UVCCM wamuonya Anthony Diallo

UVCCM wamuonya Anthony Diallo

Katibu wa umoja wa vijana wa ccm Khenan Kihongosi amemuonya mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza bwana Diallo kuwa aache upotoshaji mara moja, kitendo cha kusema baadhi ya viongozi waliopita walitakiwa kuwa mirembe ni cha kipotoshaji kwani Diallo yupo kwenye vikao vyote vya maamuzi kwani ni mjumbe wa kamati kuu.

Mwenyekiti wa CCM mkoa huwa halipwi mshahara na chama,Sasa unamuonya mtu ambaye humlipi Wala halipwi? CCM ni aibu kutokumlipa mshahara mwenyekiti wa CCM mkoa . Fikirieni hii hoja.
 
Katibu wa umoja wa vijana wa ccm Khenan Kihongosi amemuonya mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza bwana Diallo kuwa aache upotoshaji mara moja, kitendo cha kusema baadhi ya viongozi waliopita walitakiwa kuwa mirembe ni cha kipotoshaji kwani Diallo yupo kwenye vikao vyote vya maamuzi kwani ni mjumbe wa kamati kuu.

Sasa uyu nae anashindana na senior wake kwenye chama, hivi ndani ya ccm vijana hua hawafundishwi adabu, ?

Uvccm eleweni hamkijui chama chenu, KUANZIA hx na nakadhalika

That,s ndani ya chama chenu mpo makundi manne

1.ccm kindakindaki
2. Ccm limbukeni
3. Ccm Maslahi
4. Ccm halisi
 
Wengi walipigia kelele kuhusu utawala wa awamu ya 5 kuendesha nchi kiimla bila kufuata sheria na katiba huku wana CCM Mpya wa mtaa wa Lumumba wakiimba mapambio na kusifu uovu huo.

Sasa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa naye kaamua kuvunja ukimya na kusema ukweli

 
Katibu UVCCM ni Mwajiriwa.anateuliwa
M/Kiti. Mkoa anachaguliwa
Wote ni wajumbe wa vikao kitaifa
Kiprotocal UVCCM wanaweza kumuonya Mkiti wa Mkoa?
 
Ifike mahali tuheshimu mawazo au maono ya mtu hoja hupingwa kwa hoja Kama kasema kweli itabaki kua kweli lakini Kama kapotosha pinga kwa hoja iliyonyooka unaposema viongozi waliopita inaonesha unamtaja unayemjua ni yupi
Katibu wa umoja wa vijana wa ccm Khenan Kihongosi amemuonya mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza bwana Diallo kuwa aache upotoshaji mara moja, kitendo cha kusema baadhi ya viongozi waliopita walitakiwa kuwa mirembe ni cha kipotoshaji kwani Diallo yupo kwenye vikao vyote vya maamuzi kwani ni mjumbe wa kamati kuu.

 
10 Julai 2021
Tunduma, Songwe
Tanzania

UVCCM waongea kwa uchungu mkubwa kufuatia kauli ya Mwenyekiti wa CCM wa mkoa



UVCCM watoa kauli ya kulaani vikali kauli hiyo ya Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza.

UVCCM yamuomba Katibu Mkuu wa CCM kuongea na Mwenyekiti huyo wa CCM mkoa wa Mwanza Dr. Anthony Diallo.

. Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Ndugu Kenani Laban Kihongosi amesema umoja huo unaikemea na kuilaani vikali kauli Iliyotolewa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii akisema kuwa kipindi cha nyuma kuna viongozi walichaguliwa kuongoza wakati wana rekodi ya kuwa vichaa na walitakiwa kuwa 'Milembe' badala yake wakapewa kuongoza nchi.

Ndugu Kihongosi amesema kuwa UVCCM imesikitishwa na kauli hiyo ya uongo ambayo pia si ya kiungwana inayolenga kutweza na kudhalilisha viongozi waliowahi kuongoza nchi sambamba na kukosa maadili ya uongozi kwa mujibu wa taratibu za chama.

"Tumesikia maneno ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza tunaamini chama chetu, kiko makini katika kusimamia maadili ya viongozi wake, UVCCM tunaamini Chama kitatafakari na kuona namna nzuri ya kushuhulikia jambo hilo kwa mujibu wa kanuni za uongozi na maadili." Alisema Kenani Kihongosi

Amefahamisha UVCCM inaamini kuwa viongozi wa chama wanatakiwa waongozwe na busara na hekima pindi wanapozungumza kuliko kuongea mambo ambayo yanaleta ukakasi na kudhalilisha Chama na Serikali jambo ambalo linakwenda kinyume na maelekezo ya kanuni za maadili na uongozi.

"UVCCM tunaikemea na kuilaani vikali kauli hiyo, Viongozi wetu waliopita waachwe wapumzike na waheshimiwe baada ya kutekeleza majukumu yao, yeye kama aliona hivyo alibakia kwenye chama kufanya nini? Akitokea kiongozi wa namna hii anakiuka maadili ya chama chetu sisi UVCCM tutanyoosha mstari kulinda kanuni na maadili ya chama chetu," Alisisitiza Kihongosi.
 
Huyu akumtaja mtu ,Uvccm hao wamenyanua mdomo , nchi hii haiwezi endeshwa KWA sifa ,cheo , au u mwanachama wa ccm kisha mko madarakani ,Kama vile Mungu akatenda nchi KWA SSH, RAIS, na Mwanamama bado laja lingine ambapo hatutategemea, ASEMA BWANA ,tujifunze elewa madaraka ni mpito tu na hatuwezi pata wote,

Ila mliobahatika jua wapo binadam wenzenu wapo nyuma na na wanatekeleza shughuli zote kadri mungu alivyowaumba Kama binadam tofauti ni kipato , na maisha tuishio
UVCCM waongea kwa uchungu mkubwa kufuatia kauli ya Mwenyekiti wa CCM wa mkoa

 
Katibu wa umoja wa vijana wa ccm Khenan Kihongosi amemuonya mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza bwana Diallo kuwa aache upotoshaji mara moja, kitendo cha kusema baadhi ya viongozi waliopita walitakiwa kuwa mirembe ni cha kipotoshaji kwani Diallo yupo kwenye vikao vyote vya maamuzi kwani ni mjumbe wa kamati kuu.

Sio walipaswa kuwa milembe
Bali kumbukumbu zao ziko huko 🤣🤣🤣🤣
 
Wakakimbia alafu kiwanda bora kabisa Afrika cha kufua zahabu kikajengwa, nchi ikaingia uchumi wa kati , mabilionea kama akina Laizer wakaibuka, mapato ya ccm yakatoka million 5 yakafikia billioni 20 kwa mwaka!

Tunamuonya Diallo yeye amekuwa mbunge na waziri kwa miaka 20 lakini hakuna wananchi wanachomkumbuka nacho ni kama tu hajawahi kuwa kiongozi
 
Katibu wa umoja wa vijana wa CCM Khenan Kihongosi amemuonya mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mwanza bwana Diallo kuwa aache upotoshaji mara moja, kitendo cha kusema baadhi ya viongozi waliopita walitakiwa kuwa mirembe ni cha kipotoshaji kwani Diallo yupo kwenye vikao vyote vya maamuzi kwani ni mjumbe wa kamati kuu.
===

CCM imelaani kauli ya kubeza viongozi wastaafu iliyotolewa na mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Mwanza, Antony Diallo katika mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha televisheni nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumamosi Julai 10, 2021 na katibu mkuu wa umoja wa vijana wa chama hicho (UVCCM), Kenani Kihongosi katika kikao cha majumuisho ya ziara ya kuimarisha chama inayofanywa na sekretarieti ya chama hicho ikiongozwa na katibu mkuu wa CCM, Daniel Chongolo.

Kihongosi amesema kauli iliyotolewa na kiongozi huyo ni msimamo wake mwenyewe na si wa CCM na kwamba jumuiya ya vijana inalaani kauli zinazotolewa na kiongozi huyo kuwabeza viongozi walioitumikia nchi, akitaka wastaafu hao kuachwa wapumzike.

"Tangu leo asubuhi tumeona ujumbe ukisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikinukuu kauli iliyotolewa na mmoja na kiongozi ambaye anaingia kwenye vikao vya maamuzi lakini leo ameamua kutoa kauli hii ambayo imetuchukiza sana vijana kwani tulitegemea wawe wa kwanza kutuongoza, " amesema.

Kihongozi amesema kiongozi huyo wa CCM ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amenukuliwa akisema viongozi wengine wanaoteuliwa na CCM wanapaswa kuwa hospitali ya magonjwa ya akili ya Mirembe iliyopo mkoani Dodoma.

MWANANCHI
Sindano imegusa mfupa!

Mtasema yote mwaka huu! Kumbe Magufuli alikuwa na file Mirembe!🤣🤣🤣
 
Diallo ni mfukuza upepo ambaye maslahi yake yaliguswa na JPM....sasa anataka huruma dunia imsikie kama naye yupo..Hapa ndio namuumgaga mkono JPM kwa kunyooosha hizi pumbavu...
 
Huyu Katibu Mkuu aliwatandika bakora wafanyabiashara Arusha.

Huo ulikuwa msimamo wa chama !.

Huyu Katibu Mkuu alihimiza adhabu ya kifo kwa Mh Zitto Kabwe huo ulikuwa msimamo wa chama.
 
Back
Top Bottom