Huna hoja wewe
Wahindu Ng'ombe ni mungu sio symbol ya Mungu,, wanaoabudu Moto (Zoroastrianism) kwao Moto ni Mungu sio symbol ya Mungu pia yale Masanamu ya Buddha ni miungu kwao na sio Symbol ya Mungu. (Jitahidi uelewa).
Enhe sasa mbona huendelei unaishia hapo hapo tu kwenye hizo dini au hizo ndio dini pekee zilizopo duniani, vipi mbona huongelei ukristo, uislamu, uyahudi na dini nyingine ambazo zote zinaamini miungu yao iko mbinguni, kwahiyo bado narudi pale pale kwenye hoja yangu thibitisha kwamba ni mungu wa dini yako tu ndio yuko mbinguni
Unatudanganya majibu gani umetoa Bi Jadda??
Kasome tena comment yangu acha kutafuta visingizio
Nimekuuliza ukijitegesha ili upate mimba alafu asipatikane mwanaume utapata hiyo Mimba??
Hivi unaelewa maana ya mwanamke kujitegesha ili apate mimba au ni kiswahili ndio kimekupiga chenga hapo, nimemaanisha mwanamke anaweza akajitegesha kwa kufanya na mwananaume akiwa kwenye siku za hatari bila mwanaume kujua, au wewe hujawahi sikia kuna wanawake wanajibebesha mimba ya wanaume ambao hawakuwa na mpango wa kuzaa nao watoto
Aliesema Majukumu ya Baba ndio yanamfanya awe kiongozi ni nani??
Oohh kwahiyo tunakubaliana kwamba kinachofanya mwanaume awe kiongozi siyo majukumu yake, basi nisione tena huko mbele umehusianisha majukumu ya mwanaume na kuwa mtawala, tuende taratibu mwisho wa siku mbivu na mbichi zitajulikana tu
Nanufaika nayo ila wewe ulisema tunaonufaika ni sisi pekee kana kwamba familia hainufaiki.
Ni wapi niliposema mwanamke hanufaiki na hayo majukumu hebu uwe unasoma ili uelewe siyo unasoma ili ubishe, nilisema hayo majukumu yanamnufaisha mwanaume mwenyewe zaidi kuliko mwanamke, halafu kuna mahali nilikuuliza kwamba unapofanya hayo majukumu kama kuchimba visima sijui kupigana vita, hufanyi kwa ajili ya mkeo tu bali unafanya kwa ajili ya ndugu na jamaa zako na jamii yako kwa ujumla, sasa kwanini hao wengine wote wasikutii kwa sababu hiyo ila mkeo tu ndio anatakiwa akutii kwa sababu hiyo nijibu
Kwani Mada ni Kufuga wanyama Zoo au Utii wa Wanawake wa kisasa?? Naona nikiendela kukujibu katika hili unapata vichaka zaidi vya kujaza risala.
Haya ngoja nikichome hiki kichaka.
Kama umeshindwa hoja unasema tu siyo unajifanya unachoma vichaka, vichaka vyenyewe uliviotesha mwenyewe, ila baada ya kuona vimekushinda unanisingizia eti mimi ndio nimejifichia humo..pathetic!!
Suala la malalamiko ni kwa Pande zote kwa sababu Wanawake wana vituko vyao na wanaume kadhalika sijui wewe unakusudia nini??
Oohh kwahiyo sasa hivi unakubali kwamba wanalalamika sasa mbona mwanzo ulijifanya kukataa kwamba eti wanaume hawalalamiki, mimi hoja yangu ni kwamba wanaoongoza kwa hayo malalamiko ni wanaume kuliko wanawake na siku zote malalamiko ni ishara ya kuumizwa na jambo fulani, kwahiyo kitendo cha wanaume kulalamika zaidi kuliko wanawake kinadhihirisha kwamba ni wao ndio wanaumia zaidi kihisia kuliko wanawake
Pili kuathirika kisaikolojia ni kwa wote bali kwa wanawake ni zaidi kwa sababu you're too emotional.
Okay naona hapa tunazunguka sana ila ngoja nikusaidie tu na naomba hizi aya zinazohusu hii hoja uzisome kwanza zote ndio ujibu usikimbilie tu kujibu vipandevipande bila kuelewa maana nzima ya hii comment, ni hivi wanaume ndio wanaoathirika zaidi kisaikolojia na tabia mbovu za wanawake kuliko wanawake wanavyoathirika na tabia mbovu za wanaume hii ni kwa sababu maisha ya mwanaume yanarevolve around wanawake, yani mwanaume siku zote furaha yake iko kwa mwanamke kwa maana kwamba mwanaume siku zote anategemea mwanamke ndio ampe furaha hawezi kutafuta furaha nje ya hapo
Na wanaume ndio wanaopenda zile kauli za faraja na mahaba kama "pole na uchovu mpenzi" au "karibu chakula mume wangu" na kauli nyingine kama hizo maana zinawafanya wajisikie vizuri, na kama nilivyokuambia kwenye comments zilizopita kwamba mwanaume tangu zamani hajafundishwa kuvumilia maovu ya mwanamke mwanaume siku zote anategemea mwanamke awe ni kiumbe mwenye tabia njema hilo ndio linamfanya mwanaume awe na furaha, kwahiyo mwanaume akikosewa au akivurugwa na mkewe anachanganyikiwa na anakosa furaha anaanza kuona nyumba chungu kiasi cha kumfanya aanze kuchelewa kurudi nyumbani
Na atafikia hatua atapunguza hata ufanisi kwenye shughuli zake za utafutaji na hata kwenye tendo la ndoa na mwisho wa siku ataenda kutafuta faraja kwa mchepuko ambaye naye ni mwanamke, mwanaume anaweza kuwa bilionea lakini hawezi kuwa na furaha hadi atumie hizo pesa na wanawake kuna msemo unasema "kadiri mwanaume anavyozidi kupata pesa ndivyo anavyotamani kuwa na wanawake wengi zaidi, ila kadiri mwanamke anavyozidi kupata pesa ndivyo anavyotamani kuwa mbali na wanaume" na wanaume wengi matajiri hukiri kwamba moja ya faida za utajiri ni kuwa na wanawake
Lakini tukija kwa mwanamke yeye furaha yake haiko kwa mwanaume pekee mwanamke ana uwezo wa kutafuta furaha kwa watu wengine kama wazazi, watoto, ndugu na jamaa nk yani mwanamke tangu zamani alifundishwa kuvumilia maovu ya mwanaume, kwahiyo mwanamke hata akikosewa au akivurugwa na mumewe siyo rahisi kuchanganyikiwa au kuchepuka kuenda kutafuta furaha kwa mwanaume mwingine kwa sababu mwanamke hata usipomtamkia zile kauli za kimahaba kama nilizozisema hapo juu kwake ataona kawaida tu, mwanamke akipata pesa cha kwanza hawazi kutumia na wanaume bali atawaza kuzitumia na watoto na wazazi kisha watafuata ndugu na jamaa na wengine hata wazazi wengi wenye watoto wa jinsia zote husema kwamba watoto wao wakishaanza kujitegemea wa kike ndio huwa wanawakumbuka zaidi wazazi wao kuliko wa kiume ambao ahadi na kalenda zinakuwa nyingi
Hiyo ni kwa sababu wanaume wakipata pesa cha kwanza wanawaza kuhonga na kutumia na washikaji kisha ndio watawakumbuka wazazi na hao wengine ndugu na jamaa na kingine ambacho kinafanya wanaume waumie zaidi kisaikolojia kuliko wanawake ni kile kitendo cha kuhudumia, yani unakuta mwanaume kahangaika kuhudumia mwanamke halafu huyo mwanamke anakuja anamsaliti au anamuacha kirahisi tu ndio maana cases za wanaume kuua wapenzi wao ni nyingi ila za wanawake kuua wapenzi wao ni chache, sababu wanaume huwa wanahisi kama ndio wanapoteza zaidi kuliko wanawake ambao wao wakiwa kwenye mahusiano hakuna cha maana wanachooffer zaidi ya ngono na vitu vidogo vidogo huku wanaume ndio wakioffer vingi zaidi na hii ndio inawafanya wanaume waumizwe zaidi kisaikolojia na maovu ya wanawake kwahiyo usiwe unabisha bila kureason
Sio kweli,,, Kesi zaidi ya hizo zipo katika madawati ya jinsia.
Hizo kesi huwa zinahusu nini na ni ngapi kulinganisha kesi za kudai huduma za kiuchumi
Pili wanaopeleka kesi za huduma za kiuchumi Ni Huduma zipi hizo??
Huduma za kiuchumi kwa watoto wao au unataka kudanganya hapa kwamba huko kwenye madawati wanajaa wanawake wasio wa watoto, kwa taarifa yako huko asilimia kubwa wanaoenda ni wanawake wenye watoto waliotelekezwa, hivyo wanaenda kutafuta haki ya kutaka wanaume wahudumie hao watoto wao lakini hawaendi kulalamikia tabia mbovu za hao wababa
Tabia zisizo faa zipo kwa wote Bi Jadda.
Inanisikitisha kusikia kutoka kwako kwamba Umuhimu wa Mwanaume kwa Mwanamke ni Huduma za kiuchumi tuu(pesa) Wanaume Ni Walinzi wenu And Women are more comfortable with Men.
Sasa mbona umeandika kana kwamba hao wanaume hiyo kazi yao ya ulinzi wanaifanya vyema hivi ni kwamba huwajui wanaume wa kizazi hiki, wanaume wa kizazi hiki hawana kingine cha kuoffer zaidi ya pesa na mali basi na wanawake wameshaliona hilo ndio maana siku hizi kwenye mahusiano wanafuata hayo tu, wanaume wenyewe siku hizi wengi hawajielewi kwenye mahusiano wanafuata ngono na muonekano unategemea wanawake wataona umuhimu wa wanaume hapo
Hiki kichaka pia nakichoma.
Bora umeamua kuvipunguza hivyo vichaka mwenyewe, maana ningefanya hivyo mimi ungesema nakimbia hoja, mimi naenda sambamba na wewe huwa sikimbii hoja
Globalization inatusaidia kuyajua Mambo Hata ya Ulaya bila kuishi huko. Ila huo ndio Uhalisia Japo Sababu nyengine zipo ila Ujue pia U Feminism sio lazima uwe wa msimamo mkali (radical) kama huu wako kuna wengine Wanachovya chovya. Wanafanya Vitu kwa kuiga na Kusikia tuu na hata hawajui kuwa kuna kitu kinaitwa Feminism.
Oohh kwahiyo sasa hivi kuna feminism yenye afadhali na feminism yenye misimamo mikali, mbona unabadili gia angani tena wewe si ulikuwa unaitukana feminism hapa oo ni upumbavu sijui ni takataka, sasa hivi ndio unajua kwamba kuna stages za feminism hebu kuwa na msimamo mmoja basi feminism inafaa au haifai
Nimekwambia Ndoa nyingi hizi leo zinazovunjika ni Zile za wanawake wajuaji wanaoishia Kuwa single mothers Na kujidai they don't care.
Sasa si ndio nikakuambia ulete takwimu na ushahidi kuwa ndoa nyingi zinazovunjika ni zenye feminism
Unarudia jambo lile lile Vidada vijuaji Huitafuta Ndoa kama kondoo kisha Baadae huwa chui then sio muda ndoa inakufa.
Lakini kwa wale waliooa wanawake watiifu Mwanamke Hatoki bila kukuomba ruhusa Ukirudi amepika Vizuri na Anakusubiri Ule kisha ukale Unamuacha Kwa lipi??.
Hapa tena umebadili gia angani mwanzo ulisema wanawake wajuaji hawaolewi sasa hivi unasema eti wanaolewa ila wakileta ujuaji wanaachika, hivi unaelewa hata unachokisimamia na unachokitetea kweli mbona hujiamini na hoja zako unahamahama tu, kwahiyo wanawake wote wanaofanya hayo ndio hawaachiki na una uhakika ndoa zote zinazodumu ni zenye wanawake wa aina hiyo tu
Kazi Ninyi sasa Hutaki Upangiwe wapi unaenda na unaenda na nani pia Muda wa kurudi ni maamuzi yako. Kupika na hizo kucha zako za bandia ni Ngumu so atapika aunt Mumeo yupo kwa bed wewe upo na smart yako instagram unapost Ulivyokuwa Beach na Bikini. Sasa Usiachike kwa nini??
Wanawake Watiifu huoelewa Mapema angali vigoli. Ninyi Huwa hamna jinsi sasa mana una approach menopause na Huna Mume Mbaya hata Mtoto Huna Kizazi chenyewe Mtihani Zile contraceptives Chuo Zimeharibu kizazi unaona Yoyote tuu aje.
We jamaa unachekesha na unasikitisha sana hivi unajua maana ya feminism kwahiyo feminism ni wanawake kubandika kucha, kupost mitandaoni, kutumia contraceptives na huo ujinga mwingine ulioandika, yani muda wote unaitajataja feminism nikajua unajua hata maana yake kumbe hata maana yake yenyewe huijui unakuja kuleta nadharia zako hapa
Hizi Tamaduni unaziona hazina faida wewe. Sasa usilazimishe Kila uanchokiona wewe kibaya na kwa mwenzio nacho kiwe kibaya. Mind you German Ushoga ni Jambo zuri Sana na wanatushangaa sisi tunaopinga Mambo hayo.
Sasa mbona unaniambia mimi kana kwamba mimi ndiye niliyeanzisha feminism ni hivi hakuna mwanamke anayefurahia hizo tamaduni kwa utashi wake narudia HAYUPO, kitendo cha feminism kuanzishwa na wanawake kuikubali kinaonesha kwamba ni wanawake wengi waliona hizo tamaduni ni mbaya na hazina faida kwao bali zina faida kwa wanaume tu, hapa usiniongelee mimi ongelea mitazamo ya wanawake wote kwa ujumla toka feminism ilipoanzishwa hadi hapa ilipofikia
Ulevi na Usaliti ndio uanaume nani kakwambia It seems like umezungukwa na Wanaume wa aina furani hivi.
Hivi kweli unaweza kusimama hadharani ukasema Ulevi ndio Uanaume alafu ukaeleweka???
Wewe ni either unaishi kwenye nyumba za ibada na hupiti sana mitandaoni ndio maana unaishi kwa nadharia au uhalisia unaujua ila hapa unafanya makusudi tu kujitoa ufahamu ili mradi utetee uongo wako, ni mara ngapi wanaume wanajitetea kwamba mwanaume kuchepuka ni nature kwa sababu mwanaume ameumbwa na tamaa na hatosheki na mwanamke mmoja tena wenyewe ndio huwa wanasema ukiona mwanaume hachepuki ujue ni shoga au masikini au hana nguvu za kiume, hata kwenye ulevi wanaume huwa wanajitetea kwamba mwanaume lazima akae baa na washikaji zake maana ndio sehemu nzuri za kupeana madili na michongo ya pesa na biashara wanadai mwanaume hutakiwi kila siku kuwahi kurudi nyumbani mkeo atakuzoea sana..hayo ni maneno ya wanaume wenzio vijiweni na mitandaoni halafu unasema eti mimi nimezungukwa na wanaume wa aina fulani mbona unapenda kuishi kwa kukariri
Personal attack kivipi!!. Kwani Si mnajivunia kutokuolewa Kwa sababu mnasimamia mambo yenu wenyewe no need of man.
Anyway kama nimesema uongo( kwamba ndoa unayo) prove me wrong kama nipo sahihi then hiyo sio attack ni reality.
Yani unataka niprove kwako kwamba mimi nina ndoa hivi una akili kweli wewe sasa personal issues zangu zinakuhusu nini wewe umeona kuna mahali mimi nimekuuliza kama una ndoa, jitahidi kwenye public discussions kama hizi usiwe unapenda kuingiza personal issues kwa sababu inachukuliwa kama defensive mechanism na ni ishara ya kushindwa na kukwepa hoja, marital status yangu haihusiani na michango yangu ninayoitoa kwenye hii mijadala kwa sababu humu tunajadili uhalisia uliopo kwenye jamii hatujadili kulingana na hali zetu binafsi za maisha kwahiyo wewe jikite kwenye hoja
Nilikuuliza kuwa jee wewe Bibi yako amekwambia Alikuwa hana Furaha na maisha yake ya ndoa na Babu yako chini ya mfumo mnaouita mfumo dume?? (Jaribu kujibu)
Hili mbona jibu lake lipo kwenye ile comment yangu na linajieleza nenda kanisome tena
Nadharia gani Ninyi wanawake wanaharakati mnajua kupika?? Na hizo kucha mnapikaje?? Huo Muda wa kupika mnapata wapi?? Wakati Mkirudi kutoka Ofisini Mmechoka mnamkolomea Aunt awahishe Chakula.
Wewe haujui maana ya feminism, yani bado unashikilia kwamba mwanamke kubandika kucha ni feminism, nani aliyekuambia kwamba mwanamke kubandika kucha ni feminism
Vita ni mfano tuu hata Wanaume walikuwa na Shughuli chache za kufanya Baada ya Shamba. Jamii yetu miaka ya tisini sio hii unayoiona leo iliyojaa pilika pilika.
Aisee Hizo kazi mbona kwa wakati huo pia zilikuwa hazijawa kama zilivyo sasa Ulitaka wanawake wawe wahandisi sijui madaktari mwaka 1930 Uko serious??
Ndio maana nikakuuliza kwahiyo ina maana hiyo miaka watu walikuwa hawatibiwi au bidhaa zilikuwa hazitengenezwi, au ni wapi mimi nimesema kwamba hizo kazi zilikuwa zinafanyika kama zinavyofanyika miaka ya sasa, mimi nilimaanisha kwanini wanawake walikuwa hawapewi hiyo elimu kulingana na teknolojia hiyo hiyo iliyokuwepo miaka hiyo
Nasisitiza Utii unachunga Mahusiano yaliyopo baina ya Watu husika. Nakazia tena.
Nami nasisitiza kama ni hivyo basi msingi wa utii wa mwanamke kwa mwanaume siyo kuzidiwa nguvu na umadhubuti, kwa sababu hicho kigezo hakichagui aina ya mahusiano maana siku zote mwanaume yeyote ana nguvu kuliko mwanamke yeyote, hapo umechemka hauna hoja
Nachoshangaa Hili jambo ulilitolea majibu wewe mwenyewe.
Nilikuuliza Mtoto akiwa Anajitegemea aache kuwatii wazazi wake kwa kuwa hawamuhudumii tena Ukasema hapana Sababu Mtoto anatakiwa Amtii Mama yake kwa kuwa yeye amemzaa. Hivyo uhusiano wa Mama na Mtoto ni Mmoja kamzaa Mwengine Japo Mmoja ni Mwanamke na Mmoja ni Mwanaume. Sasa kama ndivyo hivyo Unaonaje ukalichukua hilo katika upande huu pia. Uhusiano wa Mke na Mume ni Mmoja kamuoa Mwengine. Sio sawa na Ule wa mmoja Kamzaa Mwengine. (Jitahidi uelewe)
Sasa ndio uone kwamba hicho kigezo chako cha nguvu na umadhubuti ni batili kwa sababu mtoto wa kiume kumzidi mama yake nguvu hakumfanyi awe mtawala, mimi niliitetea hoja yangu vizuri kabisa kwamba msingi wa mtoto kumtii mzazi (bila kujali jinsia) ni kwa sababu hao wazazi wamemzaa na wanamhudumia na hicho kigezo cha kumzaa ndio chenye nguvu, ila wewe ukasema tu kwamba kigezo cha mwanaume kumtawala mwanamke ni nguvu na umadhubuti sasa kiuhalisia hicho kigezo hakichagui aina ya mahusiano, wewe ndio unalazimisha kwamba hicho kigezo kinachagua aina ya mahusiano ila si kweli halafu mbona umeng'ang'ania hayo mahusiano ya mama na mtoto tu, kwani hukuona hayo mengine ya shangazi na dada na ndugu wengine wa kike wa mwanaume je nao wanatakiwa kumtii kwa sababu tu kawazidi nguvu na umadhubuti
Hahahaha defensive mechanism. Unapopataka wapi??
Unachotaka kusema kuwa Wanaume wana Nguvu Sawa na Wanawake na Wanauwezo sawa katika hayo Mambo uliyoyataja??
Hiyo siyo hoja hoja ni kwamba wanawake wanaweza kufanya ambayo wanaume wanaweza huo utofauti wa kuyahimili unaletwa na binadamu wenyewe, kwa sababu hata ninyi kuna majukumu ya wanawake ambayo mnaweza kuyafanya ila hamuwezi kuyafanya kwa ufanisi kama wanawake mfano kulea watoto lakini hutasikia wanawake wakijiit watawala kwa hilo, halafu kwanza kule juu umeuliza swali la kuashiria kwamba kinachomfanya mwanaume kuwa mtawala siyo majukumu yake kwahiyo sitegemei tena utahusisha haya majukumu na utawala wa mwanaume
Kwanza hoja Ilikuwa sio Hii. Umepindisha Hoja. Wewe ulisema kazi za nyumbani Wanaume hawawezi kuzifanya Mnaweza ninyi kwaiyo You're Strong for that. Poor you.
Ni wapi nimesema kwamba mwanamke ni strong kwa sababu ya kufanya kazi za nyumbani hebu paquote halafu nioneshe nasisitiza nioneshe, mimi nilisema mwanamke ni strong kwa maamuzi aliyonayo juu ya uzazi tu yani wewe ukiishiwa hoja unalazimisha kunipandikizia maneno ili upate sababu ya kuendelea kujaza magazeti, kazi za nyumbani siyo majukumu ya kimaumbile hivyo hata wanaume wanaziweza tena kwa ufanisi kabisa ila swali langu ni kwamba kwanini hawapendi kuzifanya wanataka mpaka wanawake wawafanyie tena wanadai eti ni majukumu ya kike
Pili mgawanyo wa majukumu ndio unaoongoza mambo hayo Baba Anaenda kutafuta Mahitaji Muhimu kwa ajili ya familia kutokana na Maumbile yake ya Nguvu na Umadhubuti na Mama anasimamia Majukumu ya hapo nyumbani pamoja na Malezi Nyumbani.
Sasa kumbe unajua kwamba huo mgawanyo wa majukumu uliwekwa kwa sababu ya utofauti wa kimaumbile tu na si kigezo cha kumfanya mmoja awe mtawala kwa mwenzie, yani ni kama vile mnajaribu kusema kwamba majukumu ya mwanaume ndio ya muhimu na magumu zaidi kuliko ya mwanamke wakati ugumu au urahisi wa jukumu unatokana na maumbile ya mhusika, kama kuna mtu anaona kama majukumu yake ndio ya muhimu na magumu zaidi kuliko ya mwenzie kiasi cha kutaka kumtawala mwenzie basi aishi peke yake na afanye hayo majukumu yote peke yake ikiwemo hayo anayoyaona marahisi bila kuhitaji msaada wa jinsia nyingine
Changamoto ni katika familia zenu wewe unatoka na Mumeo anatoka Watoto wenu mnaachia aunt Mtoto wako akifanyiwa vitendo vibaya Mnalalamika Wakati Binti mnamlipa laki moja.
Na Ndio mana Watoto wa Familia hizo za Baba Sharubu mama Sharubu Utaona Tabia zao zinavyokuwa.
Sasa kama shida ni watoto maana yake wanawake wasitoke kabisa wasiende hata kutafuta pesa wawe wamama wa nyumbani tu, lakini siyo kusingizia eti mitoko ya mara moja moja ndio chanzo cha watoto kuharibiwa wakati mke huyo huyo anashinda kwenye kazi au biashara siku tano au zote za wiki, na hilo suala la wanawake kuwa wamama wa nyumbani ni mada nyingine kabisa na ni kitu ambacho siyo jamii tu bali hata serikali hazitakubali kurudi huko kwa sababu huo mfumo wa maisha ni adui wa mapato na maendeleo ya nchi ila kwa sababu wanaume ni wabinafsi mnawaza maslahi yenu ya kipuuzi tu
Ujerumani na Ulaya kwa Ujumla ushoga Unalazimishwa?? au unakusudia Huku Afrika??
Ushoga duniani kote unalazimishwa ndio maana hata wanaoupinga wengi ni wanaume ambao ndio jinsia yao inahusika, lakini pia wengi wanaoipinga feminism ni hao hao wanaume siyo wanawake ambao jinsia yao ndio inahusika unadhani ni kwanini, jiulize kwanini wanawake wameifurahia feminism ambayo inahusu jinsia yao ila wanaume hawajaufurahia ushoga ambao unahusu jinsia yao halafu ndio utajua kipi kinalazimishwa na kipi hakilazimishwi
Kipimo sio Feminist apate mtoto wa Kike Bali Apate Mtoto Wa Kiume kisha tumuulize atamfundisha Nini Mtoto wake wa kiume Juu ya Mkewe atakaemuoa??
Kwamba Awe gentleman asimpangia mkewe pa kwenda wala asimzuie akiamua kutoka asiwe mkali Akipewa taarifa na mkewe kuwa hatorudi Nyumbani kwa siku hiyo yupo kwa rafiki zake. Amuhudumie Mkewe Vizuri pesa yake ni ya kumuhudumia mkewe na familia ila pesa ya mkewe Ni kwa ajili ya send off na kitchen parties. Kwamba asifatilie Mienendo ya mkewe Hasa simu yake kila mtu yupo huru katika ndoa Hakuna wa kumuongoza mwenzake. Kila mmoja anajiongoza Mwenyewe.
Aiseee kwani wewe huoni namna wamama wanavyowalea watoto wao wa kiume siku hizi hadi wanaume wanalalamika kwamba wanawake siku hizi wanaharibu watoto wa kiume, kwa taarifa yako wamama wengi wanajitahidi kuwalea watoto wao kiume kuwa gentlemen ninyi wababa ndio mnalea watoto wa kiume kuwa na ubabe wa kipumbavu mnadai eti ndio uanaume kwamba asipokuwa hivyo wanawake watampelekesha, wamama wengi huwa wanawalea watoto wao wa kiume katika misingi ya kwamba mwanamke ni mwenza wako na siyo mtumwa wako wote mnatakiwa kusaidiana kuheshimiana na kusikilizana
Binti yangu kuwa house wife Mtiifu kwa Mumewe ni jambo zuri kwangu kuliko kuwa degree holder Employed kiburi kwa mumewe. Mind you Kiburi Baada ya kusoma Ni maamuzi ya mtu kutokana na watu aliokutana nao katika safari yake ya kusoma.
Ndio maana nikakuambia hapa unaandika tu majibu ambayo yatakuwa upande wa hoja zako mradi tu utetee uongo wako ila hali halisi tunaiona namna wanaume wa siku hizi wanavyopambana kulea na kusomesha mabinti zao ili wasije kuwa watumwa wa wanaume kisa huduma za kiuchumi, kuna uzi uliwahi kuanzishwa humu jf kuwauliza wanaume kwamba "je utakubali binti yako aolewe na mwanaume mwenye matendo kama unayomfanyia mkeo", aise comments nyingi za wanaume ziliashiria hawako tayari kwa hilo na huo ni mfano tu kati ya mifano mingi inayoonesha jinsi gani wanaume wana ubinafsi juu ya wanawake wanaotaka kuwaoa tu
Huo mfano hautoshi?? Mbona unamun'gunya maneno unajidai kama vile unayajua maisha mengine Tofauti na yale anayoyasema Mwenyewe. (Prove)
Yani unataka niprove hilo ndio hoja iwe na ukweli we jamaa huna akili wewe inaonekana hata siku ukisikia mchungaji au shehe kafumaniwa au kabaka (maana hayo mambo yapo), utapinga kwa sababu tu ni mtu ambaye anasimama madhabahuni anahubiri mema na yeye anaonekana ni mtenda mema, ninyi msiojua ukweli mtamuona mtakatifu lakini sisi tunaoujua ukweli hatuwezi kuyatilia maanani hayo mahubiri yake maana mbele ya macho yetu tunamuona kama mnafiki tu
Defensive mechanism. Na malalamiko tuu.
Binadamu wote tuna mapungufu na ndio maana migogoro baina yetu haishi hata wewe inawezekana watu wako wa karibu mlishwahi kukwaluzana. Wanawake wanayakwao Katika ndoa. Kama huyajui then basi wewe ni mgeni katika Masuala ya familia.
Mapungufu binadamu tunavumiliana na kuelekezana na kuadabishana inapobidi.
Sasa kama mnavumilia mbona mnaoongoza kulalamika ni nyie na kuvunja ndoa kila siku
Kwani huoni Ndoa zinazovunjika nyingi ni za Mafeminist baada ya kushindwa kuendelea kuficha makucha yao. Na wale Wanawake wanaowaiga Wanawake kama ninyi bila kujua kuwa wengi wenu mnazungumzia ndoa wakati ninyi hamjaolewa.
Wewe una data na ushahidi gani juu ya hili
Kwaiyo Wananchi wengeshirikishwa Kipengele kingetolewa??
Ndio
Eti Kijana it's okay Sio shida
But Walioweka hiko kipengele ni katika Kuchunga heshima kwa kiongozi wa nchi na sidhani kama kuna nchi Ulaya yenye demokrasia kubwa ambapo Rais anaweza kushitakiwa akiwa madarakani.
Hapa hoja siyo lengo la kuwekwa hiko kipengele, bali hoja ni kwamba wananchi hawawezi kufurahia hicho kipengele endapo rais ana makosa, na ndio maana nchi nyingine raia wanaandamana au majeshi yanapindua serikali
Unaweza kujitengenezea mambo ukahisi unakuwa psychological tortured kumbe ni expectations zako tuu. Kama ninyi mnavyoiga maigizo ya kizungu.
Wewe kwanini umpangie mtu ni kipi kinachompa furaha na kipi kinachompa huzuni, kama mtu anaona kwamba jambo fulani kwake linampa psychological torture kwanini wewe umkatalie kwani wewe ndio umeshikilia hisia zake, na mbaya zaidi eti kauli kama hizo zinatoka kwa huyo huyo anayekupa hiyo psychological torture unategemea nini lazima tu atatetea upande wake kwa maslahi yake
Nilikuwa nataka uniambie Hizo Ndoa chache zilizokuwa na furaha. Furaha ilitoka wapi?? wakati Mwanamke hakuwahi kuwa na furaha chini ya Mfumo Dume.????
Si ndio maana nikakuambia kulikuwa na few exceptions za wanaume ambao hawakuwa na hizo tabia ambazo zilikuwa common kwa wanaume wengi, una uelewa mdogo sana kiasi kwamba umeshindwa kuelewa huo mfano wangu unamaamisha nini hapo, au unahisi mimi sijui ninachokisimamia na ninachokitetea kama wewe unavyohamahama
Hakuna hoja unajenga na Unaandika ili ubishe tuu to infinity.
Wewe ungekuwa siyo mbishi tusingefikia hapa, hata wewe pia ni mbishi tena bora mimi nabisha kwa facts, wewe unabisha kwa mihemko mradi tu usionekane umeshindwa huu mjadala kirahisi
Maandiko sio Nature acha kulazimisha.
Ndio mimi nasema maandiko siyo nature, ila watu wa dini ndio wanadai kwamba maandiko ni nature, sasa kwa hiyo kauli yako maana yake unaniunga mkono mimi
Uhuru wa Kuendelea na mahusiano mengi bila kuulizwa na yeyote.
So
Nani kazungumzia starehe hapa??
Sasa kuruka viwanja ni nini ni basic need au
Jee Sababu zipi zenye mashiko Mwanaume anaweza kumzuia mkewe kutoka?? Au hakuna kumzuia kabisa??
Sababu zenye mashiko ni zile ambazo zinatakiwa kuapply hata kwa mwanaume mwenyewe, siyo hizo sababu azitoe kwa mwanamke tu halafu yeye ajiexclude kwenye hizo sababu, kama sababu ni madhara basi hayo madhara yawe yale ambayo yanaweza kumpata yeyote kati yao endapo atafanya jambo fulani au ataenda sehemu fulani
Si ninyi mnaodai kwamba kwa sababu mwanaume na mwanamke hawako sawa kwenye maumbile tu basi hawatakiwi kuwa sawa kwenye mambo mengine yote
Hakuna maisha ya namna hii.
Ndio mhakikishe hamkwami kiuchumi sasa
Unayazungumziaje Haya Maandiko.
1 Timotheo 2:11
[11]Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
1 Timotheo 2:12
[12]Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.
1 Wakorintho 11:3,7,10
[3]Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.
[7]Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.
[10]Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na dalili ya kumilikiwa kichwani, kwa ajili ya malaika.
Kama umeamua kutumia maandiko basi usichague yale yanayofavour jinsia yako tu, haya naomba niletee na maandiko ya mwanaume kula kwa jasho na kulisha na kutunza familia, halafu uniambie kwanini mwanamke hakuambiwa hayo
Nimeshajibu.
Aisee!!!
Kwanza nikuulize wewe unafurahia talaka kuwa nyingi!! una Shida Kubwa. Mind you dada zako ndio wanaachika Na kuwa single mothers.
Ni wapi nimesema nafurahia talaka mimi naandika hali halisi iliyopo tu, kwani ni uongo kwamba watu hawapeani talaka kila siku, we vipi mbona unalazimisha kunipandikizia maneno
Hakuna uhusiano na hii mada yetu acha porojo.
Ndio kuna uhusiano jamii nyingi bibi zetu walikeketwa kwa sababu babu zetu walioa wake wengi na wakati mwingine walishindwa kuwaridhisha ipasavyo, hivyo kwa kuhofia kuwa watawasaliti wakaanzisha utamaduni wa wanawake kukeketwa ili wasiwe wanapata hamu ya tendo hata kama hawajakutana na waume zao kwa muda mrefu, hivyo hiyo ingewafanya kushindwa kuchepuka na kubaki waaminifu kwa waume zao tu
Una ushahidi juu ya hili??
Hahahha eti wanaume wanaojielewa Wanapatikana kwa wingi Mkoa Gani??
Kwamba kujielewa ni kabila, hadi watu wanaojielewa wapatikane mkoa fulani, we jamaa mbona unafurahisha sana
Sasa mara kwamba unayajua Ya chinichini mara yeye sio kielelezo cha Wanawake wote Hueleweki.
Yote hayo ni majibu acha kukwepa hoja, nasisitiza rais samia siyo kielelezo cha namna wanawake wote duniani wanavyotakiwa kuwa, huo ni mtazamo wake binafsi na siyo sheria na wala haumfanyi kuwa sahihi au kuwa na akili kuliko wanawake wengine wote
Aisee Kwaiyo Unaolewa na Una guarantee utii katika Pesa zikikosekana unaonyesha uhalisia wako (Changamoto).
Siyo kuguarantee utii katika pesa bali huo ndio msingi wa utii wa mwanamke kwa mwanaume, yani wewe mtu hujamuumba wala hujamzaa unataka akutii kwa lipi, hivi hata kwa akili ya kawaida tu wewe unaona hiyo inaingia akilini kweli..anyway wewe lazima ikuingie akilini kwa sababu ina maslahi kwako huwezi kutumia common sense kwenye jambo linalokufavour hata kama ni baya kwa mwingine au kwa ujumla
Jike dume kama ilivyo literally.
Sijui ulishawahi kujiuliza kwanini Wewe tukikwambia una Tabia za kiume kiume Haitakuwa shida sana and may be Uta feel proud ila Mwanaume tukimwambia ana tabia za kike kike Hiyo ni Vita imeanzishwa hatokubali.
Sasa hilo suala la mtu wa jinsia fulani kufurahia au kuchukia kupewa sifa za jinsia nyingine limekujaje hapa, anyway kwakuwa mimi sikimbii hoja acha nikujibu kwamba hayo yote ni kutokana na fikira tu zilizojengeka kwenye jamii, lakini huwezi kusema moja kwa moja kwamba kumuita mtu wa jinsia fulani kwa jinsia nyingine ni vizuri au vibaya labda useme inategemea
Usitoe majibu mepesi katika hoja ngumu.
Wewe kuna hoja gani ngumu umeweka hapo hebu jistukie
Mwanaume akiwa na sababu ya msingi anaruhusiwa kumzuia mkewe akitaka kutoka??
Ndio endapo hiyo sababu itakuwa applicable to both parties hilo nimeshaeleza
Kwani tulikuwa tunajadiri Waarabu au Jamii yetu ya Zamani??
Duuh kwahiyo informal education, inakuwa defined kulingana na maisha ya jamii zetu za kiafrika tu, aise yani unapuyanga hadi unatia huruma
Aaah kwanini umetanguliza "bila mshahara" Defensive mechanisms zako Hovyo kabisa.
Anyways Tufanye hunyimwi mshahara jee Kumtii boss wako unakosa furaha??
Aiseee hivi we jamaa unasoma comments zangu zote hadi mwisho kweli au ukifika katikati tu basi unakimbilia kujibu, si nimekuambia hapo kwamba hakuna anayefurahia kumtii boss wake ila watu wanakubali kwa sababu tu ya mshahara, nikakutolea na mfano kwamba ndio maana watu wengi wenye uwezo huwa wanaanzisha biashara zao kwa sababu wanaona ajira ni utumwa
Uongo.
Nadharia.
Hueleweki.
Huna hoja wewe
Okay kwahiyo mfano huyo mwanaume anamuwajibisha mkewe, na huyo mkewe hasikii bado anaendelea, je huyo mwanaume bado anatakiwa kuendelea kumpenda huyo mke wake
Maneno yako ni sahihi kwamba uliposema Mshahara ni Huduma ulikuwa sahihi??
Kwanza ni wapi niliposema kwamba mshahara ni huduma nioneshe
Hahahaaaa
Unajua unachokiandika kweli??
Kwamba wale pet dogs na puppies ni hatari??
Aise kwahiyo wewe unajua hao tu ndio mbwa pekee wenye mionekano mizuri, nikikuambia unitajie aina za mbwa unazijua kweli au ndio kwa hisani ya google, ndio maana nikakuambia usiishi kwa kukariri wapo mbwa wenye mionekano mizuri na ni hatari
Cheo kina nini kwanini unamtii??
Ni kwa sababu wananchi wenyewe ndio wamemchagua na wamempa kile cheo na yuko pale kuwatumikia wananchi, pia unaweza kumtii kwa sababu unamuogopa lakini si kwa sababu eti umependa kumtii, hili kila wakati nakujibu lakini unajitia kukaza kichwa nishakuambia utii unaoletwa na uoga siyo nature
Maandiko katika Utii wa Mke kwa Mumewe hayana Tofauti.
Sawa mbona huongelei na maandiko ya mume kumpenda na kumhudumia mkewe na kwanini mwanamke hakuambiwa afanye hayo kwa mumewe
Tangu katikati ya Karne ya 19 harakati za ukombozi wa mwanamke (feminism) zilianza.
Lakini sio Harakati zote zilikuwa na Malengo makuu yanayofanana au Kuhusisha Kundi moja la Wanawake baina ya vizazi.
Katika historia harakati za kudai haki za wanawake zilianza Ulaya wakati haki za binadamu zilipoanza kutangazwa, ambazo awali zilijadiliwa kwa wanaume pekee.
Kutokana Na Tofauti Zilizopo Baina ya Vizazi kwenye Harakati za Feminism kuanzia Karne ya 19(1848) hadi karne Hii. Zimegawanywa Harakati hizi katika sehemu Kuu Tatu (au nne) (Waves)
First Wave: 1848 - 1920
Katika Wimbi hili Lengo kuu lilikuwa ni Kupambania Haki Sawa ya Kupiga Kula kati ya Wanaume na Wanawake (Suffragettes)
Harakati ya kuwapa wanawake haki za kupiga kura kwenye uchaguzi wa kisiasa ilikuwa kampeni ya awali kuanzia karne ya 19, lakini hasa ya 20.
Katika jambo hili waliohusika Walikuwa ni Wanawake wakizungu wenye hadhi ya Juu ambapo Wanaume weusi wa hadhi ya kawaida waliruhusiwa kupiga kura lakini Wanawake wa kizungu wa Hadhi ya Juu Hawakuruhusiwa.
Mnamo mwaka 1920 Rasmi Wanawake wa kizungu waruhusiwa kupiga kura.
Haikuwa hivyo hadi ilipofika mwaka 1965 ndipo Wanawake wa Rangi nyengine nao waliporuhusiwa kupiga kura.
Second Wave: 1963 - 1980s.
Katika Wimbi Hili Wanaharakati Walienda mbele zaidi kutaka Majukumu ya kijamii yatazamwe upya. Kwamba Mwanamke kazi yake si tuu kuwa Mke au Mama. Wakidai Usawa kati ya Wanaume na Wanawake.
Bado Harakati hizi ziliwahusu Sana Wanawake wa Kizungu Hadi kupelekea kuanzishwa kwa Harakati za Wanaharakati wanawake weusi(National Black Feminist Organization (NBFO)).
Third wave 1990- (radical feminism).
Harakati zimezonga mbele zaidi Kudai Usawa kamili Wa Mwanamke na Mwanaume katika nafasi za uongozi na majukumu ya kijamii.
Kwa mfano, kulingana na itikadi hii, tabia kati ya jinsia siyo za kibiolojia bali ni ya mafunzo tu.
Wafuasi hao wanaamini tofauti hizi zipo ili wanaume waweze kudhulumu wanawake.
Kwamba Mwanamke anaweza kufanya Kila Kitu ambacho mwanaume anaweza fanya Na Hizi tofauti zilizopo katika Jamii Ni matokeo ya Wanaume kuiaminisha Jamii kuwa Ni wao pekee wanaoweza kufanya hayo Jambo ambalo sio kweli.
Wimbi hili Limekufanya makundi mengi ya Jinsia na Rangi (Marginalized groups) Pamoja na Trans genders.
KATIKA MAELEZO HAYA UNAWEZA UKAONA KUWA HILI JAMBO LA U FEMINISM HALIKUANZA KAMA LILIVYO HIZI SASA HIVYO BAADA YA KUPATA NGUVU KUBWA YA KIMADALAKA HUENDA HARAKATI HIZI ZIKAFIKA MBELE ZAIDI KUDAI MASUALA MENGINE ZAIDI AMBAYO HATA HATUWEZI KUYAFIKILIA HIVI LEO. NA HAPO HUENDA KIKATOKEA KITU AMBACHO HATUWEZI KUKIFIKILIA KWA SASA.
Aise sasa mbona hujajibu swali langu, yani muda wote unaniambia nisubiri kwamba utakuja na jibu ila hapa ndio unaona umekuja na jibu kweli, yani umekimbilia kuniambia habari za waves za feminism wakati mimi nilikuuliza kwamba
Kama kila mwanamke anazaliwa na fikira za kutaka kutawaliwa na mwanaume, na hakuna mwanaume anayezaliwa na fikira za kutaka kutawaliwa na mwanamke (maneno ambayo ulisema mwenyewe), je feminism ilianzishwa na nani na kwa faida ya nani hebu nijibu kwanza hilo
Kuhusu waves za feminism mbona nilikuambia kwamba lengo kubwa la feminism ni wanawake kuanza kuwa na access ya elimu na ajira, na kumiliki pesa na mali sawa na wanaume hayo mengine yote ni matokeo ya wanawake kuwa na hivyo nilivyovitaja, kwahiyo nijibu swali langu acha kutafuta vichaka vingine vya kujifichia