama mlivozoea. Pia nakusihi usipende kusema unaipenda nchi yako ili kufurahisha watu au keyboard warriors. Kuipenda nchi kwa watu wengine ina maana kubwa so please dont make it look so cheap.
 
Makala ndefu ila hukuweka ataisadiaje na utayari wa israel katika hilo.
Mimi nadhani njia nzuri ni kuweka bajeti ya kuwapeleka vijana kusoma nchi mbali mbali kutokana na hitajio.
Huwezi ukautoa usalama wa nchi kwa taifa moja na kusaidiwa...
Ukumbuke israel ni kama US haina rafiki wa kudumu wao wanaweka maslahi yao kwanza..
Na pia isreal wanatania ya kupandikizw chuki pale nchi ikiwa ina dini mbili hizi...
Ni vizuri kuwa na uhusiano ndio utandawazi lakini kama taifa uasalama wetu ni wetu wenyewe haihusu taifa jengine.
Sasa hivi hii Tiss inatakiwa iwe na vijana wabobezi wa investigation katika mamno ya uchumi , makampuniya kimataifa, mfumo wa biashars za maguta na gesi..
Yuwe na vijana ambao ukiwapa file kuhusu kampuni fulani inayo taka kuja kuwekeza wanakupa data zote mesani...
Au vijana ambao ukitaka kumchagua mtu kuwa kiongozi wanakuoa data za uhakika kuanzia kolomije mpaka moshi ushirika...
 
Tanzania tayari ina mahusiano ya kibalozi na Marekani, UK, Russia, France, China, Germany na kadhalika na kadhalika.

Israel ni cha mtoto katika kila eneo ukiilinganisha na hayo ma nchi, mbona hiyo TISS ya Bongo miaka yote hiyo haijasaidiwa?

Haya ni ma imani ya the Christian right wanaoamini biblia is literally true. Kama unaamini biblia is literally true basi Israel ni nchi ya ahadi, taifa teule ambalo ndio bingwa wa kila kitu ulimwenguni.

Theological baloney. Mashudu!
 
Makala ndefu ila hukuweka ataisadiaje na utayari wa israel katika hilo.
Mimi nadhani njia nzuri ni kuweka bajeti ya kuwapeleka vijana kusoma nchi mbali mbali kutokana na hitajio.
Huwezi ukautoa usalama wa nchi kwa taifa moja na kusaidiwa...
Ukumbuke israel ni kama US haina rafiki wa kudumu wao wanaweka maslahi yao kwanza..
Na pia isreal wanatania ya kupandikizw chuki pale nchi ikiwa ina dini mbili hizi...
Ni vizuri kuwa na uhusiano ndio utandawazi lakini kama taifa uasalama wetu ni wetu wenyewe haihusu taifa jengine.
Sasa hivi hii Tiss inatakiwa iwe na vijana wabobezi wa investigation katika mamno ya uchumi , makampuniya kimataifa, mfumo wa biashars za maguta na gesi..
Yuwe na vijana ambao ukiwapa file kuhusu kampuni fulani inayo taka kuja kuwekeza wanakupa data zote mesani...
Au vijana ambao ukitaka kumchagua mtu kuwa kiongozi wanakuoa data za uhakika kuanzia kolomije mpaka moshi ushirika...

Tuko pamoja mkuu maana kabla ya serikali ya awamu ya 5 huko nyuma kwenye kutiliana saini mikataba mwekezaji anaweza kusema ana assets au hiki na kile huko watokako.

Lakini kama huna vijana na nyenzo za kufuatilia kampuni zinazotaka kuingia mikataba kama ya uchimbaji madini basi yanatokea sasa hivi kwenye suala la makontena ni kielelezo tosha kwamba kuna mahitaji katika hilo.

Pia, hata suala la ulinzi wa viwanja vya ndege ni wazi kuwa vijana wamepwaya sana kwenye kuchunguza aingiaye na atokae nchini mwetu awe na madini au mchanga.
 
Balozi Job Masima ameanza kazi rasmi ya kuiwakilisha Tanzania nchini Israel akiwa balozi wa kwanza nchini humo tangu Tanzania (wakati huo ikiitwa Tanganyika) ivunje uhusiano wake na taIfa hilo teule yapata miaka 43 ilopita.

Ni mmoja wa mabalozi waloapishwa jana Ikulu kabla ya kwenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Ujerumani, Israel na Oman.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya mahusiano kati ya nchi hizo mwezi October mwaka 2015 aliekuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alimkaribisha balozi wa Israel bwana Yahel Vilan alipokwenda kukabidhi hati za utambulisho tayari kuridhia mahusiano ya kimataifa kwa nchi hizi mbili.

Baada ya raisi John Magufuli kuingia madarakani mwezi January mwaka jana Balozi Vilan alimtembelea raisi Magufuli na kumhakikishia uhusiano huo kwamba upo na kusisitiza kwamba Israel itafungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.

Raisi John Magufuli nae akamhakikishia balozi Vilan kwamba Tanzania ilikuwa mbioni kuhakikisha inakuwa na ubalozi mjini Tel Aviv.

Baada ya Tanzania kupata uhuru wake December 1 mwaka 1961, Tanzania ilifungua ubalozi wake nchini Israel lakini makazi yakiwa nchini Misri.

Mwaka 1973 umoja wa nchi za kiafrika uliamua kujitenga na Israel baada ya nchi hiyo kuwa inaitawala Palestina kwa kuwa na sera za kibaguzi na za kuitenga Palestina na kuizuia kuvuka ukanda wa Gaza.

Lakini pia sababu ingine ilikuwa ni khasa baada ya vita ya Yom Kippor ambapo mataifa sita ya kiarabu yakiongozwa na Misri na Syria yalikuwa yakipigana vita na Israel katika milima ya Golan na Sinai.

Kusudio ya vita hiyo ilikuwa ni kuyakomboa maeneo hayo kutoka kwa Israel ambayo iliyateka baada ya vita ilojulikana kama "six days war" ya mwaka 1967 na pia raisi wa Misri Anwar Sadat alikuwa na mpango wa kufungua mfereji wa Suez.

Pamoja na hayo uhusiano wa nchi hizi haukuwa umezimwa moja kwa moja na ilipofikia mwaka 1995 mahusiano kati ya nchi hizi yalirudishwa na Tanzania ikarejesha ubalozi wa Tanzania Israel lakini makazi yakiwa nchini Misri na Israel ikawa na ofisi ya ubalozi mjini Nairobi nchini Kenya.

Tanzania na Israel walikuwa wakishirikina katika miradi mbalimbali na mmojawapo ni mradi mkubwa wa Bugando nchini Mwanza na miradi mingine.

Mwezi Julai mwaka jana Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alihudhuria mkutano wa viongozi wa nchi za Afrika Mashariki ulofanyika nchini Uganda na akakabidhiwa barua rasmi na waziri wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa na kikanda Dr Augustine Mahiga, kutoka kwa raisi John Magufuli.

Katika barua hiyo raisi Magufuli alimweleza waziri mkuu Netanyahu kwamba Tanzania ilikuwa imeamua kufungua rasmi ofisi ya ubalozi nchini Israel.


Dr Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri mkuu wa Israel mjini Entebbe mwezi julai mwaka 2016. (Picha na Kobi Gideon wa GPO)

Israel inajulikana duniani kwa kuwa wataalam kwenye maeneo ya kilimo na umwagiliaji, Israel ina kiwanda kikubwa cha plastiki kijulikanacho kama Plazit Polygal Group ambacho kina wafanyakazi wapatao 500 na kinapata faida ya mauzio kiasi cha doka milioni 250 kwa mwaka.

Pia Israel inajulikana duniani kwa utengenezaji bidhaa mbalimbali za kiteknolojia zikiwemo satellite, silaha za kivita kama makombora na ndege zijiendeshazo zenyewe au Drones.

Lakini kikubwa zaidi ni kuhusu jeshi la Israel ambalo mpaka kufikia mwaka 2015 matumizi ya jeshi la Israel yaani "military expenditure" nchi hiyo ni ya 15 duniani huku ikiwa ni nchi ya 8 kwa uuzaji wa silaha duniani.

Lakini asilimia 20 ya bajeti ya ulinzi ya nchi hiyo inatolewa na Marekani sawa na dola bilioni 3.8 kwa mwaka baada ya kutiliana saini mkataba utakaokuwa ni wa mwaka 2018 hadi 2028.

Lakini uteuzi wa balozi Job Masima hauwezi kupita bila kuangaliwa kwa jicho la tatu kwani unaelekeza wadadisi kuona kwamba ni uteuzi wa kimkakati zaidi.

Kabla ya uteuzi wa balozi Masima, alikuwa ni katibu mkuu wizara ya Ulinzi na jeshi la kujeng taifa nafasi ambayo aliichukua mwaka 2011 alopoteuliwa na aliekuwa raisi wa serikali ya awamu ya nne Jakaya Kikwete.

Lakini balozi Job Masima ni mmoja wa watu muhimu sana katika kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania, akiwa tayari amekaa sehemu mbalimbali za ulinzi na usalama, raisi Magufuli ameamua kumpa majukumu ya kuimarisha uhusiano wake na Israel lakini kukiwa na malengo maalum.

Raisi John Magufuli ametambua haja ya kuimarisha idara ya ujasusi Tanzania TISS na amekusudia kuiimarisha kiutawala na kiutendaji ambapo vijana wengi sasa wanapata nafasi za kujiendeleza zaidi na kijifunza mbinu mpya za ulinzi wa taifa khasa katika ulimwengu wa leo ambao umejaa mikikimikii ya kila aina.

Hapo ndipo unapokuja kuwaamini Israel katika masuala ya ulinzi na usalama kwani wana msemo wao ambao unasema kwa kiingereza kwamba "Security is a subject that can be taught theoretically, but nothing is a substitute for a real hands-on experience and we've got lots of it."- yaani wakimaanisha kwamba usalama ni somo ambalo laweza kufundishwa kinadharia, lakini hakuna mbadala wa mikono halisi yenye uzoefu ambayo tunayo mingi tu.

Ni dhahiri kuwa yanayojiri leo hii ni pamoja na nafasi pana ya mawasiliano kati ya maofisa, muunganiko yaani "coordination" kati ya idara na idara na uimarishaji wa "kitengo" ambacho ndicho kiko katika ngazi ya juu kabisa ya uangalizi wa taifa hili.

Bila shaka Israel inatusaidia katika nyanza mbalimbali za ulinzi na usalama, uchumi na maendeleo mengine kwa ujumla, lakini Amani na ulutivu na ustawi wa watanzania unahitaji ulinzi na usalama imara.

Ulinzi na usalama imara ndiyo nguzo ambayo inahitaji kuboreshwa kwa gharama yoyote ile na hiyo ni moja ya mipango ya serikali ya awamu ya tano.

Waweza kupata mwanga wa nini nimekusudia katika Makala hii ndogo kwa kujikumbusha Makala hizo hapo chini, lakini wenzangu wadadisi wa masuala ya ujasusi kama mkulu Yeriko Nyerere naomba michango yenu kwa kuongezea nyama kwenye hili.

Je, raisi John Magufuli anajimaarisha kiusalama zaidi au anaisuka zaidi TISS?

Je, balozi Job Masima ana cheo gani kijeshi?

https://www.jamiiforums.com/threads...kuwa-kwa-kasi-je-tanzania-iko-tayari.1098506/

https://www.jamiiforums.com/threads...kitine-waasisi-wa-tiss-imara-tanzania.966599/

https://www.jamiiforums.com/threads/hili-ni-jaribio-jingine-kwa-system-state-au-kitengo.896405/
Asante hii ni fursa njema kama taifa kuvuna ujuzi wa intelligence kutoka kwa hawa wenzetu
 
Tanzania tayari ina mahusiano ya kibalozi na Marekani, UK, Russia, France, China, Germany n kadhalika na kadhalika.

Israel ni cha mtoto katika kila eneo ukiilinganisha na hayo ma nchi, mbona hiyo TISS ya Bongo miaka yote hiyo haijasaidiwa?

Haya ni ma imani ya the Christian right wanaoamini biblia is literally true. Kama unaamini biblia is literally true basi Israel ni nchi ya ahadi, taifa teule ambalo ndio bingwa wa kila kitu ulimwenguni.

Theological baloney. Mashudu!

Nadhani hujasoma na kuelewa kwa undani nilichokieleza, yaani pengine unahitaji akili za ziada.

Mtu unaweza kuwa una shahada ya chuo kikuu lakini katika kujadili masuala ya msingi na muhimu kabisa ambayo mara nyingi yanahitaji kutumia welevu au "intelligence" ukajikuta unafeli.

Na kutumbuliwa kwa profesa Ntalikwa leo pale wizara ya nishati na madini ni mfano tosha wa ninachomaanisha.

Security is a subject that can be taught theoretically, but nothing is a substitute for a real hands-on experience and we've got lots of it."-
 
Nadhani hujasoma na kuelewa kwa undani nilichokieleza, yaani pengine unahitaji akili za ziada.

Mtu unaweza kuwa una shahada ya chuo kikuu lakini katika kujadili masuala ya msingi na muhimu kabisa ambayo mara nyingi yanahitaji kutumia welevu au "intelligence" ukajikuta unafeli.

Na kutumbuliwa kwa profesa Ntalikwa leo pale wizara ya nishati na madini ni mfano tosha wa ninachomaanisha.

Security is a subject that can be taught theoretically, but nothing is a substitute for a real hands-on experience and we've got lots of it."-


Anhaa, mimi nahitaji akili za ziada? Okay.

Kwanza acha ku speculate na kutudanganya sababu ya Profesa Ntalikwa kutumbuliwa Nishati, hujui! Nobody knows, msomi hafanyi fanyi ma wild speculation kama hayo kwamba Ntalikwa ameshindwa ukatibu mkuu kwa sababu hawezi kujadili masuala muhimu japo kasoma. Such ridiculous, wild and woolly conclusions.

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania basi unatakiwa kujua kwamba teua-tengua za utawala huu ziko erratic and inexplicable, hazielezeki, and sometimes vindictive, visasi, kama Nape. TRA, kwa mfano, ina mabosi wangapi toka JPM achukue nchi, kwa nini hafanyi thorough vetting and prior perfomance evaluation of his nominees?

Hakuna teuzi za JPM ambazo ni thought through and strategic. Balozi wa Israel kachaguliwa kwa mtindo wa random draws.

Israel ni nchi ya kawaida tu, ila nyinyi ambao mnasema the bible is literally true then of course Israel ndio mwisho wa kila kitu. Incredibly feeble mind.


 
Makala ndefu ila hukuweka ataisadiaje na utayari wa israel katika hilo.
Mimi nadhani njia nzuri ni kuweka bajeti ya kuwapeleka vijana kusoma nchi mbali mbali kutokana na hitajio.
Huwezi ukautoa usalama wa nchi kwa taifa moja na kusaidiwa...
Ukumbuke israel ni kama US haina rafiki wa kudumu wao wanaweka maslahi yao kwanza..
Na pia isreal wanatania ya kupandikizw chuki pale nchi ikiwa ina dini mbili hizi...
Ni vizuri kuwa na uhusiano ndio utandawazi lakini kama taifa uasalama wetu ni wetu wenyewe haihusu taifa jengine.
Sasa hivi hii Tiss inatakiwa iwe na vijana wabobezi wa investigation katika mamno ya uchumi , makampuniya kimataifa, mfumo wa biashars za maguta na gesi..
Yuwe na vijana ambao ukiwapa file kuhusu kampuni fulani inayo taka kuja kuwekeza wanakupa data zote mesani...
Au vijana ambao ukitaka kumchagua mtu kuwa kiongozi wanakuoa data za uhakika kuanzia kolomije mpaka moshi ushirika...

Hii ndio intellegency tunayoihitaji sio ile ya kutoa kucha watu wanaosema ukweli!
 
Mkuu umeleta uzi mzuri sana, Mkuu ana nia ya dhati kabisa ya kuumarisha taasisi yetu hii ya Usalama ambayo kiuhalisia imekuwa iko operate locally sana na haitakii kubadilika kwa mwavuli tu wa kuwa utendaji wao ni secret Mheshimiwa JPM alianza kuonesha nia ya ya dhati pale tu alipo mteua Modestus kipilimbi kama GD wa idara Kumuweka tu mtu ambae ni professional wa Computer science basi kutamfanya aipelekee idara Kisasa kabisa , Mbinu za Intelligence karibia katika agency zote ni Moja tunachozidiana Ni technology leo ukiangalia M15 ya uk au FBI utaona wanapopishana ni Tech tu, Uteuzi huo wa Job masima kama Balozi utaleta matokeo chanya katika kujifunza na kupata mapya juu ya usalama Huko.
Ni kweli Israel inaongoza katika teknnologia na ukiangalia tech security companies za Israel ndizo zenye tenda nyingi sana Ulimwenguni. Ushauri wangu waanze na mradi wa NIDA ambao naamini kwa kuwa Modestus anaufahamu fika ni eneo ambalo mchango wao unaweza kuwa wa manufaa sana kwetu. Mradi huu una impact kubwa sana kwenye ustawi wa Uchumi wa nchi yetu kwa ujumla. Pili kwenye kilimo na Umwagiliaji wako mbali sana. Israel ni almost jangwa lakini huwezi kuamini mazao ya kilimo yanayotoka kwenye jangwa hilo. Ukiona swimming pools zilizoko Tel Aviv utafikiri hawa jamaa wana mito kama huku kwetu. Tatu ni kuhusu Elimu, maandalizi yafanywe kuanza kuwaandaa wanafunzi kusoma na kujua Kiyahudi kwani ukitaka kupata Elimu nzuri Israel ni kwenye vyuo vyao ambavyo sharti moja kubwa ni ujue kiyahudi.
 
Mbona Trainers wao wengi huwa wanatokea huko huko Israel na mara nyingi Wajanja huwa tunagongana nao sana pale JNIA wakiwa wanakuja kuwafunza Vijana katika Vyuo vyao? Sasa unaposema kuwa Ubalozi umeanzishwa ili kuiimarisha hiyo idara unataka kutuambia nini labda ambacho hatukijui?

Nakumbuka mwaka juzi Trainer mmoja ( najua Vijana wa Idara mliokuwa zamu pale JNIA ) mtakumbuka baada ya huyu Trainer wa Kiyahudi kutoka Mossad alipokuwa anaingia aliambiwa akaguliwe vitu vyake lakini akakataa kata kata na Jamaa walipozidi kumlazimisha akatishia kugeuza na kurudi Kwao ndipo ikapigwa Simu Magogoni kwa Mkwere na Chuoni baada ya hapo ikatoka tu amri kuwa aruhusiwe kupita na asikaguliwe Jamaa akaingia nchini kweli na kutufundishia Vijana kwa wiki mbili tu lakini waliofunzwa wanasema mafunzo yake utadhani ni ya mwaka na baadae akaondoka zake.

Hii story yako ulitaka kutueleza nini?/? Maana hujaeleweka

Nyie vijana Wa Lumumba very bogus kabisa

Aliwafundisha nini?
 
Anhaa, mimi ninahitaji akili za ziada? Okay.

Kwanza acha ku speculate na kutudanganya sababu ya Profesa Ntalikwa kutumbuliwa Nishati, hujui! Nobody knows, msomi hafanyi fanyi ma wild speculation kama hayo kwamba Ntalikwa ameshindwa ukatibu mkuu kwa sababu japo kasoma hawezi kujadili masuala muhimu. Such ridiculous, wild and woolly conclusions.

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania basi unatakiwa kujua kwamba teuzi na tengua za utawala huu ziko erratic and inexplicable, hazielezeki, and sometimes vindictive, visasi, kama Nape. TRA, kwa mfano, ina mabosi wangapi toka JPM achukue nchi, kwa nini hafanyi thorough vetting and prior perfomance evaluation of his nominees?

Hakuna teuzi za JPM ambazo ni thought through and strategic. Balozi wa Israel kachaguliwa kwa mtindo wa random draws.

Israel ni nchi ya kawaida tu, ila nyinyi ambao mnasema the bible is literally true then of course Israel ndio mwisho wa kila kitu. Incredibly feeble mind.


Naona kama imani yako ni mlengo wa kigaidi.acha kudharau imani za watu we mzee wa kitabu
 
Back
Top Bottom