Uvaaji wa magauni mafupi, vimini, kikaptula

Uvaaji wa magauni mafupi, vimini, kikaptula

e83c7b9a39fbce7b345c2e40ac7d50d5.jpg
 
Mko poa walimbwende,

Ngoja niwape darasa kidogo, kimsingi uvaaji wa nguo fupi kwa wanawake pia ni fasheni ya mjini nazungumzia gauni fupi,kimini au kikaptula(kichupi) ila nazungumzia zaidi vimini na magauni mafupi.

1/Mazingira yanaruhusu?
Kabla hujavaa kimini au gauni fupi jiulize kwanza unaenda ofisini,sehemu ya ibada,starehe au kitaani tu au utapanda daladala? Ukijiridhisha wewe jipigie tu kimini chako.

2/Una miguu?
Kuvaa tu kinguo kifupi wakati una miguu mibaya ni sawa na kujidhalilisha tu kama unajijua unatembelea mikono usivae vazi hili.

3/Kiatu kirefu ndio mwake
Ili utoke bomba na gauni fupi au kimini hakikisha unavaa kiatu kirefu, lakini kimini pia kinaweza kuvaliwa na flat shoes kikaeleweka utaonekana wa kijanja.

4/Epuka kuinamainama
Ukivaa vazi fupi kamwe usitake kuinama unaweza kujikuta mali zako zinabaki nje.Njia bora wakati unaokota/kuchukua kitu ni kuchuchumaa tu.

5/Kaa kwa staha
Wakati wa kukaa hakikisha unapishanisha miguu badala ya kuachanisha au kuitanua, utakaa uchi.

6/Uvaaji wa kaptula fupi/kichupi
* Huvaliwa chumbani au sehemu ya starehe
* Inapendeza ukivalia top au blauzi
* Hakikisha miguu yako ipo soft
5e38f63d40c1dca971cfa93bfa274361.jpg
1cdcd1c7b59ebeaac3542a1e8470025c.jpg


Mwanamitindo wa Uswazi
The Bitoz
Imeniacha hoi...
 
Back
Top Bottom