Utumivu wa maneno kimakosa katika kiswahili

Utumivu wa maneno kimakosa katika kiswahili

De Opera

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2013
Posts
780
Reaction score
1,664
Wapwa, habari za muda huu?

Kuna neno 'Onyesha' naona linatumika vibaya na mara nyingi limekuwa likitumika mahali ambapo si mahali pake.

Kuna maneno mawili watu tumekuwa tukiyachanganya 'Onesha' na 'Onyesha'.

'Onesha' likisimama kwa maana ya kumfanya mtu atazame kitu au jambo fulani, wakati 'Onyesha' likisimama kwa maana ya kumkataza au kumzuia mtu ama kiumbe chochote kisifanye jambo fulani.

Sasa hapo nimeona kwa watu wengi wakitumia Onyesha badala ya Onesha.

Mfano hata kwenye mabango makubwa unakuta yameandikwa 'MAONYESHO YA SABASABA' , 'MAONYESHO YA NANENANE', na mengine mengi.

Sasa ile ni sehemu ya kuwaonya watu au ni sehemu ya kuwafanya watu waone bidhaa?

Maana mimi ninavyojua 'Maonyesho' ni mahali ambapo mtu anapewa maonyo na 'Maonesho' ni sehemu ambapo mtu anaoneshwa jambo fulani.

Sasa unakuta mtu kakoma kaonyeshwa mzigo sio wenyewe, usiku kaota akaonyeshwa jumba la kifahari.

Ahsanteni wapwa, tunaelimishana tu kidogo!
 
Upo sawa,

Vipi kuna wale hawajui matumizi mazuri ya sarufi una kuta kwenye R ana weka L pia kwenye L ana weka R [emoji849]

Yaani yeye mara nyingi anaenda kinyume nyume hawa nao mimi huwa wana ni boa sana halafu wengine sio kwenye kuandika tu, bali hata anavyo ongea.

Unakuta matamshi kisarufi bado ana puyanga mfano mtu ana itwa Laban yeye ata mwita Raban [emoji23] pia kwenye kweli yeye atasema kweri hamja wahi kukutana na watu wa namna hii...!? [emoji1787][emoji1787]
 
Upo sawa,

Vipi kuna wale hawajui matumizi mazuri ya sarufi una kuta kwenye R ana weka L pia kwenye L ana weka R [emoji849]

Yaani yeye mara nyingi anaenda kinyume nyume hawa nao mimi huwa wana ni boa sana halafu wengine sio kwenye kuandika tu, bali hata anavyo ongea.

Unakuta matamshi kisarufi bado ana puyanga mfano mtu ana itwa Laban yeye ata mwita Raban [emoji23] pia kwenye kweli yeye atasema kweri hamja wahi kukutana na watu wa namna hii...!? [emoji1787][emoji1787]
Hivi lipi neno sahihi kati ya kuroga na kuloga....?
 
Wapwa, habari za muda huu?
Kuna neno 'Onyesha' naona linatumika vibaya na mara nyingi limekuwa likitumika mahali ambapo si mahali pake.

Kuna maneno mawili watu tumekuwa tukiyachanganya 'Onesha' na 'Onyesha'.

'Onesha' likisimama kwa maana ya kumfanya mtu atazame kitu au jambo fulani, wakati 'Onyesha' likisimama kwa maana ya kumkataza au kumzuia mtu ama kiumbe chochote kisifanye jambo fulani.

Sasa hapo nimeona kwa watu wengi wakitumia Onyesha badala ya Onesha.

Mfano hata kwenye mabango makubwa unakuta yameandikwa 'MAONYESHO YA SABASABA' , 'MAONYESHO YA NANENANE', na mengine mengi.
Sasa ile ni sehemu ya kuwaonya watu au ni sehemu ya kuwafanya watu waone bidhaa?
Maana mimi ninavyojua 'Maonyesho' ni mahali ambapo mtu anapewa maonyo na 'Maonesho' ni sehemu ambapo mtu anaoneshwa jambo fulani.
Sasa unakuta mtu kakoma kaonyeshwa mzigo sio wenyewe, usiku kaota akaonyeshwa jumba la kifahari.

Ahsanteni wapwa, tunaelimishana tu kidogo!
Mkuu naomba kupingana na wewe, kamusi ya Kiswahili ya TUKI imetafsiri neno onyesha kama show, exhibit, demonstrate na yote yanapingana na ulichosema hapa.
Kuna shida ya matumizi ya maneno ndiyo na ndio na siyo na sio watu wanayachanganya sana na pia kupenda kutumia baadae wakati ni neno halisi ni baadaye
 
Utumivu ndio nini tena jamani kiswahili kweli lugha pana
 
Shida watu walio wengi taifa hili wana Usonji ulio sugu. Kwahiyo hatuna namna. TUTALITIZAMA NA HILI.
 
Upo sawa,

Vipi kuna wale hawajui matumizi mazuri ya sarufi una kuta kwenye R ana weka L pia kwenye L ana weka R [emoji849]

Yaani yeye mara nyingi anaenda kinyume nyume hawa nao mimi huwa wana ni boa sana halafu wengine sio kwenye kuandika tu, bali hata anavyo ongea.

Unakuta matamshi kisarufi bado ana puyanga mfano mtu ana itwa Laban yeye ata mwita Raban [emoji23] pia kwenye kweli yeye atasema kweri hamja wahi kukutana na watu wa namna hii...!? [emoji1787][emoji1787]
Mimi nirikura wari mchafu ukanizulu! 😂😂. Sasa hapa utajua unaongea na mtu wa aina gani!
 
Mkuu naomba kupingana na wewe, kamusi ya Kiswahili ya TUKI imetafsiri neno onyesha kama show, exhibit, demonstrate na yote yanapingana na ulichosema hapa.
Kuna shida ya matumizi ya maneno ndiyo na ndio na siyo na sio watu wanayachanganya sana na pia kupenda kutumia baadae wakati ni neno halisi ni baadaye
Mkuu hapo ni kimakosa, walioandika nao ni watu.

Kwa hiyo mkuu na wewe unaona kabisa ni kweli kwamba 'Onyesha' ni 'Show'?

Hapanaaa!
'Onyesha' ni kumuadhibu mtu kutokana na kosa alilofanya, eitha kwa maneno ama vitendo.

Nisawa na mchezaji anapocheza rafu, anaonywa kwa kadi ya njano au nyekundu.
 
Shida watu walio wengi taifa hili wana Usonji ulio sugu. Kwahiyo hatuna namna. TUTALITIZAMA NA HILI.
😂😂 sawa! taimu izi makangabiliti, watakaa tu sawa.
 
Mkuu naomba kupingana na wewe, kamusi ya Kiswahili ya TUKI imetafsiri neno onyesha kama show, exhibit, demonstrate na yote yanapingana na ulichosema hapa.
Kuna shida ya matumizi ya maneno ndiyo na ndio na siyo na sio watu wanayachanganya sana na pia kupenda kutumia baadae wakati ni neno halisi ni baadaye
Onyesha = Onyo
Onesha = Ona

Niliwahi kuwasikia BAKITA wakiweka sawa jambo hili. TUKI najua wataweka sawa kwenye matoleo yao mapya
 
Back
Top Bottom