Uuguzi wa Tanzania sio kada ya mtu kujivunia kusoma

Uuguzi wa Tanzania sio kada ya mtu kujivunia kusoma

imekuaje

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2024
Posts
221
Reaction score
426
Habari.

Mimi ni kijana wa kiume niliyebahatika kusoma uuguzi nchini Tanzania.

Nipende kuwapongeza wote waliobahatika kusoma uuguzi Tanzania maana moja ya kada inayoiendesha hospitali kwa asilimia kubwa sana na wanasaidia wagonjwa maana ndio wanaoshinda nao masaa 24.

Niseme ukweli mimi nitakuwa wa kwanza kuuacha uuguzi pindi nitakapoenda kujiendeleza elimu ya juu.

Nilisoma nikiwa na mapenzi ya dhati sana na moyo wangu ukiipenda hii kazi lakini niliyokutana nayo kazini ni Tofauti na hayo ndio yananifanya nikiri nitaiacha hii fani mapema sana.

1.Uuguzi Tanzania ni miongoni mwa kada za afya zinazodharaulika kupita kiasi na inaonekana kada ha watu wasio na akili hali ambayo ni tofauti kwa nchi za ulaya na uarabuni .

2.Upande wa maslahi uuguzi haiwezekani muuguzi wa degree Mwenye kusoma miaka minne sawa na mfamasia ,fizio yeye akalipwa TGHs C (around million 1 basics) wakati wenzake wakaanza na TGHs D(around million 1.3basics) na mpaka sasa inaonekana kawaida.

3.Upande wa Hopitali muuguzi anaongozea kudharauliwa sana na watu wa kada nyingine Hasa medical doctor kwa kumchukulia muuguzi kama mtu aliye muoa(mke wake)kiasi kwamba hospital nyingine hasa za mission wauguzi wamekuwa wakiwekeana zamu ya kuwapikia na kuwaandalia madaktari chakula.

4.Jamii inamuona muuguzi katili na mtu Mwenye majibu ya ovyo hali ambayo ni tofauti kwa wauguzi wa hivi karibuni wanaojaribu kupambana kwa hali na mali kubadilisha Hadhi ya uuguzi lakini bado hali inaonekana muuguzi ni katili ndo maana kila lawama za hospitali ni MUUGUZI.

5.Muuguzi Hajapewa nafasi ya maamuzi ya matibabu kwa mgonjwa hata kwenye emergency kiasi kwamba kutoa panadol tu mpaka amsubiri daktari hali ambayo ni tofauti kwa nchi za wenzetu hasa ulaya na muuguzi hajawekwa sehemu ya uongozi wala maamuzi ya hospital ilhali muuguzi wa degree Anasoma vitu vingi vinavyohusu mgonjwa na uongozi pia.

6.Chama cha Wauguzi TANNA na TNMC haviko katika minajili ya kumsaidia muuguzi zaidi ya kumkandamiza na kumnyanyasa ndo maana kila siku kazi yao kuongelea maadili lakini wanamwacha muuguzi huyu kwenye mazingira magumu kumsaidia kwenye masuala ya maslahi ,hela ya overtime ,na haki zake binafsi.

Wauguzi wa nchi za wenzetu kama Nchi za ulaya wameufanya ionekane kada bora na yenye malipo mazuri na zaidi kuwafanya wafanye kazi kwa ufanisi na kuspelize kabisa kama muuguzi wa watoto,usingizi,magonjwa tofauti na nchi ya Tanzania muuguzi amekuwa ni kilaka wa kufanya kazi popote pale .


Muuguzi wa ulaya analipwa hela nzuri kwa lisaa wengine hasa wa ICU wamezidi mishahara hata baadhi ya madaktari.


Kiukweli mambo ni mengi ila kama kada ya uuguzi Tanzania haitabadilika tutarajie kupunguza idadi kubwa ya vijana kusoma uuguzi hasa wanaume.


Wa kwanza nitakuwa Mimi.
 
Kiufupi, Kada ya Afya nchini ina matatizo mengi sana ambayo yana discourage sana watu waliosoma hizo course za Afya bila kuwa na wito wa hizo kada zenyewe kuendelea na kazi. Changamoto zilizokuwepo humo zinaweza kuvumiliwa na wataalam wenye wito tu pekee. Mdogo wangu kama yamekushinda, wewe jiengue tu, hautakuwa wa kwanza nor the last.

Main question should be, ukiacha hio kazi unaenda kufanya nini..??
 
Kiufupi, Kada ya Afya nchini ina matatizo mengi sana ambayo yana discourage sana watu waliosoma hizo course za Afya bila kuwa na wito wa hizo kada zenyewe kuendelea na kazi. Changamoto zilizokuwepo humo zinaweza kuvumiliwa na wataalam wenye wito tu pekee. Mdogo wangu kama yamekushinda, wewe jiengue tu, hautakuwa wa kwanza nor the last.

Main question should be, ukiacha hio kazi unaenda kufanya nini..??
Of course Mimi nitajiengua mapema sana wala sitaweza kufika umri wa kustafu nipo kwenye hii kada.

Bora niwe winga kariakoo
 
Kiufupi, Kada ya Afya nchini ina matatizo mengi sana ambayo yana discourage sana watu waliosoma hizo course za Afya bila kuwa na wito wa hizo kada zenyewe kuendelea na kazi. Changamoto zilizokuwepo humo zinaweza kuvumiliwa na wataalam wenye wito tu pekee. Mdogo wangu kama yamekushinda, wewe jiengue tu, hautakuwa wa kwanza nor the last.

Main question should be, ukiacha hio kazi unaenda kufanya nini..??
Hapana siachi uzuri nina diploma na Niko Serikali.

Nitaenda kusoma kada nyingine ziko nyingi kwa hii diploma nitasoma nadhani nitapumzika kidogo.
 
Habari.

Mimi ni kijana wa kiume niliyebahatika kusoma uuguzi nchini Tanzania.

Nipende kuwapongeza wote waliobahatika kusoma uuguzi Tanzania maana moja ya kada inayoiendesha hospitali kwa asilimia kubwa sana na wanasaidia wagonjwa maana ndio wanaoshinda nao masaa 24.

Niseme ukweli mimi nitakuwa wa kwanza kuuacha uuguzi pindi nitakapoenda kujiendeleza elimu ya juu.

Nilisoma nikiwa na mapenzi ya dhati sana na moyo wangu ukiipenda hii kazi lakini niliyokutana nayo kazini ni Tofauti na hayo ndio yananifanya nikiri nitaiacha hii fani mapema sana.

1.Uuguzi Tanzania ni miongoni mwa kada za afya zinazodharaulika kupita kiasi na inaonekana kada ha watu wasio na akili hali ambayo ni tofauti kwa nchi za ulaya na uarabuni .

2.Upande wa maslahi uuguzi haiwezekani muuguzi wa degree Mwenye kusoma miaka minne sawa na mfamasia ,fizio yeye akalipwa TGHs C wakati wenzake wakaanza na TGHs D na mpaka sasa inaonekana kawaida.

3.Upande wa Hopitali muuguzi anaongozea kudharauliwa sana na watu wa kada nyingine Hasa medical doctor kwa kumchukulia muuguzi kama mtu aliye muoa(mke wake)kiasi kwamba hospital nyingine hasa za mission wauguzi wamekuwa wakiwekeana zamu ya kuwapikia na kuwaandalia madaktari chakula.

4.Jamii inamuona muuguzi katili na mtu Mwenye majibu ya ovyo hali ambayo ni tofauti kwa wauguzi wa hivi karibuni wanaojaribu kupambana kwa hali na mali kubadilisha Hadhi ya uuguzi lakini bado hali inaonekana muuguzi ni katili ndo maana kila lawama za hospitali ni MUUGUZI.

5.Muuguzi Hajapewa nafasi ya maamuzi ya matibabu kwa mgonjwa hata kwenye emergency kiasi kwamba kutoa panadol tu mpaka amsubiri daktari hali ambayo ni tofauti kwa nchi za wenzetu hasa ulaya na muuguzi hajawekwa sehemu ya uongozi wala maamuzi ya hospital ilhali muuguzi wa degree Anasoma vitu vingi vinavyohusu mgonjwa na uongozi pia.

6.Chama cha Wauguzi TANNA na TNMC haviko katika minajili ya kumsaidia muuguzi zaidi ya kumkandamiza na kumnyanyasa ndo maana kila siku kazi yao kuongelea maadili lakini wanamwacha muuguzi huyu kwenye mazingira magumu kumsaidia kwenye masuala ya maslahi ,hela ya overtime ,na haki zake binafsi.

Wauguzi wa nchi za wenzetu kama Nchi za ulaya wameufanya ionekane kada bora na yenye malipo mazuri na zaidi kuwafanya wafanye kazi kwa ufanisi na kuspelize kabisa kama muuguzi wa watoto,usingizi,magonjwa tofauti na nchi ya Tanzania muuguzi amekuwa ni kilaka wa kufanya kazi popote pale .


Muuguzi wa ulaya analipwa hela nzuri kwa lisaa wengine hasa wa ICU wamezidi mishahara hata baadhi ya madaktari.


Kiukweli mambo ni mengi ila kama kada ya uuguzi Tanzania haitabadilika tutarajie kupunguza idadi kubwa ya vijana kusoma uuguzi hasa wanaume.


Wa kwanza nitakuwa Mimi.
Unapoandika toa ufafanuzi wa nnya unazoziandika!! Sasa mtu wa kawaida ukimwandikia "TGHs C na TGHs D" ndo vitu gani? Mxiuuuuh!
 
Of course Mimi nitajiengua mapema sana wala sitaweza kufika umri wa kustafu nipo kwenye hii kada.

Bora niwe winga kariakoo
Be careful na unachokitamani. Mtaani napo pako hovyo kijana. Jaribu kuangalia fursa za kwenda kufanya kazi nje ya nchi kwa taaluma yako. Mahitaji yenu huko nje ni makubwa sana. Seek right information, jiwekee na period of time kwamba mpaka mwaka fulani sitakuwa hapa tena.
 
Be careful na unachokitamani. Mtaani napo pako hovyo kijana. Jaribu kuangalia fursa za kwenda kufanya kazi nje ya nchi kwa taaluma yako. Mahitaji yenu huko nje ni makubwa sana. Seek right information, jiwekee na period of time kwamba mpaka mwaka fulani sitakuwa hapa tena.
Hii nilijiwekea nakumbuka nilikuwa natamani sana kwenda Canada na hii ndoto nimekuwa nayo muda mrefu.

Changamoto kila nikifuatilia sijapata taarifa sahihi hadi leo.
 
Be careful na unachokitamani. Mtaani napo pako hovyo kijana. Jaribu kuangalia fursa za kwenda kufanya kazi nje ya nchi kwa taaluma yako. Mahitaji yenu huko nje ni makubwa sana. Seek right information, jiwekee na period of time kwamba mpaka mwaka fulani sitakuwa hapa tena.
Asante
 
Habari.

Mimi ni kijana wa kiume niliyebahatika kusoma uuguzi nchini Tanzania.

Nipende kuwapongeza wote waliobahatika kusoma uuguzi Tanzania maana moja ya kada inayoiendesha hospitali kwa asilimia kubwa sana na wanasaidia wagonjwa maana ndio wanaoshinda nao masaa 24.

Niseme ukweli mimi nitakuwa wa kwanza kuuacha uuguzi pindi nitakapoenda kujiendeleza elimu ya juu.

Nilisoma nikiwa na mapenzi ya dhati sana na moyo wangu ukiipenda hii kazi lakini niliyokutana nayo kazini ni Tofauti na hayo ndio yananifanya nikiri nitaiacha hii fani mapema sana.

1.Uuguzi Tanzania ni miongoni mwa kada za afya zinazodharaulika kupita kiasi na inaonekana kada ha watu wasio na akili hali ambayo ni tofauti kwa nchi za ulaya na uarabuni .

2.Upande wa maslahi uuguzi haiwezekani muuguzi wa degree Mwenye kusoma miaka minne sawa na mfamasia ,fizio yeye akalipwa TGHs C (around million 1 basics) wakati wenzake wakaanza na TGHs D(around million 1.3basics) na mpaka sasa inaonekana kawaida.

3.Upande wa Hopitali muuguzi anaongozea kudharauliwa sana na watu wa kada nyingine Hasa medical doctor kwa kumchukulia muuguzi kama mtu aliye muoa(mke wake)kiasi kwamba hospital nyingine hasa za mission wauguzi wamekuwa wakiwekeana zamu ya kuwapikia na kuwaandalia madaktari chakula.

4.Jamii inamuona muuguzi katili na mtu Mwenye majibu ya ovyo hali ambayo ni tofauti kwa wauguzi wa hivi karibuni wanaojaribu kupambana kwa hali na mali kubadilisha Hadhi ya uuguzi lakini bado hali inaonekana muuguzi ni katili ndo maana kila lawama za hospitali ni MUUGUZI.

5.Muuguzi Hajapewa nafasi ya maamuzi ya matibabu kwa mgonjwa hata kwenye emergency kiasi kwamba kutoa panadol tu mpaka amsubiri daktari hali ambayo ni tofauti kwa nchi za wenzetu hasa ulaya na muuguzi hajawekwa sehemu ya uongozi wala maamuzi ya hospital ilhali muuguzi wa degree Anasoma vitu vingi vinavyohusu mgonjwa na uongozi pia.

6.Chama cha Wauguzi TANNA na TNMC haviko katika minajili ya kumsaidia muuguzi zaidi ya kumkandamiza na kumnyanyasa ndo maana kila siku kazi yao kuongelea maadili lakini wanamwacha muuguzi huyu kwenye mazingira magumu kumsaidia kwenye masuala ya maslahi ,hela ya overtime ,na haki zake binafsi.

Wauguzi wa nchi za wenzetu kama Nchi za ulaya wameufanya ionekane kada bora na yenye malipo mazuri na zaidi kuwafanya wafanye kazi kwa ufanisi na kuspelize kabisa kama muuguzi wa watoto,usingizi,magonjwa tofauti na nchi ya Tanzania muuguzi amekuwa ni kilaka wa kufanya kazi popote pale .


Muuguzi wa ulaya analipwa hela nzuri kwa lisaa wengine hasa wa ICU wamezidi mishahara hata baadhi ya madaktari.


Kiukweli mambo ni mengi ila kama kada ya uuguzi Tanzania haitabadilika tutarajie kupunguza idadi kubwa ya vijana kusoma uuguzi hasa wanaume.


Wa kwanza nitakuwa Mimi.
Wale failures wote sekondari siku hizi naona ndio wauguzi.
 
mkuu unatakiwa ujiproud ww mwenyew kwanza kwa kusoma huo uuguzi, kuna watu wanazibua vyoo na wanajiproud sembuse wewe? then ondoa iyo dhana ya kutaka kuheshimika bila pesa, kiufupi sio uuguz wala sio udaktar, watumishi wa umma hawaheshimiki na wanamaisha magumu, heshima ni pesa mkuu sio kadegree ulichokua nacho iko cha uuguz au Md, pafanye hapo kwenye uuguzi ndio daraja la kutoboa kimaisha, kopa zako weka plan zako vizur ukiona vimekaa sawa achana na makazi aya ya utumishi wa umma, iyo ishu ya kada yenu watoto wa kike kupikia madaktar ni dhana tu ambayo wauguz wakike wamejiwekea kuwanyenyekea hao madaktar na wakat mwingine mtu anapewa huduma zaidi yabkupikiwa,iyo ni watoto wa kike wenyew wamejiweka ivyo...wauguzi ni kada muhimu sana katika vituo vyetu vya kutolea huduma, jiproud kaka usitake had watu waanze kukusifia kitaa haina maana, we piga kazi feel proud..
 
Sasa mkuu ukisema hivyo wewe,Mwalimu au Polisi naye asemeje kwa nchi hii?
Kwa kifupi kazi za Afya ni moja ya kazi za wito!
Mimi ni Mteknolojia wa Radiology nashukuru hakuna mwanangu aliyeisomea!
Kwa nchi yetu ukiwa katika fani hizo ni bora mkono uende kinywani.
Mwisho jitahidi uipende fani yako!
 
Sio wote lkn wauguzi wengi ni pilipili wanaongea vibaya mno mno mno....
 
1. Si kweli kwamba uuguzi unadharaulika sana. Japokuwa kuna baadhi ya wajinga wana udharau.

2. hapo nakuunga mkono.

3. Hapa majibu ni kama namba moja.
Lakini pia wauguzi wenyewe mnasababisha kudharauliwa kwa sababu ya kutokujitambua. wengi majukumu yao hawayajui, wanasubiri kutumwa na kada nyingine, na hata wakipewa orders hawatekelezi kama standard zinavyotaka.
Matokeo yake ni kudharaulika na kutumwa kuchemsha chai.

Hivi wewe Muuguzi unaejitambua umesoma three years au four years unakubalije kwenda kumchemshia chai mtu mwingine Hayo yalikuwa zamani ila sio leo. badilikeni.

4. Majibu ya ovyo.
Hii ni kweli, na chanzo ni wauguzi wenyewe, hasa hawa mama zetu na dada zetu.
Tatizo ni maadili kutokuzingatiwa sana huko shuleni.
Zamani watu walikiwa wanapita tuu na kozi za muda mfupi anakuwa muuguzi tayari. Hii imechangia sana kuleta wapuuzi kwenye hiyo
kada.

5. Duniani kote muuguzi anafanya kazi kwa kuzingatia order ya daktari.(except kwa wale ambao nicertified practitioner huko majuu)

Hiyo ndiyo kazi kuu Ya muuguzi,

Hospitali kumegawanywa majukumu
kuna anae diagnose na kupriscribe
Mwingine ana dispense
Mwingine ana administer
Mwingine ana investigate.
na wote hao wanafanya kazi kwa kushirikiana kwa pamoja.

Katika emergency wauguzi wamekuwa wakifanya maamuzi mbalimbali.
mfano mgonjwa yuko kwenye cardiac arrest huwezi kusema unasubiri daktari akuambia ndio muanze CPR.

muhimu muuguzi hakikisha umeiva kwenye kila kitu kinachokuhusu hakuna atakae kusumbua wala kukudharau.

6. Kwanza kijana inabidi uelewe Tanna na TNMC ni nini.
Tanna ni chama cha wauguzi.
hii ndio inatakiwa kuwa sauti ya wauguzi.

TNMC ni baraza la wauguzi na wakunga wauuguzi.

Kitu kimoja elewa TNMC ipo kwa ajili ya KUILINDA JAMII DHIDI YA HUDUMA ZITOLEWAZO NA WAUGUZI NA WAKUNGA.
Tnmc haiko kwa ajili ya kumtetea muuguzi.
TNMC ni mkono wa serikali.
Ndio maana wajumbe wote wanateuliwa na waziri wa afya.



Mwisho, Uuguzi ni Kada nzuri na muhimu kwenye uhai wa sekta ya afya.
 
Habari.

Mimi ni kijana wa kiume niliyebahatika kusoma uuguzi nchini Tanzania.

Nipende kuwapongeza wote waliobahatika kusoma uuguzi Tanzania maana moja ya kada inayoiendesha hospitali kwa asilimia kubwa sana na wanasaidia wagonjwa maana ndio wanaoshinda nao masaa 24.

Niseme ukweli mimi nitakuwa wa kwanza kuuacha uuguzi pindi nitakapoenda kujiendeleza elimu ya juu.

Nilisoma nikiwa na mapenzi ya dhati sana na moyo wangu ukiipenda hii kazi lakini niliyokutana nayo kazini ni Tofauti na hayo ndio yananifanya nikiri nitaiacha hii fani mapema sana.

1.Uuguzi Tanzania ni miongoni mwa kada za afya zinazodharaulika kupita kiasi na inaonekana kada ha watu wasio na akili hali ambayo ni tofauti kwa nchi za ulaya na uarabuni .

2.Upande wa maslahi uuguzi haiwezekani muuguzi wa degree Mwenye kusoma miaka minne sawa na mfamasia ,fizio yeye akalipwa TGHs C (around million 1 basics) wakati wenzake wakaanza na TGHs D(around million 1.3basics) na mpaka sasa inaonekana kawaida.

3.Upande wa Hopitali muuguzi anaongozea kudharauliwa sana na watu wa kada nyingine Hasa medical doctor kwa kumchukulia muuguzi kama mtu aliye muoa(mke wake)kiasi kwamba hospital nyingine hasa za mission wauguzi wamekuwa wakiwekeana zamu ya kuwapikia na kuwaandalia madaktari chakula.

4.Jamii inamuona muuguzi katili na mtu Mwenye majibu ya ovyo hali ambayo ni tofauti kwa wauguzi wa hivi karibuni wanaojaribu kupambana kwa hali na mali kubadilisha Hadhi ya uuguzi lakini bado hali inaonekana muuguzi ni katili ndo maana kila lawama za hospitali ni MUUGUZI.

5.Muuguzi Hajapewa nafasi ya maamuzi ya matibabu kwa mgonjwa hata kwenye emergency kiasi kwamba kutoa panadol tu mpaka amsubiri daktari hali ambayo ni tofauti kwa nchi za wenzetu hasa ulaya na muuguzi hajawekwa sehemu ya uongozi wala maamuzi ya hospital ilhali muuguzi wa degree Anasoma vitu vingi vinavyohusu mgonjwa na uongozi pia.

6.Chama cha Wauguzi TANNA na TNMC haviko katika minajili ya kumsaidia muuguzi zaidi ya kumkandamiza na kumnyanyasa ndo maana kila siku kazi yao kuongelea maadili lakini wanamwacha muuguzi huyu kwenye mazingira magumu kumsaidia kwenye masuala ya maslahi ,hela ya overtime ,na haki zake binafsi.

Wauguzi wa nchi za wenzetu kama Nchi za ulaya wameufanya ionekane kada bora na yenye malipo mazuri na zaidi kuwafanya wafanye kazi kwa ufanisi na kuspelize kabisa kama muuguzi wa watoto,usingizi,magonjwa tofauti na nchi ya Tanzania muuguzi amekuwa ni kilaka wa kufanya kazi popote pale .


Muuguzi wa ulaya analipwa hela nzuri kwa lisaa wengine hasa wa ICU wamezidi mishahara hata baadhi ya madaktari.


Kiukweli mambo ni mengi ila kama kada ya uuguzi Tanzania haitabadilika tutarajie kupunguza idadi kubwa ya vijana kusoma uuguzi hasa wanaume.


Wa kwanza nitakuwa Mimi.
Aiseee kama unaelimu nzuri jaribu nje ya nchi hasa UK, Canada nk wanahitaji Sana hii taaluma acha na hizi kazi za kiccm
 
Back
Top Bottom