UVCCM Songwe yatia neno mikopo ya Vijana kusitishwa

UVCCM Songwe yatia neno mikopo ya Vijana kusitishwa

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
Mwenyekiti wa Umoja wa vijana wa CCM (UVCCM) Mkoa wa Songwe Ndg Fatuma Hussein amewatoa hofu vijana kutokana na serikali kusitisha utoaji wa mikopo ya 10% iliyokuwa ikitolewa katika ngazi za Halmashauri.

Fatuma ameleza kuwa kama UVCCM wanaamini kuwa serikali itakuja na mpango bora zaidi wa utoaji wa mikopo hivyo hivyo kuvitaka vikundi ambavyo vilikwisha undwa kuendelea kujiandaa na pindi dirisha la mikopo litakapozinduliwa wawe wa kwanza kunufaika na fedha hizo.

Aidha katika hatua nyingine Fatuma ameiomba serikali kuharikisha ujenzi wa soko la Tunduma ambalo lipo katika hatua za mwisho kwani wananchi wengi wanasubiri kwa hamu soko hilo, kwani litakuwa ndio mkombozi wa vijana wengi kujiajiri

Mwenyekiti Fatuma ameyasema hayo katika Ziara ya kamati ya utekelezaji ya UVCCM Mkoa wa Songwe ambapo Leo tarehe 18 Aprili wapo wilayani Momba.
 

Attachments

  • VID-20230418-WA0016.mp4
    13.2 MB
  • IMG-20230418-WA0015.jpg
    IMG-20230418-WA0015.jpg
    153.8 KB · Views: 5
  • IMG-20230418-WA0012.jpg
    IMG-20230418-WA0012.jpg
    117 KB · Views: 5
  • IMG-20230418-WA0013.jpg
    IMG-20230418-WA0013.jpg
    110 KB · Views: 5
  • IMG-20230418-WA0014.jpg
    IMG-20230418-WA0014.jpg
    153.4 KB · Views: 5
  • IMG-20230418-WA0011.jpg
    IMG-20230418-WA0011.jpg
    125.7 KB · Views: 4
Hawa ndiyo matapeli na mafisadi wetu wajao toka lumumba
 
Dunia ina mambo. Kwani hafahamu ya kuwa kupata mikopo ya vijana na wanawake bila connection ni ngumu kwa mkoa wake. Unless kuwe na mkono wa Mungu.
 
Back
Top Bottom