Utumishi ya Kapteni Mkuchika wa awamu ya tano hii imekuwa mbaya na kisiasa zaidi

Utumishi ya Kapteni Mkuchika wa awamu ya tano hii imekuwa mbaya na kisiasa zaidi

Kuhusu kupandishwa na mishahara, tatizo ni maafida utumishi, hao ndiyo mchwa na wanastahili kufungwa au kufukuzwa kazi.

Wala huna haja ya kumtetea Jiwe ,Sheria ni zenu/ Majeshi ni yenu/Mahakama ni zenu mnashindwa nini kuwa wajibisha hao wanao kosea !!??
 
Kila siku watumishi wa umma wamekuwa wa kulialia, huu ni ujinga uliopitiliza! Kila siku kila siku as if hakuna maswala mengine zaidi ya maslahi yao, mbaya zaidi ukienda kuhudumiwa na hao watumishi wa umma ndipo utapochoka kabisa wamejaa viburi dharau za kila aina!
Nasemaje, Magu kanyaga twende wabane hivyo hivyo hadi akiki ziwakae sawa

Sent using Jamii Forums mobile app

Wewe endelea kumsifia huyo mungu wako. Ila kiufupi tu watumishi wa umma tulio wengi kwa sasa tunazingua tu kwenye maeneo yetu ya kazi. Ukweli ni kwamba, hatuna tena morali ya kazi kama ilivyokuwa enzi za JK.

Na umwambie asipokubali kubadilika, basi tutazingua zaidi. Hakuna mgomo mtamu kama ule wa kugomea moyoni. Utamlazimisha punda kwenda mtoni, ila hutaweza kumlazimisha kunywa maji.
 
Tarehe 01/05/2020 mambo yatakuwa mazuri kwa Watumishi wa Umma wote na Wafanyakazi wa Umma wote.

Kwasasa nimelazimika kutofautisha kati ya Watumishi wa umma na Wafanyakazi wa umma.

WATUMISHI WA UMMA:
Ni wale wanaokula Good life Mawizarani hasa serikali Kuu.

WAFANYAKAZI WA UMMA:
Ndiyo kina sisi, Walimu, Health Personnels wanaokimbia wagonjwa wa Corona and Co. Mostly ni wale wa Local Government.
Hawa wanaajiriwa Maskini na Wanastaafu wakiwa Maskini kwasababu si Watumishi bali ni Wafanyakazi wa Umma.

KN
 
Miaka mitano hakuna nyongeza ya mishahara alafu uchumi keshautibua. Gharama za maisha na familia zimeongezeka.

Kisha unamkuta fundi rangi,nguo,selemara,kupaua anamsifia Jiwe kwa kubana watumishi! Kesho yake analalamika kazi hamna au amepata amelipwa kidogo ila njaa tu ndio imemfanya akubali,au kakimbiwa na nesi/daktari wakati anaumwa 'kohona'!

Hawajui kuwa baba mbabaishaji huzaa watoto wabaishaji!
 
Tarehe 01/05/2020 mambo yatakuwa mazuri kwa Watumishi wa Umma wote na Wafanyakazi wa Umma wote.

Kwasasa nimelazimika kutofautisha kati ya Watumishi wa umma na Wafanyakazi wa umma.

WATUMISHI WA UMMA:
Ni wale wanaokula Good life Mawizarani hasa serikali Kuu.

WAFANYAKAZI WA UMMA:
Ndiyo kina sisi, Walimu, Health Personnels wanaokimbia wagonjwa wa Corona and Co. Mostly ni wale wa Local Government.
Hawa wanaajiriwa Maskini na Wanastaafu wakiwa Maskini kwasababu si Watumishi bali ni Wafanyakazi wa Umma.

KN
Ndugu yangu yupo Wizarani lkn malalamiko ni yale yale tu. Wizara inayokula good time labda ni ile ya Fedha na Mipango tu - najua pia unajua PS wake ni nani?
 
Miaka mitano hakuna nyongeza ya mishahara alafu uchumi keshautibua. Gharama za maisha na familia zimeongezeka.

Kisha unamkuta fundi rangi,nguo,selemara,kupaua anamsifia Jiwe kwa kubana watumishi! Kesho yake analalamika kazi hamna au amepata amelipwa kidogo ila njaa tu ndio imemfanya akubali,au kakimbiwa na nesi/daktari wakati anaumwa 'kohona'!

Hawajui kuwa baba mbabaishaji huzaa watoto wabaishaji!
Umetoa mfano mzuri sana ni kweli hapa Idukilo kuna Mfanyakazi anajenga ila ameishia kwenye renta mwaka wa pili sasa huu
 
Kila siku watumishi wa umma wamekuwa wa kulialia, huu ni ujinga uliopitiliza! Kila siku kila siku as if hakuna maswala mengine zaidi ya maslahi yao, mbaya zaidi ukienda kuhudumiwa na hao watumishi wa umma ndipo utapochoka kabisa wamejaa viburi dharau za kila aina!
Nasemaje, Magu kanyaga twende wabane hivyo hivyo hadi akiki ziwakae sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa wakiwa na jazba zenye msingi wa madai yao ya kisheria, inategemea wakuhudumie wakiwa na furaha kweli?

Wakati huo mtu amefura hasira za Kodi,bills,kofokewa fokewa na "politicians" wajinga wajinga,unatarajia nini?

Maana eti mpaka wenye viti wa serikali za mitaa/vijiji wanakuwa maboss wa manesi,walimu,matabibu,na waajiriwa wengineo! Hahahaaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu wimbo wa nyongeza ya mshahara nimekuwa nikiusikia kila inapokaribia Mei Mosi, hakuna mwaka ambao sijausikia, hivi kwa mfano ndio serikali ikawa inaongeza mshahara kila mwaka kama watumishi wanavyotaka, si unaweza kuta mtu analipwa milioni mia mbili sasa??

Nashauri tu pale mnapoweza kutafuta chanzo kingine cha mapato na kuacha sasa fedha ziende kuimarisha sekta nyingine pia, sio kupandisha mishahara tu kila mwaka.
 
Sasa wakiwa na jazba zenye msingi wa madai yao ya kisheria, inategemea wakuhudumie wakiwa na furaha kweli?

Wakati huo mtu amefura hasira za Kodi,bills,kofokewa fokewa na "politicians" wajinga wajinga,unatarajia nini?

Maana eti mpaka wenye viti wa serikali za mitaa/vijiji wanakuwa maboss wa manesi,walimu,matabibu,na waajiriwa wengineo! Hahahaaa...

Sent using Jamii Forums mobile app
Du! Kumbe unajua kweli mfumo wa uongozi wa nchi hii. Yaani Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji anayetoka CCM hapa TZ ana nguvu kuliko hata Katibu Mkuu wa Wizara. Usione akina Kitila Mkumbo wanataka ubunge - sio mchezo babake!
 
Huu wimbo wa nyongeza ya mshahara nimekuwa nikiusikia kila inapokaribia Mei Mosi, hakuna mwaka ambao sijausikia, hivi kwa mfano ndio serikali ikawa inaongeza mshahara kila mwaka kama watumishi wanavyotaka, si unaweza kuta mtu analipwa milioni mia mbili sasa??

Nashauri tu pale mnapoweza kutafuta chanzo kingine cha mapato na kuacha sasa fedha ziende kuimarisha sekta nyingine pia, sio kupandisha mishahara tu kila mwaka.
Kaka inawezakana we unafanyia kazi Benki Kuu au Wizara ya Fedha ndiyo maana unatapika tu hovyohovyo!
 
Kaka inawezakana we unafanyia kazi Benki Kuu au Wizara ya Fedha ndiyo maana unatapika tu hovyohovyo!
Hapana mkuu mimi ni mkulima ambaye kodi yangu ndio hiyo wafanyakazi wanayotaka kujipendelea nayo kila mwaka, ni muda muafaka sasa mkajifunza kutengeneza vyanzo vingine vya mapato na sio kutunyonya sisi wanyonge. Kuna mambo mengine muhimu pia ya kufanya sio mishahara yenu tu. eboo.
 
Hapana mkuu mimi ni mkulima ambaye kodi yangu ndio hiyo wafanyakazi wanayotaka kujipendelea nayo kila mwaka, ni muda muafaka sasa mkajifunza kutengeneza vyanzo vingine vya mapato na sio kutunyonya sisi wanyonge. Kuna mambo mengine muhimu pia ya kufanya sio mishahara yenu tu. eboo.
Mie pia sio mfanyakazi na kilichonishinda ni manyanyaso wanayoyapata. Ninanunua mazao unayolima wewe then nauza ninapata mahela. Ila ukweli hayo mahela hayaji vizuri siku hizi kwa sababu walaji wengi ni wafanyakazi wa Umma ambao ni kweli kwa sasa baadhi wanadhalilika isipokuwa wachache waliowekwa sehemu zenye neema! Kwa maana hiyo wana haki ya kualalamika ili wasikike!
 
Ukweli niliamua kuacha kazi mwishoni mwa Mwaka 2016 na nikaamua kurudi kijijini na nyumbani kwetu Idukilo Shinyanga na kuanza kazi zangu za biashara. Kilichonifanya niache kazi ni kutokana na tu na maamuzi ya kibabe ya watu wenye mamlaka kuamua kibabe kuhusu mambo ya mtumishi wa umma hata kama hajapenda.

Kwa kifupi nilihamishwa kibabe kutoka mkoa ambao tayari nilishawekeza na kutokana na mshahara mdogo wa utumishi wa umma basi kipato changu cha ziada kikawa kinanifanya niishi vizuri.

Hilo likawakera binadamu wenzangu wakanisema vibaya na kuniundia majungu tu hadi nikahamishwa kupelekwa Dar es Salaam

Dar es Salaam yao ikanishinda - pamoja na kushawishiwa sana kwamba mambo yataniendea vizuri nikaona siwezi kumudu nikaacha kazi na kwa umri wangu ulivyo nisingeweza kustaafu kwa hiari.

Naambiwa eti vihela vyangu vya pensheni nisubiri nifikishe miaka 55 - na sasa nimebakiza miaka minne sasa kuifikia hiyo 55 - Mwenyezi Mungu anijalie nisife angalau nivipate hivyo vihela.

Pamoja na kutokuwa kwenye ajira kwa kweli kadri siku zinavyoenda naona watumishi wenzangu waliobaki bado wanaendelea kunyanyasika sana. Kuna mambo kadhaa ambayo yamejitokeza katika awamu hii ambayo yanaonekana kama kuboresha utumishi lakini kumbe yanakandamiza zaidi, nimeorodhesha kwa mtiririko ufuatao:

1. Kwa sasa hivi watumishi wa umma hawafikiriwi kabisa kwenye mambo ya uhamisho - mtu anaomba uhamisho lkn hajibiwi na utumishi wapo kimya tu. Yule ambaye hajaomba uhamisho anahamishwa kibabe - tena anahamishwa bila hata kupewa stahili zake za kiutumishi anaambia atalipwa malimbikizo.

2. Watumishi wengi wameandikiwa barua za kupandishwa vyeo lakini mabadiliko kwenye mishahara yao hayafanyiki. Kinachofanyika sasa ni kuziandika barua hizo kwa tarehe ya mbele ili wasidai malimbikizo - mwenyewe mpaka ninaacha kazi mwishoni wa 2016 sikuwa nimerekebishiwa mshahara pamoja na kuwa nilishapata barua ya kupandishwa cheo kwa miezi zaidi ya 8 nyuma. Nasimuliwa na wenzangu tangu niondoke wamebadilishiwa barua za kupandishwa vyeo mara kibao ili kuzuia wasidai malimbikizo.

3. Hata watumishi ambao wanakaimu nao wanakaimishwa zaidi hata ya miaka miwili bila kulipwa stahiki zao na wanapotolewa kwenye nafasi za kukaimu hawana tena nafasi ya kudai maslahi waliyokaimia.

4. Kwa sasa hata Sheria ya Utumishi inadaiwa imebadilishwa na Katibu Mkuu wa utumishi anaweza kukuhamisha popote pale, kukupunguza cheo au hata kukupandisha tu cheo hata kama hustahili na hawezi kufanywa chochote.

5. Wanasiasa kama kina Mkuchika kwa sasa wanawachukia watumishi wa umma - kumekuwa na mpambano ambao upo indirect, wanasiasa hawaongelei kabisa maslahi ya wafanyakazi katika mtazamo chanya. Juzi Mkuchika kaongelea kuhusu kucheleweshwa kwa mafao ya wastaafu lakini hakuongelea kabisa kuhusu wafanyakazi ambao bado wapo kazini na wana madai kibao.

Hakuongelea kuhusu nyongeza za mishahara, hakuongelea kuhusu manyanyaso ya uhamisho wa kibabe, hakuongelea kuhusu ajira mpya na za wazi ambazo hawataki kuziziba, hakuongelea kuhusu, kuthibitisha wale ambao wanapandishwa vyeo, hakuongelea kuhusu malimbikizo ya madai mbalimbali ya watumishi km malipo ya uhamisho, nyongeza za mishahara, nyongeza za pensheni, nk.

Kwa ujumla wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamekuwa kitu kimoja. Wanawanyanyasa na kuwanyonya watumishi wa umma. Watumishi wa Umma wanawafanyia wanasiasa kazi zao, wanawalipa viongozi wa vyama vya wafanyakazi ada zinazowajaza matumbo yao lakini wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamenyamaza kimywa. Hii sio haki, tena sio haki kabisa.

Kilichobaki kwa wenzangu mlio bado kwenye ajira msimame kidete kuangalia maslahi yenu, wanasiasa na vyama vya wafanyakazi hawana maana kwenu, waondosheni kwa kutumia utaratibu wa kidemokrasia - ondoa wanasiasa kwa kura na ondoa viongozi wa vyama vya wafanyakazi kwa kura. Mtaniona mimi mwoga - sawa mie mwoga lkn mwaka huu hata Chama changu cha Mapinduzi naona sitakipa kura.

Nimeamua hata kama sitagombea lakini nitapigia kura upinzani isipokuwa tu pale mgombea wa CCM mwenye moyo wa dhati kuyaondoa hayo atajitokeza na kwa sura yake nikaamini anaweza kufanya kitu. Tusipofanya uamuzi mzuri kina Mkuchika wataendelea tu na maneno yao yasiyo na msaada wowote.

Asanteni na Mwenyezi Mungu azidi kutuepusha na balaa la #COVID19

Keep distance and please vaa Barakoa.

Its Tila Lila2 me
Kama akili hawana acha wanyanyaswe tu maana hakuna namna nyingine
 
Kila siku watumishi wa umma wamekuwa wa kulialia, huu ni ujinga uliopitiliza! Kila siku kila siku as if hakuna maswala mengine zaidi ya maslahi yao, mbaya zaidi ukienda kuhudumiwa na hao watumishi wa umma ndipo utapochoka kabisa wamejaa viburi dharau za kila aina!
Nasemaje, Magu kanyaga twende wabane hivyo hivyo hadi akiki ziwakae sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbwakoko wewe [emoji34][emoji34][emoji34][emoji34]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom