Utosi wa mtoto kurudia kupiga!

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Kuna mtoto mdogo wa miaka minne ambaye utosi ulishaacha kupiga kwa muda mrefu, na hivi sasa amekuwa mvulana mkubwa hadi ameanza masomo yake ya chekechea, lakini ghafla utosi wake umeanza kupiga tena! Hili suala limenishangaza sana maana sijawahi kusikia wala kushuhudia tukio kama hili hapo kabla.

Jamani, kama kuna mtu aliwahi kushuhudia kitu kama hiki naomba anisaidie ili nijue pa kuanzia. Je, hili tatizo ni la kitabibu au inawezekana likawa la kimazingira? Tafadhali nijulishe ili nijue hatua muafaka (za kitabibu au mazingira) za kuchukua.

:help:
 
Mpeleke hospitali,mambo kama hayo ya watoto sio ya kutaka ushauri.tanguliza mungu kwa kila jambo..kuna doctor wa muhimbili lakini anakuwa anapiga kazi private ijumaa kuanzia saa kumi yuko tmj na jumamosi saa sita na nusu yuko agakhan na jumapili kuanzia saa tatu..mpeleke akushauri anaitwa kuboja doctor mzuri sana wa watoto na public holiday pia anapiga kazi agakhan..nakupm namba yake umuulize leo yuko hospital gani.
 

Mkuu, hebu niPM namba yake nimtafute faster. Nakushukuru sana kwa msaada wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…