DOKEZO UTUMISHI, Kuvuja kwa mitihani ya oral interviews Chemist II(Forensic science & toxicology Posts), Mwajiri Maabara ya Mkemia Mkuu (GCLA)

DOKEZO UTUMISHI, Kuvuja kwa mitihani ya oral interviews Chemist II(Forensic science & toxicology Posts), Mwajiri Maabara ya Mkemia Mkuu (GCLA)

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Artificial intelligence

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2021
Posts
1,265
Reaction score
2,252
Kichwa cha mada chahusika hapo juu. Usaili wa mahojiano wa nafasi tajwa hapo uliofanyika leo tarehe 08/09/2022 umegubikwa na vitendo vya udanganyifu. Maswali yote sita ya nafasi tajwa juu hapo yamevujishwa na baadhi ya maofisa wa sekretarieti ya utumishi wa umma kwa kushirikiana na viongozi kadhaa wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali yaani GCLA.

Maswali hayo yamevuja kupitia kwa msailiwa aitwaye Mercy ambaye alikuwa na maswali hayo huku akitaja baadhi ya maswali hayo na majibu yake kabla ya sahili zote mbili, TCRA Inaweza kuchunguza mawasiliano ya mtahiniwa huyo ya hivi karibuni ili kuthibitisha hili.

Ikumbukwe vitendo vya uvujishaji mitihani kwa wasailiwa kabla ya usaili havirusiwi chini ya sheria ya Utumishi ya sekretarieti ya ajira, na yeyote anayejihusisha na vitendo hivyo anastahili kuadhibiwa kisheria.

Vitendo hivyo uchangia pakubwa kuajiri incompetent personnel's katika taasisi mbali mbali na uminya haki na usawa kwa wasailiwa wote wa kada husika.

Hivyo basi napendekeza Serikali kufuatilia usaili wa mahojiano wa GCLA uliofanyika leo tarehe 08/09/2022 kupitia utumishi na endapo itajiridhisha na uwepo wa vitendo hivyo vya udanganyifu, ifute usaili huo na nafasi hizo zitangazwe upya na mchakato urudiwe chini ya usimamizi na uangalizi wa Serikali.

GCLA ni taasisi nyeti ya Serikali, hivyo inatakiwa kuajiri kwa kufuata misingi ya haki na usawa.
nape nauye
 

Pole sana
Sijafurahishwa kabisa ikizingatiwa niliacha majukumu yangu ya kikazi na kwenda Dodoma, mara nyingi naitwaga ila kutokana na majukumu yangu nashindwaga kwenda, leo nikasema ngoja nitoroke niende, kumbe mitihani ishavujishwa, maswali yalikuwa mepesi sana kwa mtu anayejua na aliyejiandaa vizuri hakukuwa na haja ya kutumia vimemo, ikizingatiwa muajiri ni taasisi nyeti inayo simamia sheria ya matumizi ya kemikali za viwandani na majumbani, tafiti za kimaabara, uchunguzi na tafiti za vina saba, mambo haya yote yanamugusa kila mtanzania katika nyanja tofauti tofauti, hivyo taasisi kama hii haitaji kuajiri mtu kwa vimemo bali competence ya mtu husika ili kutoa huduma bora kwa jamii.
 
Sijafurahishwa kabisa ikizingatiwa niliacha majukumu yangu ya kikazi na kwenda Dodoma, mara nyingi naitwaga ila kutokana na majukumu yangu nashindwaga kwenda, leo nikasema ngoja nitoroke niende, kumbe mitihani ishavujishwa, maswali yalikuwa mepesi sana kwa mtu anayejua na aliyejiandaa vizuri hakukuwa na haja ya kutumia vimemo, ikizingatiwa muajiri ni taasisi nyeti inayo simamia sheria ya matumizi ya kemikali za viwandani na majumbani, tafiti za kimaabara, uchunguzi na tafiti za vina saba, mambo haya yote yanamugusa kila mtanzania katika nyanja tofauti tofauti, hivyo taasisi kama hii haitaji kuajiri mtu kwa vimemo bali competence ya mtu husika ili kutoa huduma bora kwa jamii.
Kumbe mkuu Artificial intelligence siku hizi umetingwa ndiyo maana ulitelekeza uzi wetu wa vatican kule.
Mambo ya Serikali ni hovyo hovyo tu, endelea kukomaa huko huko private Mkuu.
 
Sijafurahishwa kabisa ikizingatiwa niliacha majukumu yangu ya kikazi na kwenda Dodoma, mara nyingi naitwaga ila kutokana na majukumu yangu nashindwaga kwenda, leo nikasema ngoja nitoroke niende, kumbe mitihani ishavujishwa, maswali yalikuwa mepesi
Kwahio Mwizi anamshtaki Mwizi ?!!!
 
Hebu tupia hayo maswali tuyaone kwa ushahidi zaidi,mmeulizwa vitu gani huko oral Leo kwenye hizo Posts
 
Back
Top Bottom