Uvaaji wa mavazi haya ni ulimbukeni wa kiwango cha juu sana

Uvaaji wa mavazi haya ni ulimbukeni wa kiwango cha juu sana

Son of Gamba

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2012
Posts
4,720
Reaction score
6,957
Aina hii ya mavazi huvaliwa Ulaya na Amerika ya kaskazini kipindi hichi cha mwaka kwa sababu ya baridi kali na barafu inayodondoka huko. Kichekesho ni pale unapomwona mtu mzima na akili zake amevaa mavazi haya hapa Dar huku joto likiwa kali kiasi kwamba wewe uliyevaa T-shirt tu unatamani kuivua utembee kifua wazi.

Huu ni ulimbukeni wa kiwango cha kupitiliza, hata Wazungu waliobuni aina hii ya mavazi wakiona mtu amevaa mavazi haya huku kwetu na joto lote hili la Dar huwa wanacheka sana, wanatudharau sana na kutuona bado sana sisi ni watumwa wa fikra.


pagani 4.jpg
pagani3.jpg
pagani2.JPG


Kuna watu watatetea ulimbukeni huu kwa kisingizio cha sikukuu ya X-mass ambayo nayo ni upagani tu wala haina maana yoyote katika dini ya KWELI ya KIKRISTO. Na wengine watasema ni namna ya kuvutia biashara; lakini bado haileti maana hata kidogo. Nasema haileti maana sababu hakuna uhalisia wowote ule wa kuvaa nguo kama hizi sana sana anayevaa anageuka kuwa kituko kwa wale wanaoelewa maana ya mavazi haya.

Kwa akili hizi sisi Waafrika tutabakia kuwa watumwa wa Wazungu mpaka siku ile BWANA YESU atakaporudi tena kwa mara ya pili. Kwa akili hizi ndio maana Wazungu wanatuibia madini yetu mpaka na mchanga pia wanachukua na kusafirisha kwenda kwao tena tukiwasindikiza sisi wenyewe mpaka uwanja wa ndege na bandarini huku tukiwalinda na silaha nzito, na wao kutuachia mahandaki matupu.

Ningekuwa mimi ni Rais wa nchi hii ningepiga marufuku kabisa aina hii ya ulimbukeni kama alivyofanya Rais wa Korea ya Kaskazini Kim Jong-un; amesema hataki kabisa kuona raia wake wanasheherekea X-mass ama wanajihusisha na tamaduni zozote zinazoambatana na sherehe hizi za kipagani zilizoanzishwa na Wazungu wa Rumi.
 
Kuna ulimbukeni kama kuiga dini za wenzetu? Mbona unatambua uwepo wa Kristu. Je uislam ulitoka Africa na hao wanaovaa vibandiko na kuficha nyuso unawasemaje? At least hii ni shughuli ya muda wa mwezi mmoja basi je, wanaovaa maisha yao na ulimbukeni mbona hutaji?
Kama wewe ni mwafrika wa kweli basi abudu kwenye dini za babu zako siyo hizi za kuletewa. Ukishaabudu kwenye dini za kuja, kubali kila kitu.

Usitudanganye, sasa hivi Australia na New Zealand ni joto, je hawatavaa hayo mavazi? Oh hata wazungu wanatucheka. Unajicheka mwenyewe labda.
 
Kwani Jumamosi ndio siku ya saba au siku ya sita? Haha mi napita tu
 
Povu povu povuuuu
Mtoa mada Leo umewaka kweli kweli kila mtu na maisha yake kifupi hata wewe ni mtumwa vile vile tukiachana na hayo mavazi kuna vitu vingine tayari vimekuathiri kisaikolojia ambavyo vimeanzishwa na mzungu halafu wewe ukavifanya..... Usikariri mavazi tu kuna vitu vingi bado wewe utabaki kuwa mtumwa. [emoji23] [emoji1]
 
Kuna ulimbukeni kama kuiga dini za wenzetu? Mbona unatambua uwepo wa Kristu. Je uislam ulitoka Africa na hao wanaovaa vibandiko na kuficha nyuso unawasemaje? At least hii ni shughuli ya muda wa mwezi mmoja basi je, wanaovaa maisha yao na ulimbukeni mbona hutaji?
Kama wewe ni mwafrika wa kweli basi abudu kwenye dini za babu zako siyo hizi za kuletewa. Ukishaabudu kwenye dini za kuja, kubali kila kitu.

Usitudanganye, sasa hivi Australia na New Zealand ni joto, je hawatavaa hayo mavazi? Oh hata wazungu wanatucheka. Unajicheka mwenyewe labda.
Tena Australia kwa mwezi huu Dec kuna joto la level nyingine kabisa....anasemaje kuhusu wakina Mama wanaovaa zile nguo nyeusi tiii zikiwafunika hadi kope za macho na wanapita Kariakoo na jua kali la nyuzi joto 40?
Anasemaje kuhusu uvaaji wa suti nzito wakati Dar kuna joto kali kabisa?
Ndugu .....hizi ni tamaduni za watu tu...tume kopi na tukubaliane kutokubaliana....kila mtu ana imani yake.Shika yako,waachie yao.
 
Back
Top Bottom