Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Nimuite Etugrul Bey sio Jina halisi, alikuwa ni boss ambaye alikuwa ana jali Sana utu WA watu, kwake yeye kila binadamu alikuwa na thamani Sawa maadamu tu ni binadamu ni tofauti na watu wengine ambao huwathamini watu kutokana na kitu walinacho,au hadhi waliyo nayo au elimu waliyo nayo.
Tabia hii ilimfanya awapende na kuwathamini wafanyakazi wote iwe WA ngazi ya juu au wa Chini kabisa...na alikuwa na kawaida ya kumsalimia kila mfanyakazi aliyekutana naye pale kazini.
Tabia hii ilimfanya apendwe na kila mtu pale kazini, tofauti na maboss wengine ambao kwao uboss unawafanya wajione miungu watu,wamejawa na kiburi pamoja na majivuno na hivyo kuwafanya wasipendwe na wafanyakazi, kitu ambacho mara nyingi huleta uadui.
Etugrul Bey alikuwa na kawaida ya kuwasalimia walinzi wake pale kazini asubuhi na jioni wakati anapoondoka na alikuwa mkarimu Sana kwao kiasi ambacho kilijenga mahusiano mazuri Sana Kati Yao, siku isiyo na jina iliwadia ambayo ndio ilikuwa ichukue Uhai WA boss huyo, ilikuwa ni mida karibia na jioni boss huyo alikuwa katika kupitiapitia maeneo yake ya kazi basi alikuwa ktk chumba kimoja ambacho ni cold room kinahifadhi samaki wasioze, chumba Hicho kina baridi ya kutosha nikisema ya kutosha ina maana ni baridi haswaa!
Kama unavyojua makosa kaumbiwa mwanadamu, basi afisa anayesimamia chumba kile bahati mbaya nadhani alikuwa na haraka zake, kwahiyo Mda wa kuisha kazi ulipofika yeye kutokana na haraka aliyokuwa nayo alisahau kupitia chumba Hicho kama kawaida yake kuhakikisha kwamba kila kitu kipo Sawa kabla ya kuondoka na kuelekea nyumbani.
Sasa kwakuwa etugrul bey alikuwa na kawaida ya kuaga walinzi wake kabla hajaondoka kurudi nyumbani, walinzi wa zamu wa siku hiyo walijiuliza mbona si kawaida ya boss kuondoka kazini Bila kuwaaga, ndipo walipoenda kuangalia gari lake kweli lipo na kucheki ofisini hayupo, wakaanza kuingiwa na wasi wasi na kuhisi kuna shida ambayo huenda imempata boss wao mpendwa.
Wakaanza msako wa kumtafuta boss wao sehemu mbali mbali mule kiwandani lkn hawakumuona, ndipo mmoja wao akawa na mashaka Sana isije ikawa boss wao akawa amefungiwa ndani ya chumba kile kimakosa kwani alikuwa na kawaida ya kukagua kabla hajaondoka kwenda nyumbani.
Weka pozi Kwanza kidogo hapo. Leo hatuli pop corn wala nini, hakikisha unahesabiwa Sawa? Umuhimu wake ushasemwa Sana kwahiyo naamini kabisa tutalimaliza hili zoezi salama, hata kama hupendi ndo hivyo tena kuhesabiwa lazima!
Haya tuendelee na madini yetu Bbasi wakajadiliana na kuamua wavunje ule mlango wa cold room....lahaula! Kama walivyochezwa na machale baharia alikuwa anakaribia kuganda Kwa baridi Ile Kali...walimkuta ktk Hali mbaya Sana huenda wangechelewa kidogo mwamba angerest in peace! Lkn kama unavyojua kila mtu anakufa Tu siku yake inapofika Hilo halina ubishi! Basi walimuokoa na kumpa huduma ya Kwanza na hatimaye baada ya masaa kadhaa bey alipata nafuu na kuwa Sawa alhamdulillah.
Hekima ya story hii:
Wema unalipa...Utu unalipa ...Ubinadamu unalipa....ebu fikiria kama etugrul bey asingekuwa boss mzuri Kwa wafanyakazi wake bilashaka Leo hii bey angekuwa katika ulimwengu mwingine kabisa....haijalishi wewe Una hadhi gani ktk jamii, Una elimu kiasi gani,unahela kiasi gani, Una cheo kiasi gani...kumbuka mwisho wa siku wote bado ni binadamu na kama binadamu tunategemeana Kwa namna moja au nyingine.
Ukiwa boss mbaya unajenga uadui na watu na huenda hata wafanyakazi wanaweza kupanga kukufanyia ubaya....tafuta hii movie inaitwa THE HORRIBLE BOSSES nadhani wale waliyo icheki hii movie wanajua shughuli yake.
Ni hayo Tu.
Tabia hii ilimfanya awapende na kuwathamini wafanyakazi wote iwe WA ngazi ya juu au wa Chini kabisa...na alikuwa na kawaida ya kumsalimia kila mfanyakazi aliyekutana naye pale kazini.
Tabia hii ilimfanya apendwe na kila mtu pale kazini, tofauti na maboss wengine ambao kwao uboss unawafanya wajione miungu watu,wamejawa na kiburi pamoja na majivuno na hivyo kuwafanya wasipendwe na wafanyakazi, kitu ambacho mara nyingi huleta uadui.
Etugrul Bey alikuwa na kawaida ya kuwasalimia walinzi wake pale kazini asubuhi na jioni wakati anapoondoka na alikuwa mkarimu Sana kwao kiasi ambacho kilijenga mahusiano mazuri Sana Kati Yao, siku isiyo na jina iliwadia ambayo ndio ilikuwa ichukue Uhai WA boss huyo, ilikuwa ni mida karibia na jioni boss huyo alikuwa katika kupitiapitia maeneo yake ya kazi basi alikuwa ktk chumba kimoja ambacho ni cold room kinahifadhi samaki wasioze, chumba Hicho kina baridi ya kutosha nikisema ya kutosha ina maana ni baridi haswaa!
Kama unavyojua makosa kaumbiwa mwanadamu, basi afisa anayesimamia chumba kile bahati mbaya nadhani alikuwa na haraka zake, kwahiyo Mda wa kuisha kazi ulipofika yeye kutokana na haraka aliyokuwa nayo alisahau kupitia chumba Hicho kama kawaida yake kuhakikisha kwamba kila kitu kipo Sawa kabla ya kuondoka na kuelekea nyumbani.
Sasa kwakuwa etugrul bey alikuwa na kawaida ya kuaga walinzi wake kabla hajaondoka kurudi nyumbani, walinzi wa zamu wa siku hiyo walijiuliza mbona si kawaida ya boss kuondoka kazini Bila kuwaaga, ndipo walipoenda kuangalia gari lake kweli lipo na kucheki ofisini hayupo, wakaanza kuingiwa na wasi wasi na kuhisi kuna shida ambayo huenda imempata boss wao mpendwa.
Wakaanza msako wa kumtafuta boss wao sehemu mbali mbali mule kiwandani lkn hawakumuona, ndipo mmoja wao akawa na mashaka Sana isije ikawa boss wao akawa amefungiwa ndani ya chumba kile kimakosa kwani alikuwa na kawaida ya kukagua kabla hajaondoka kwenda nyumbani.
Weka pozi Kwanza kidogo hapo. Leo hatuli pop corn wala nini, hakikisha unahesabiwa Sawa? Umuhimu wake ushasemwa Sana kwahiyo naamini kabisa tutalimaliza hili zoezi salama, hata kama hupendi ndo hivyo tena kuhesabiwa lazima!
Haya tuendelee na madini yetu Bbasi wakajadiliana na kuamua wavunje ule mlango wa cold room....lahaula! Kama walivyochezwa na machale baharia alikuwa anakaribia kuganda Kwa baridi Ile Kali...walimkuta ktk Hali mbaya Sana huenda wangechelewa kidogo mwamba angerest in peace! Lkn kama unavyojua kila mtu anakufa Tu siku yake inapofika Hilo halina ubishi! Basi walimuokoa na kumpa huduma ya Kwanza na hatimaye baada ya masaa kadhaa bey alipata nafuu na kuwa Sawa alhamdulillah.
Hekima ya story hii:
Wema unalipa...Utu unalipa ...Ubinadamu unalipa....ebu fikiria kama etugrul bey asingekuwa boss mzuri Kwa wafanyakazi wake bilashaka Leo hii bey angekuwa katika ulimwengu mwingine kabisa....haijalishi wewe Una hadhi gani ktk jamii, Una elimu kiasi gani,unahela kiasi gani, Una cheo kiasi gani...kumbuka mwisho wa siku wote bado ni binadamu na kama binadamu tunategemeana Kwa namna moja au nyingine.
Ukiwa boss mbaya unajenga uadui na watu na huenda hata wafanyakazi wanaweza kupanga kukufanyia ubaya....tafuta hii movie inaitwa THE HORRIBLE BOSSES nadhani wale waliyo icheki hii movie wanajua shughuli yake.
Ni hayo Tu.