Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Halmashauri ya wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma imechukua hatua ya kumpumzisha daktari wa zamu ili kupisha uchunguzi baada video ya Mwanamke anaedaiwa kujifungua na kukosa huduma kwa zaidi ya saa moja katika Kituo cha Afya Kata ya Basanza kusambaa mtandaoni.
Halmashauri baada ya kufatilia ilibaini mteja huyo alifika zahanati ya Basanza Juni 09, 2024 akitokea maabara binafsi kwaajili ya kupata huduma zaidi lakini kabla ya kupatiwa huduma alijifungua.
Muhudumu wa zamu anayeishi umbali wa mita 5 kutoka kituo hicho baada ya kupata taarifa alifika wodini na kukuta mjamzito ameshajifungua mtoto wa kiume
Halmashauri ilimpumzisha kuendelea na majukumu yake kuanzia Juni 14 kupisha uchunguzi na endapo atabainika kuwa na makosa atachukuliwa hatua za kinidhamu.
Pamoja na hayo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Fred Milanzi ametoa wito kwa umma kuwasilisha malalamiko kupitia mfumo uliowekwa ili zifanyiwe kazi na amesikitishwa na mwananchi aliyeingia wodi ya wazazi bila ridhaa na kuchukua video ya tukio hilo na kusambaza mitandao ya kijamii na kuleta taharuki kwa jamii.
Pia SOMA=> Kigoma: Mwanamke adaiwa kujifungua na kukosa huduma kwa zaidi ya saa moja katika Kituo cha Afya Kata ya Basanza
Halmashauri baada ya kufatilia ilibaini mteja huyo alifika zahanati ya Basanza Juni 09, 2024 akitokea maabara binafsi kwaajili ya kupata huduma zaidi lakini kabla ya kupatiwa huduma alijifungua.
Muhudumu wa zamu anayeishi umbali wa mita 5 kutoka kituo hicho baada ya kupata taarifa alifika wodini na kukuta mjamzito ameshajifungua mtoto wa kiume
Halmashauri ilimpumzisha kuendelea na majukumu yake kuanzia Juni 14 kupisha uchunguzi na endapo atabainika kuwa na makosa atachukuliwa hatua za kinidhamu.
Pamoja na hayo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri, Fred Milanzi ametoa wito kwa umma kuwasilisha malalamiko kupitia mfumo uliowekwa ili zifanyiwe kazi na amesikitishwa na mwananchi aliyeingia wodi ya wazazi bila ridhaa na kuchukua video ya tukio hilo na kusambaza mitandao ya kijamii na kuleta taharuki kwa jamii.
Pia SOMA=> Kigoma: Mwanamke adaiwa kujifungua na kukosa huduma kwa zaidi ya saa moja katika Kituo cha Afya Kata ya Basanza