Uthubutu: Kijana atakayeelezea jinsi atakavyoizalisha elfu 50 ndani ya mwezi mmoja nitamkopesha bila riba

Uthubutu: Kijana atakayeelezea jinsi atakavyoizalisha elfu 50 ndani ya mwezi mmoja nitamkopesha bila riba

Idea ya biashara|| juice za u-fresh

Maeneo ya biashara|| shule za msingi

Mchanganuo wa biashara:
Box za u- fresh (caton)
each 4,500×3= 13,500
box moja linakaa u - fresh 60
Dell la kuhifadhia u-fresh - 20,000
Pesa ya kulipia kugandishiwa - 2000
Jumla 13,500+20,000+2,000= 35,500
Mtaji 50,000-35,500= 14,500
14,500 utatumia kwa ajili ya chakul na maji mwanzoni mwa biashara

Matokeo:
Unaweza kuuza box tatu kwa siku 1
Kila u-fresh moja ni shillingi 100
Gharama ya box tatu ni shillingi 13,500

Box tatu- 60×3=180
180×100(shilingi)= 18,000 shilingi
Gharama ya box = 13,500
Kugandishiwa = 2,000
Faida = 3500
Kwa mwezi 3,500×30= 105,000

[emoji769]Fenisher

Sent using Jamii Forums mobile app
faida yake ndogo sana na inaumiza yani box moja unapata 1,500/= but gud idea though!!
 
Hongera kwa wazo lako pia shukrani kwa kuutambua mchango wangu mpaka kuuweka kwenye top ten yako,,
Hongera kwa mshindi na waliotoa mawazo yao kwa uwazi bila choyo

Nishauri tu hii kitu iwe endelevu na watakaofanyia kazi baadhi ya mawazo yaliyotolewa humu walete mrejesho, hata kama itakuwa negative ili tuzijue changamoto za mawazo husika maana tunajua kuandika wazo na kulitekeleza mara nyingi havifanani

Mi nitaendelea kuandika fursa kadri nitakavyokuwa nakutana nazo huko mahangaikoni
Mimi si tajiri ila nataka kuwafundisha utu na ubinadamu matajiri walioko JF.

Nataka kijana mwaminifu mmoja kutoka Jf nimwazime 50 na airejeshe baada ya mwezi mmoja au miwili ili nimwazime mwingine.

Changanua wazo lako na weka namba ya simu kama utapenda kuiweka hapa Kisha members wengine watanisaidia kumchagua mtu sahihi.

Please huu sio mkopo kwa wanaojiweza kwa sababu hauna riba na utakuwa umedhulumu haki ya mwingine.

Masharti na vigezo vitazingatiwa. Mshindi atatakiwa kusubmit some of his/ her details PM.

Pesa nitamtumia au kumkabidhi Ijumaa 21/ Febuari/2020.

Shindano litadumu kwa siku 3 tu.


UPDATES
23:15 Jumatano, nimefunga shindano
Nashukuru kwa mliojitokeza kuwania hichi kiasi kidogo cha 50.
Niko busy kidogo na majukumu na washiriki ni wengi.
Ninaomba Jumamosi weekend ndio nipitie post to post ili kuleta haki.
Mshindi atatangazwa na nitampa pesa mkononi kama yuko Dar na kama yuko mkoani nitamtumia na ya kutolea.
Kila mwezi nitafanya kitu hichi na atakayetengeneza faida kubwa zaidi nitampa Pesa nyingi zaidi.

UPDATES
JUMAMOSI SAA 2:50 ASUBUHI
Nimeanza kufanya sorting,niko page number 3,leo hii hii mshindi atatangawa.

UPDATES
09:15 AM
Nimemaliza uchambuzi wa awali na kupata post 22 zenye nguvu zaidi.
Nakunywa chai kisha nimalizie kusort na kupata vijana 3 nitakaowaleta yenu, asanteni.

Updates
09:48 am
Saturday
Nimepata watu hawa, na uchambuzi unaendelea miongoni mwao.
Kama kuna mtu hajatendewa haki anaruhusiwa kuleta malalamiko within one hour.
Walioingia kwenye kinyang'anyiro ni;
1.Zero IQ post no.29
2.Zwenge Ndaba post no.
3.Noelia, post no.170
4.CONTROLA post no.175
5.Davie post no.236
6.Naipenda Familia yangu, post.#57
7.Peramiho Yetu post #30
8.FK21 post #147.

Updates
1930 hrs
Ninaomba radhi kwa kuchelewesha matokeo ya mwisho.
Sikuwa hewani kwasababu zilizo nje ya uwezo.
But nikitulia nitamaliza kazi leo hii hii na mhusika atapewa chake kwa kadri tutakavyokubaliana njia ya kumfikishia Pesa yake.

Updates
23: 50
Nawashukuru washiriki wote wa shindano hili dogo.
Ninatamani kila mshiriki nimpe pesa nyingi kwaajili ya wazo lake ila kamba yangu ni fupi.
Nawashukuru pia wasomaji na wachangiaji wa Uzi huu.
Washindi ni hawa wafuatao;
3: Zwenge Ndaba, katika post yake #208 inayoelezea biashara ya maziwa kutoka Chalinze kwenda Kibaha au Dar es salaam.
2.Peramiho Yetu, katika post yake #30 anaelezea biashara ya Mahindi mabichi ya kuchoma kutoka Stereo Temeke .
1:Napenda Familia Yangu, katika post yake #57 ameelezea biashara ya maandazi na half cake .
Mimi kwasasa nitaanza na kutoa zawadi kwa mshindi nambari 1.
Kwa atakayekuniunga mkono anaweza kuungana nami kuwapa mtaji washindi nambari 2 & 3 au kumwongezea mtaji mshindi nambari moja.
Note:
Nitaendeleza hili jambo kila baada ya mwezi mmoja na ninawashauri watakaokosa wajaribu tena.
Mshindi anione pm

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa wazo lako pia shukrani kwa kuutambua mchango wangu mpaka kuuweka kwenye top ten yako,,
Hongera kwa mshindi na waliotoa mawazo yao kwa uwazi bila choyo

Nishauri tu hii kitu iwe endelevu na watakaofanyia kazi baadhi ya mawazo yaliyotolewa humu walete mrejesho, hata kama itakuwa negative ili tuzijue changamoto za mawazo husika maana tunajua kuandika wazo na kulitekeleza mara nyingi havifanani

Mi nitaendelea kuandika fursa kadri nitakavyokuwa nakutana nazo huko mahangaikoni

Sent using Jamii Forums mobile app
Thanks a lot
 
Biashara ya maziwa ,Kuna sehemu chalinze wanauza Lita 1 elfu moja
Mchanganua kwa elfu 50
Lita 40@1000=40000
Dumu la Lita 50=3000
Nauli =7000
Apo elfu hamsini inakua imekwisha
Maziwa kwa dar Lita moja 2000 mpaka 1500
Kwa kua Lita hamsini ni kidogo ,sio lazima kufikisha mzigo dar.unaweza uzia kibaha kwa Kila lita 1500
Faida 20000 kwa siku.ukiuza dar kwa 2000 kwa Lita ,faida 40000 kwa siku.
Nikiikosa 50000 hiyo ,kutakua na mkono wa mtu
Hongera kwa ushindi mkuu, ningependa kufahamu namna unavyouza hayo maziwa, ni kwamba unakuwa na kijiwe unaweka kambi au unawafuata watu vijiweni unakuwa unawauzia kama vile wanavyouza wale jamaa wa kahawa...


Na hayo maziwa yanakuwa ni fresh au mtindi, kama siyo mtindi yanapokuwa hujauza yote yanayobaki unafanyaje, na kama ni ya mtindi unafanya vipi kuyaweka katika hali ya ubaridi. Nitashukuru nikipata ufafanuzi
 
Hongera kwa ushindi mkuu, ningependa kufahamu namna unavyouza hayo maziwa, ni kwamba unakuwa na kijiwe unaweka kambi au unawafuata watu vijiweni unakuwa unawauzia kama vile wanavyouza wale jamaa wa kahawa...


Na hayo maziwa yanakuwa ni fresh au mtindi, kama siyo mtindi yanapokuwa hujauza yote yanayobaki unafanyaje, na kama ni ya mtindi unafanya vipi kuyaweka katika hali ya ubaridi. Nitashukuru nikipata ufafanuzi


Jinsi alivyoandika inaonekana ameamua kushare .sio kitu anachofanya...nimewaza hvyo!na mshindi ilisemekana ni yule anayetaka anza na sio aliye na business!
Hongera@zwangedaba
 
Mimi si tajiri ila nataka kuwafundisha utu na ubinadamu matajiri walioko JF.

Nataka kijana mwaminifu mmoja kutoka Jf nimwazime 50 na airejeshe baada ya mwezi mmoja au miwili ili nimwazime mwingine.

Changanua wazo lako na weka namba ya simu kama utapenda kuiweka hapa Kisha members wengine watanisaidia kumchagua mtu sahihi.

Please huu sio mkopo kwa wanaojiweza kwa sababu hauna riba na utakuwa umedhulumu haki ya mwingine.

Masharti na vigezo vitazingatiwa. Mshindi atatakiwa kusubmit some of his/ her details PM.

Pesa nitamtumia au kumkabidhi Ijumaa 21/ Febuari/2020.

Shindano litadumu kwa siku 3 tu.


UPDATES
23:15 Jumatano, nimefunga shindano
Nashukuru kwa mliojitokeza kuwania hichi kiasi kidogo cha 50.
Niko busy kidogo na majukumu na washiriki ni wengi.
Ninaomba Jumamosi weekend ndio nipitie post to post ili kuleta haki.
Mshindi atatangazwa na nitampa pesa mkononi kama yuko Dar na kama yuko mkoani nitamtumia na ya kutolea.
Kila mwezi nitafanya kitu hichi na atakayetengeneza faida kubwa zaidi nitampa Pesa nyingi zaidi.

UPDATES
JUMAMOSI SAA 2:50 ASUBUHI
Nimeanza kufanya sorting,niko page number 3,leo hii hii mshindi atatangawa.

UPDATES
09:15 AM
Nimemaliza uchambuzi wa awali na kupata post 22 zenye nguvu zaidi.
Nakunywa chai kisha nimalizie kusort na kupata vijana 3 nitakaowaleta yenu, asanteni.

Updates
09:48 am
Saturday
Nimepata watu hawa, na uchambuzi unaendelea miongoni mwao.
Kama kuna mtu hajatendewa haki anaruhusiwa kuleta malalamiko within one hour.
Walioingia kwenye kinyang'anyiro ni;
1.Zero IQ post no.29
2.Zwenge Ndaba post no.
3.Noelia, post no.170
4.CONTROLA post no.175
5.Davie post no.236
6.Naipenda Familia yangu, post.#57
7.Peramiho Yetu post #30
8.FK21 post #147.

Updates
1930 hrs
Ninaomba radhi kwa kuchelewesha matokeo ya mwisho.
Sikuwa hewani kwasababu zilizo nje ya uwezo.
But nikitulia nitamaliza kazi leo hii hii na mhusika atapewa chake kwa kadri tutakavyokubaliana njia ya kumfikishia Pesa yake.

Updates
23: 50
Nawashukuru washiriki wote wa shindano hili dogo.
Ninatamani kila mshiriki nimpe pesa nyingi kwaajili ya wazo lake ila kamba yangu ni fupi.
Nawashukuru pia wasomaji na wachangiaji wa Uzi huu.
Washindi ni hawa wafuatao;
3: Zwenge Ndaba, katika post yake #208 inayoelezea biashara ya maziwa kutoka Chalinze kwenda Kibaha au Dar es salaam.
2.Peramiho Yetu, katika post yake #30 anaelezea biashara ya Mahindi mabichi ya kuchoma kutoka Stereo Temeke .
1:Napenda Familia Yangu, katika post yake #57 ameelezea biashara ya maandazi na half cake .
Mimi kwasasa nitaanza na kutoa zawadi kwa mshindi nambari 1.
Kwa atakayekuniunga mkono anaweza kuungana nami kuwapa mtaji washindi nambari 2 & 3 au kumwongezea mtaji mshindi nambari moja.
Note:
Nitaendeleza hili jambo kila baada ya mwezi mmoja na ninawashauri watakaokosa wajaribu tena.
Mshindi anione pm
Ongera kwa mshindi, Ni wakati wake sasa kuchukua wazo kuliingiza kwenye Field,

Changamoto na Vikwazo ni mapito tu yasikukatishe tamaa, focus kwa kile unachokifanya naamini utaleta mrejesho Chanya hapa.


Cc Zero iq

Sent using Jamii Forums mobile app
 
faida yake ndogo sana na inaumiza yani box moja unapata 1,500/= but gud idea though!!
Faida ni ndogo kwa box moja lakin angalia mchanganuo, pia biashara inahitaji uvumilivu mpaka ikae sawa wengine huanza na hasara.

Kuna jamaa anafanya hyo biashara, alinunua freezer na akatafuta vijana akawasambaza katika mashule na matokeo yake ni mazuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MREJESHO
Wakuu habari ya leo,
Tumshukuru mungu kwa wale tulio na afya njema, na kwa wale wenzetu wenye shida mbalimbali basi mungu awafanyie wepesi.

Kama nilivyoanza na kichwa cha habari hapo juu nimeleta mrejesho wangu wa kinyang'anyiro hiki kilichokuwa kinaendelea kwa siku kadhaa hapa jukwaani, na wengi wetu kutoa mawazo yetu mbalimbali.

Mleta mada jana usiku wa saa sita aliahidi kumleta mshindi wa hili shindano,ambalo miongoni mwa orodha ile nami nilikuwepo na kuibuka na ushindi mnamo saa sita na dakika mbili usiku.

Akanifuata pm tukawasiliana usiku ule na akaahidi leo akishatoka ibadani, basi atakamilisha lile dhumuni lake. Na ilipofika saa 11:42am alinitumia hiyo pesa ikiwa kamili na ya kutolea.

Shukrani zangu za dhati ni kwa mwenyezi mungu kwanza,halafu wale wote tulioshiriki kutoa mawazo yetu hapa, sababu yatanufaisha watu wengi.

Bwana Bonde la Baraka mungu akuzidishie baraka zaidi kama unavyojiita, kwani umekuwa faraja kubwa sana kwetu,na naomba na wengine wenye uwezo mjitokeze zaidi ili kuweza kusogeza gurudumu hili la maendeleo hasa kwetu vijana.
Mungu awabariki sana.

NB:Si mwandishi mzuri kwa hiyo tuvumiliane kwa hili.
IMG_20200223_122140.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom