Uteuzi wa Meneja wa Maji Dodoma watenguliwa

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Waziri wa Maji, Jumaa H. Aweso ametengua uteuzi wa Meneja wa Maji Mkoa wa Dodoma, (RUWASA) Mhandisi Godfrey Kabula Mbabaye, Aweso amechukua hatua hiyo kwa Mamlaka aliyonayo kupitia Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019, kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Aidha, Waziri Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba kunda timu ya Wataalam ya kufuatilia changamoto ya utekelezaji wa Miradi ya Maji kwa Mkoani Dodoma na kutoa suluhisho la kumaliza changamoto hizo mara moja.

Vilevile, ameelekeza timu hiyo ya Wataalam itakayoundwa na katibu Mkuu ifanye tathimini ya utendaji kazi wa Mameneja wa Wilaya zote wa Maji Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Dodoma.

Chanzo: Millard Ayo
 
Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa H. Aweso (Mb) ametengua uteuzi wa Meneja wa Maji Mkoa wa Dodoma, (RUWASA) Mhandisi Godfrey Kabula Mbabaye kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Waziri Aweso amechukua hatua hiyo kwa Mamlaka aliyonayo kupitia Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019,

Aidha, Waziri Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba kuunda timu ya Wataalam ya kufuatilia changamoto ya utekelezaji wa Miradi ya Maji kwa Mkoani Dodoma na kutoa suluhisho la kumaliza changamoto hizo mara moja.

Vilevile, ameelekeza timu hiyo ya Wataalam itakayoundwa na katibu Mkuu ifanye tathimini ya utendaji kazi wa Mameneja wa Wilaya zote wa Maji Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Dodoma.

 
Saa100 yuko wapi? Xiara kama hizi JPM alikuwa anamaliza hapo hapo kutumbua.
Sasa kutumbua lazima katibu mkuu alalamike then waziri aitwe ndio waziri atumbue? Hizo fedha za miradi hsmjui ni za wananchi wa maeneo husika?
 
Hadi karine hizi bado Mameneja wana teuliwa badala ya watu kutuma CV na kufanyiwa usaili? Nchi imejaaa wajinga sana hii
 
Saa100 yuko wapi? Xiara kama hizi JPM alikuwa anamaliza hapo hapo kutumbua.
Sasa kutumbua lazima katibu mkuu alalamike then waziri aitwe ndio waziri atumbue? Hizo fedha za miradi hsmjui ni za wananchi wa maeneo husika?
Mameneja kuendelea kuteuliwa aina ya ujinga
 
Huyo Aweso amewahi kutoa kauli yoyote kuhusu uuzwaji wa bandari zote?
 
Hivi haya mambo mengine hayawezi kusubiri tukamaliza swala la bandari kwanza?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…