Utofauti wa Rwanda na Tanzania

Utofauti wa Rwanda na Tanzania

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
12,675
Reaction score
25,924
kwa waliotembelea Kigali (though not the whole Rwanda), kuna kitu kikubwa sana nimejifunza toka kwao, ambacho muda unavyoendelea wanaweza kufikia level zile za nchi za ulaya kabisa kwenye suala la usafi.

1. Tanzania usafi wa mazingira tupo nyuma sana, wenzetu wameweka misingi iliyokwisha ingia kwenye tabia ya mtu binafsi, ila sisi ipo tu kwenye nadharia ila mioyoni watu ni wachafu sana wa mazingira.

2. Barabara kuanzia Kibamba hadi Ubungo kwa mfano, imejengwa vizuri sana kuliko hata barabara za Kigali, kuna gardens katikati na pembezoni mwa barabara, lakini hazijafyekwa vizuri na kusawazishwa. wenzetu ulaya na kigali kidogo, pembezoni mwa barabara na kwenye gardens hata kwenye nyua za nyumba za watu, wamesawazisha na kama maji yapo wamemwagilizia gardens. hapa unakutana na vichaka katikati ya barabara na pembezoni, mateja wanakunyya na wazinzi wamerusha condoms.

3. Pembezoni mwa barabara, kuna marundo ya uchafu watu wamemwaga usiku. zile takataka magari ya uchafu yanapita kukusanya, DSM huwa wanatoka usiku wanamwaga karibu na barabara. ni uchafu wa moyo kabisa.

4. Pembezoni mwa barabara kuna gereji bubu kibao. angalia kutoka kibamba hadi ufike fire, kuna gereji bubu ngapi.

5. Pembezoni mwa barabara kuna vituo vya bodaboda na bajaji ambavyo sio rasmi. barabara nzurii ila kwa uwepo wa hawa jamaa holelaholela haina tofauti sana na zamani.

6. Mama ntilie wamejazana pembezoni mwa barabara, wanapika vyakula, kwenye lami zilezile safi, wanaosha mabakuli ya ugali na kumwaga barabarani. wakimaliza hawasafishi.ndio maana nnzi zipo everywhere DSM.

7. Wamenya machungwa na maembe na wauza mahindi ya kuchoma wamepangana pembezoni mwa barabara. barabara safiii ila unakutana na mtu kaweka toroli lake pale anakata machunga, wengine wanadondosha takataka haokoti anaacha palepale.

Kuna mengi ya kuandika. kwa wale wasioelewa, sijashobokea Kigali kana kwamba mimi ni mshamba hapana, nimeishi ulaya miaka mingi tu, najua maisha ya hapa na mbele, ila kwa afrika nimeona kama kigali wamejitahidi kwasababu vitu vyoote hivyo nilivyoorodhesha hapo juu, hauwezi kuvikuta pale, na ndio maana kidogo kidogo inaenda kuipiku Arusha kama Geneva ya Africa, mashirika makubwa na mikutano imeanza kwenda kigali badala ya Arusha.

Arusha imeshindwa nini, au Tz imeshindwa nini kuweka sheria za mchuma ili mazingira yawe safi na watu watajiadjust wenyewe polepole itafika mahali wataona ni tabia kuwa msafi.

mbarikiwe.
 
Sisi hadi tutakapoacha siasa uchwala ndo mambo yataenda.
 
Hivi inakujaje akilini barabara tuliyogarimia kwa kodi nyingi, kuona mtu kaweka gereji bubu anamwaga maoil, mamantilie hovyohovyo, vichaka katikati ya barabara, mimavi, mtu kamwaga jalala katikati ya garden ya barabara. manispaa kazi yao nini?
 
hivi inakujaje akilini barabara tuliyogarimia kwa kodi nyingi, kuona mtu kaweka gereji bubu anamwaga maoil, mamantilie hovyohovyo, vichaka katikati ya barabara, mimavi, mtu kamwaga jalala katikati ya garden ya barabara. manispaa kazi yao nini?
Wakitaka kuwatoa si malalamiko huwa yanapigwa sana. Unakumbuka walipotaka kuwatoa wamachinga barabarani, na wale wanaopanga vitu kkoo barabarani? Kelele za wanyonge
 
Wakitaka kuwatoa si malalamiko huwa yanapigwa sana. Unakumbuka walipotaka kuwatoa wamachinga barabarani, na wale wanaopanga vitu kkoo barabarani? Kelele za wanyonge
ni kweli, anatakiwa kutokea mtu katili kidogo, hali hii ikiendelea uchafu hautakuja kuisha. na ushamba.
 
Rwanda wana ardhi kidogo, barabara zao zingine sio bora kuliko za Tanzania, ila wameweka management nzuri sana kwenye suala la usafi, na ndicho kinachoongelewa hapa. hatuongelei uwingi wa watu, level ya maisha ya watu, majengo au chochote, ni usafi. ni mji gani Tanzania msafi kama kigali hata kama unaweza kuwa na barabara bora kuliko kigali? this is what we ware discussing here.
 
Kigali bodaboda wanasimama kwenye taa hawavuki mpaka ziruhusu, kwa mimi m-TZ nlishangaaa na sikutarajia kuona ule ustaarabu
 
kwa waliotembelea Kigali (though not the whole Rwanda), kuna kitu kikubwa sana nimejifunza toka kwao, ambacho muda unavyoendelea wanaweza kufikia level zile za nchi za ulaya kabisa kwenye suala la usafi...
Hao mamantilie wakiguswa si ndio nyie haohao manakuja humu, eti mtetezi wa wanyonge amekufa. Umesahau mgomo wa Iringa? Wacha watu waishi kwenye uchafu wao ni tabia zao.
 
Tunalinganisha nchi na ncĥi, jiji na jiji . Hapa n kama kulinganisha ujao na uzito...hesabu gani hizo?
 
Tunalinganisha nchi na ncĥi, jiji na jiji . Hapa n kama kulinganisha ujao na uzito...hesabu gani hizo?
kwa jinsi nchi yetu isivyojali mazingira, nachelea kusema, tunastahili kuwa challenged hata na mji mdogo kama kigali tu. weka mji wa Tanzania msafi kama kigali hapa. msikimbie ukweli, changieni nini kifanyike kutatua tatizo. msione shida kukubali kwamba kigali imeizidi Tanzania nzima kwa usafi. najua shida ni kwamba mnaona kama mnajidharaurisha kwa Rwanda ambayo kwa watanzania huwa tunaidharau kwasababu imekua wakati tunaiona. badi angalieni hata miji mingine hata ya ulaya tu, ni kitu gani kinaifanya iwe misafi mjifunze kwayo ili kuepuka kujisikia vibaya kulinganishwa na kigali.
 
Unalinganisha Tanzania na kamji kanaitwa Kigali, we umelogwa? Kwanza hata kulinganisha Tanzania na Rwanda lazima kwanza uwe mwehu.

Wilaya ya kinondoni tu ni kubwa kuliko kigali nzima.. miundombinu na maghorofa yaliyopo pembezoni ya bara bara kutokea mwenge mpaka mpaka surrender bridge yanazidi majengo ya kigali nzima kwa idadi na gharama za kuyajenga
 
Wilaya ya kinondoni tu ni kubwa kuliko kigali nzima.. miundombinu na maghorofa yaliyopo pembezoni ya bara bara kutokea mwenge mpaka mpaka surrender bridge yanazidi majengo ya kigali nzima kwa idadi na gharama za kuyajenga
dada, hapa tunaongelea USAFI, sio wingi wa majengo au watu. nahamasisha usafi. akili umetupa wapi?kinondoni ni safi kuliko kigali? hakuna anayebisha, kigali ni mji mdogo sana kimajengo na miundombinu, ilan i msafi kuliko sehemu yeyote ya Tanzania.
 
Wakitaka kuwatoa si malalamiko huwa yanapigwa sana. Unakumbuka walipotaka kuwatoa wamachinga barabarani, na wale wanaopanga vitu kkoo barabarani? Kelele za wanyonge
Upo sahihi mpaka akatafutwa mtetez wa wanyonge, kuna mijianaume et nayo inajiita minyonge? Mtoto wa kiume unakuaje mnyonge,na unakubali kuitwa mnyonge?
 
Wazo tu ukubwa wa Rwanda ni sawa na dsm ni vyema ukaifananisha Rwanda na dsm ipi ambayo kimadhari kimonekan kiusalam kiusafi na huduma za jamii.
Maana siku hiz Rwanda Rwanda kam vip hamia uko tu
 
Si ungesema kigali vs Dar es salaam, Tanzania yote siyo wachafu kama hao watu wa Daslam huko, usituchafue
 
Back
Top Bottom