Utoro wa wabunge bungeni tena bunge la bajeti, tatizo ni nini?

Nadhani bunge halina meno mbele ya serikali
 

Bajeti ya matumizi yao kila Mwaka ni kubwa sana, mishahara, Magari posho, Safari , matibabu n.k

Lakini tunaweza kujiuliza faida wananchi wanayopata kwa uwepo wao ni kama zipi kwa mfano ?

Au tubaki kuwa na Serikali na mahakama tu ?

Ikiwa kinachotatoka serikalini kinapita kama kilivyo kuna haja ya uwepo wa bunge la bajeti kwa mfano ?

Je Gharama wanazolipwa zikajengee
Mabarabara, hospital, Shule , Nyumba za watumishi, mishahara na marupurupu ya watumishi yaongezwe n .k. ?
 


Hivi Kwani bajeti ya bunge huwa inawasilishwa kupitia chombo gani?
Sijawahi kusikia ikisomwa wala kujadiliwa.
 


Ushauri :
Tufanye majaribio kwa ku-foregone bajeti yao iende kwenye miradi ya maendeleo.

Tuendelee kuiamini Serikali kuwa mambo yatafanyika kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma na Kwamba hakutakuwa na ubadhirifu wa fedha za umma wala mali za umma.
Office ya CAG iwe huru kufanya kaguzi kwa mujibu.

Huenda tukapiga hatua kubwa sana!
Tuone ?!
 
Kiukweli nami nadhan iwe hivyo,tunawalipa kwa kazi ambao haina matokeo.
 
Nadhan kuna haja ya kujitathimini upya.
 
Huenda wanakimbilia majimboni kuweka mambo sawa!
 
Hapo hakuna bunge mbali kuna kusanyiko la majngili tupu
 
Tulia kijana tushasaini posho tupo chako ni chako tunachoma kuku
 
Hawana muda wa kukaa hapo bungeni maana hilo ni bunge kibogoyo, na hawaruhusiwa kupinga chochote kinacholetwa na serekali bungeni. Zamani kukiwa na wabunge wengi wa upinzani walikuwa wanajitahidi Ili wazomee, na sio kujadili hoja, maana hawana uwezo wa kujadili hoja.
 
Tlaatlaah
 
Hivi bado mnafatilia bunge..duuh..hivi hapo kuna bunge kweli..
 
si muungwana hapo amekiri wazi yeye sie mjuzi wa masuala bayana kabisa ya Bunge πŸ’

ameghafulika tu kukerwa na kitu ambacho hana uelewa au ufahamu wa kutosha nacho, na hata hivyo sio mbaya, ndivyo binadamu tulivyo....

by the way,
mjengoni sio shuleni na kwahivyo hakuna alie mtoro....

nachelea kusisitiza kwamba wabunge mahiri sana hapa Dodoma wana kazi nyingi, ngumu na muhimu sana ndani na nje ya bunge kwa maslahi mapana ya nchi.

na zote hizo wanazifanya kwa mujibu wa kanuni za bunge, sheria na katiba ya nchi. na katika vikao vya bajeti vinavyoendelea hivi sasa, speaker ana taarifa na kila mbunge ambae humuoni mule ndani ila yupo kwa taarifa anaendelea na majukumu mengine ya kibunge na anachangia, anafuatilia kila hatua ya mjadala kwa njia ya mtandao πŸ’

bunge digital πŸ’
 
Kwahiyo
Kwahiyo bungeni kazi za nje ya bunge ambazo ni muhimu kuliko kuhudhuria vikao. Wapo spika anaruhusu wabunge wengi kutokuhudhuria kwa sababu ya bunge digital ,sisi wananchi je nasi digital
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…