Uvumbuzi wa kurunzi iletayo giza

Uvumbuzi wa kurunzi iletayo giza

Mbege umelewa?! Point yako ni kuwasema maboss wa TANESCO, Kila mtu anakerwa na kukatika umeme.Mimi sio mfanyakazi wa TANESCO, nafikiri katika hali tulivu.Ninavyoifahamu jiografia ya Tanzania kusema ukweli tunawalaumu bure watu hawa! HEPs zetu ni ndogo, miundo mbinu ni chakavu, usambazaji wa Kila siku kwa wateja wapya, kubadilisha nguzo, nguzo kuanguka, maji kupungua, transformer kuungua kwa sababu tumeiba mafuta(coolant) na mengine mengi.Umeme sio nyumba ya miti ambayo mtu anaweza kuendelea na ujenzi wakati anaishi ndani! Inapotokea hitilafu,matengenezo, kusambaza ni lazima umeme ukatwe.Let's be considerate and stop blaming the guys who are actually overworked!
Acha siasa, hayo unayoyaongea yalikuwepo kitambo tu na Hali haikuwa hivi. Emu kuwa na aibu kidogo aisee.
 
The Theory of Mbenge Effect - Part 3

Ukikusudia kufanya uvumbuzi wowote ule kuna vitu viwili muhimu sana vya kuzingatia. Ama itakupasa utembee ndani ya kanuni za awali zinazotawala, ama la, uje na kanuni nyingine mpya kabisa ambayo itapaswa kuthibitishwa kisayansi.

Tunatambua mwanga wa jua ama nuru ya jua ni mionzi iliyopo katika umbo la nuru inayoonekana kwa macho ya binadamu. Kisayansi mionzi hiyo ni sehemu za mnururisho wa nguvu ya sumaku-umeme unaotoka kwenye jua.

Kivuli kinaweza kupatikana kupitia kifaa kipya ambacho kitatumika kugeuza nishati ya mwanga huu wa jua na kuweza kuibadilisha kwenda katika nishati nyingine mpya ambayo itatengeneza kivuli papo hapo.

Kivuli ni eneo lenye nuru kidogo katika mazingira yenye nuru zaidi, na hupatikana kupitia kizuizi kinachoangazwa upande moja na kuizuia nuru kuendelea na hivyo kuunda eneo lenye giza au nuru kidogo nyuma yake.
Kila kitu kisichopitisha nuru ndani yake kinaweza kuwa na kivuli kikianganzwa upande mmoja.

Mpaka sasa sayansi inakosa majibu katika kizuizi ambacho hakina kivuli kama vile hewa au vioo vya dirishani. Nipende tu kukumbushia ya kwamba ni lazima kanuni mpya yenye
vichochezi hasi vya "mbe" [emoji822] na "nge' [emoji747] vitanya kazi ya kuigeuza nishati yà mionzi ya jua na ku "generate
"mbenge effect" kwa hesabu ifuatayo ya

1/[emoji822]+2/[emoji747]+3/[emoji822][emoji747]

Hii ni kwa kuwa mionzi hiyo ya jua ni sehemu za mnururisho wa nguvu ya sumaku-umeme unaotoka kwenye jua.

Sehemu ijayo nitadadavua kwa undani kidogo kuhusu hivi vichocheo hasi. Stay tuned.
 
Kuna mawazo mengi ya kitechonolojia sema hayana back up za formula. Kwani unafikiri kabla ya gravitational forces kuwa documented hiyo force haikuwep? Ilikuwepo sema hakukuwa na chapisho a maelezo ya kisayansi. Kwa mfano, unafikiri wazungu hawaamini uchawi? Sema uchawi unakosa document na formula ili kufanyika popote na yeyote.

Wazo ni zuri. Kuna kipindi fulani miaka fulani wakati nasoma kuna document nilikuwa nazitaka kuzikopi moja kwa moja kutoka ktk image yaani nizipige picha kwa simu nikahamishie ktk assignment niliona ile kuandika kwa peni then nika type ni shida sana.

Huwezi amini hiyo technologia ya kubadilisha image ya maandishi kuwa MS word imeshaanza tumika. Mpka najiuliza Ina maana sikuweitafuta ilikuwepo au ni mpya maana nimeliona miaka ya hivi karibuni.
uchawi unafanyika popote na yoyote, kwanza inatakiwa ujue tofati ya uchawi, mchawi na mshirikina.
uchawi upo na kuna chawi za aina nyingi sana na mtu anaejua uchawi husika ndo anaitwa mchawi,
kwa sababu uchawi unafanya na mtu yoyote hata ambaye sio mchawi ndio maana kuna washirikina,

mshorikina ni mtu ambaye hajui uchawi ila anayanya uchawi kwa kupewa maelekezo mfano wanaoenda kwa waganga ambao sio matapeli, waganga hao ni machawi yaliyo kubuhu yanatibu kichawi ila ndo hayataki dhambi utaelekezwa kufanya uchawi utakao kusaidia kutatua shida yako na kama kweye huo uchawi kuna hatia inafanyika bas mganga yeye hana hatia maana hakufanya yeye huo uchawi. Hii ndo maana waganga hawataki hela za kichawi.


Mwenyewe nilikuwa siamini hizo mambo za kichawi, ila kilichofanya niamini kuna mshikaji wangu alisharogwa sana na ndugu zake sasa kwa sababu alisha pata tiba nyingi za kichawi kwa waganga mbalimbali kama kawaida waganga wanamuelekeza kufanya hizo tiba za kichawi jamaa ana note amejikuta anajua chawi mbalimbali kiasi kwamba akirogwa kwa style ileile hata haendi kwa mganga, anafanya tu uchawi aliowahi kuelekezwa na mganga pekeyake inakuwa problem solved.

Jamaa sasa na yeye amesha kuwa mchawi maana uchawi unaotumia kutibu kinyume chake unaweza kuutumia kuua, jamaa amesoma yuko very bright ndo maama anarogwa sana na ndugu zake bas kupitia dawa anazopewa na waganga mbalimbali anapewa maelekezo kufanya hizo tiba za kichawi na yeye anajifunza vitu ambavyo haambiwi anajikuta anajua hata kuua kupitia hizo tiba anazoelekezwa, ni kama dokta anakupa dose inayo kutibu ila akikuover dose kama dawa ni kali unakufa.

Mwisho: uchawi ni kama formula unafanywa na mtu yoyote, anayeujua(mchawi) au asiyeujua(mshirikina) yeye anafanya uchawi kwa kupewa maelekezo fanya hivi vile ila ila wote mchawi na mshirikina wakifanya uchawi reaction yake ni ileile.
 
Haya majina yaliyokuwa "anonymous" ambayo wengi wetu tunayoyatumia humu jukwaani tumejipa sisi wenyewe, na tena kwa hiyari yetu sisi wenyewe, isipokuwa kwa wachache tu ambao hawakuona haja ya kuficha "identity" zao. "But all in all" kanuni za jukwaa zinampa mtu uhuru wa kuchagua.

Ila haya majina ya kificho ni vyema watu wangalifikiria mara mbili mbili kuyachagua kabla hawajaanza kuyatumia na kuyahalalisha yawe juu ya nafsi zao. Kwa wale wanaotumia "acronym" kama mimi ya MBENGE , labda kwa ajili ya ufahamu "personally I can a bit unlock the codes". Mimi nilichagua jina hili lenye herufi 6, kwa mantiki ya kuwa ni namba yenye maana ya kimaandiko kuwa ya kibinadamu, kwa hiyo yote ninayofanya yapo katika nafsi hai ya kibinadamu.

Vifupisho vingine vya jina hili uwakilisha kwanza imani juu ya ukuu wa Mungu wangu, na sehemu anayoishi, yaani M ni MUNGU na tena MB ni MBINGUNI, E ni elimu ambayo imenipa uwezo wa kujitambua na pia nawajibika kwa kila nilitendalo, na yalitobakia ni vifupisho vya majina kwa ajili ya heshima ya wazazi wangu NGE, Sasa sijui wenzangu mlitumia "criteria" zipi kujipa majina yenu.

Hii hoja ni nje ya mada, na wala haiusiani kabisa na "the theory of mbege effect" lakini imekuja tu "by the way" kutokana na baadhi ya wachangiaji katika mada yangu. Ila pia ni vyema tukayatafakari kwa pamoja maneno yafuatayo ambayo nimeyanukuu kutoka katika maandiko matakatifu, ili tutafakari zaidi juu ya haya majina yetu.

1 SAMWELI 25:25

"Nakusihi, ee bwana wangu, wewe usimuangalie huyu mtu asiyefaa, yaani, Nabali ; Kwa maana KAMA LILIVYO JINA LAKE NDIVYO ALIVYO YEYE; jina lake ndilo Nabali, na upumbavu anao, lakini mimi mjakazi wako, sikuwaona hao vijana wa bwana wangu uliowatuma".

MITHALI 22:-1:-"

"HERI KUCHAGUA JINA JEMA kuliko Mali nyingi ; Na neema kuliko fedha na dhahabu"
 
Hiyo mbenge effect huku uziguani inaitwa DIUKIZULA ifekti na praktikale huku ni miaka mingi inafanyika uje huku Mazingala au hata Mzundu upigwe lecture and practical Kisha ukafanye rehearsal kwenu maana ukifanyia huku wataku sublimate
 
The Mbenge Effect Theory - Part 4

Siku zote ni vyema ieleweke kuwa ahadi huwa ni deni. Kwa hiyo ninawiwa kwa dhati kabisa kukitekeleza kile ambacho nilikiahidi kukifanya kwa 100%

Aidha nianze kwa kuipongeza Wizara ya Nishati sambamba na shirika letu la TANESCO kwa kuweza kuuwasha mtambo namba 9 katika Bwawa la Umeme la Julius Nyerere, hali iliyopelekea kupungua kwa kiasi kikubwa cha makali ya mgao wa umeme hapa nchini. Natambua kuwa nyie ni waungwana, na mlipokea kwa mikono miwili malalamiko, lawama na shutuma nyingi zilitolewa kwenu katika kipindi chote cha makali hato, nafikiri hiyo imekuwa ni kichocheo chanya kwenu kilichowafanya mpambane usiku na mchana ili kutafuta suluhu ya muda mfupi na hatimaye mje kupata ufumbuzi wa kudumu.

Turudi katika mada yetu, haijalishi kuhusu sayansi ya sasa kukosa majibu ili kuking'amua kizuizi kipya ambacho kitaleta kivuli mara moja katika hewa. Kanuni mpya inakuja na
vichochezi hasi vya "mbe" [emoji822] na "nge' [emoji747] ili vifanye kazi kisayansi na kuigeuza nishati yà mionzi ya jua na ku "generate
"mbenge effect" kwa hesabu ifuatayo ya

1/[emoji822]+2/[emoji747]+3/[emoji822][emoji747]

Hii ni kwa kuwa mionzi hiyo ya jua ni sehemu za mnururisho wa nguvu ya sumaku-umeme unaotoka kwenye jua, hivyo ni dhahiri kuwa itakutana na [emoji822] ili kuipelekea ishuke na kuwa nguvu yenye kiwango cha "zero" na' [emoji747] ambayo itaunda nishati mpya ya kutengeneza "giza" mara moja!

Sehemu ijayo nitadadavua kwa undani kidogo kuhusu ujio wa kichochezi hasi cha "mbe" [emoji822] "Just stay tuned"
 
The Mbenge Effect Theory - Part 5

Siku zote ukiwa upo ndani ya nadhiri ya jambo fulani, ni lazima uitekekeleze kwa kiwango sahihi kama vile ambavyo inapaswa kuwa. Kwa hiyo ninawiwa kwa dhati kabisa ya mtima wa moyo wangu kukitekeleza kile ambacho nilikiahidi kukifanya kwa 100%

Mpaka sasa ninaendelea kufanya utafiti wa kisayansi. Zoezi hili si rahisi kama vile pengine wengi wetu wangaliweza kufikiria. Imenibidi kuigawanya timu ya wataalamu wangu katika makundi manne, ambayo mengi kati ya hao yanashauri tuibadilishe kanuni ya msingi

Bado nakusanya "facts" ili nikubaliane nao na ili pia tuweze kwenda mbele vizuri zaidi, na pia kwa njia bora zaidi, ili kuweza ku "unlock the way foward with expectation of producing the positive results". Wadau naomba tuwe wastahimilivu katika kipindi hiki muhimu cha kutupeleka kwenye "bliss"

CIAO.
 
Bangi haijawahi acha mtu salama...
Kuna mmoja namfahamu iliwahi kumuacha salama, ila baada ya hapo akaenda akaingia kwenye pipa la mafuta yaliyokuwa yanachemka kwenye moto
 
Dunia ya sasa inaendeshwa kupitia kanuni za sayansi na teknolojia ambazo zilivumbuliwa na wanasayansi katika karne zilizopita. Kanuni hizi siamini kuwa zinazima ndoto ya uvumbuzi wa kanuni mpya ambazo zinaweza kuja na majibu katika maeneo mengine mapya ambayo uvumbuzi mpya bado haujafanyika mpaka hivi sasa.

Eneo mahususi ambalo mimi binafsi nataka kulifanyia kazi ni kupata sayansi ambayo itakuwa kinyume na hii ya sasa katika nishati ya mwendo wa mwanga pamoja na chanzo chake. Ni lazima nitoe pongezi zangu kwa TANESCO kupitia mgao wao usioisha wa umeme, jambo ambalo limemiwezesha kuja na wazo hili kuhusu uvumbuzi huu wa kisayansi ninaotegemea kwenda kuufanya.

Nikianza na nadharia ya kifaa hiki kipya, kitafanya kazi kinyume kabisa na vile ambavyo kurunzi za kawaida zinazotoa mwanga zinavyofanya kazi. Kwa kuanzia, mimi na timu yangu ya wataalamu tutaingia chaka ili kujifunza kuhusu nishati hasi ambapo endapo ikiachiwa itatengeneza nguvu hasi na kupelekea giza ama kivuli kutokea mara moja, kwa hiyo basi mwanga kutoweza kupita hali itakayopelekea giza kutokea na kutawala "automatically on the surface under influence"

Athari ya kanuni ya nishati hii hasi dhidi ya mwanga itaitwa "mbenge effect" na ili iweze kufanya kazi zake kwa ukamilifu uliokusudiwa itabidi itegemee "formular" ya kimahesabu na kiithibati ili kukidhi mfumo mpya wa kanuni ya vichochezi hasi yaani "mbe" ambacho kitawakilishwa na alama ya [emoji822] na "nge' ambacho alama yake itakuwa ni [emoji747]

Kwa hiyo ukitaka ku "generate
"mbenge effect" itabidi kanuni ifuatayo itumike

1/[emoji822]+2/[emoji747]+3/[emoji822][emoji747]

Kwa leo basi tuishie hapa, kwa kuwa sina "background" ya sayansi, ngoja kwanza nitafute jopo la baadhi ya wanasayansi ili niuze wazo hili kwao na tuanze kulifanyia kazi mara moja. Stay tune kwa mrejesho.
Bonge la idea.

Mwanasayansi wa kwanza hapa nnasubiri jopo likamilike tuanze kazi bwana Mbenge😆😆😆😆😆😆😆😂🤓
 
Bonge la idea.

Mwanasayansi wa kwanza hapa nnasubiri jopo likamilike tuanze kazi bwana Mbenge[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji851]
Thank you for your compliment chief.

Ni watu wachache sana ambao huwa tayari kupima mantiki iliyopo nyuma ya wazo jipya pale linapotolewa na pia hata kuweza kumtia mtu moyo.
 
Back
Top Bottom