uvumilivu...


....hahaha....nilijua tu. Kwani, uvumilivu sio sehemu ya mapenzi, mahaba na upendo mkuu?
 
Last edited by a moderator:
Eiyer lakini pia nilisema kama mtu huyo atajifunza kwa kosa hilo, kamwe hatorudia tena...................

 
nimemsoma Gfsonwin nampa hongera na pole pia uvumilivu unategemea na mambo unayoyavumilia nadhani kwa wale waliosoma uzi uliosema ANATAMANI AFANYE MAAMUZI MAGUMu,ni kuhusu rafiki yaangu ambaye ameolewa lakini mume wake hataki afanye kazi wala ajiendeleze kielimu hatuna mkataba na Mungu je huyo mwanaume asipokuwepo leo je na yeye pia aendelee kuvumilia hayo maisha ya kuwa mama wa nyumbani ilhal amesoma au akimbie aangalie future yake
 
eversilin gal huyu rafiki yako analichukuliaje ilo la kuambiwa asifanye kazi wala kujiendeleza kielimu? je anaona kama ni changamoto ama limemzalia chuki kwa mwenzi wake kiasi cha kutaka kuondoka? hapo ndipo penye ugomvi mkubwa sana na wanawake wengi kwani kila mapungufu ya mwanaume yanachukuliwa kama chuki jambo ambalo ni baya sana.

binafsi ningemshauri huyu dada alione kama ni changamoto na aanze kulifanyia kazi kwa kuproove kwa mumewe kwamba akifanya kazi basi maendeleo yataonekana nyumbani.Jamani mtanisamehe lakin huu ndio ukweli kuna baadhi ya wanawake tukifanya kazi hata senti haiji nyumbani na kila siku lazima hela atoe mr sasa je kwa stail hii si bora ubaki tu nyumbani akulishe ajue moja? manake hata kama utajiendeleza kielimu halafu iwe ni kwa faida yako binafsi what does it have to do with the reat of the family? bora usijiendeleze.

amwaminishe mumewe kwa kuwa muwajibikaji bora ndani ya nyumba yake, kipato akipata ashee na mumewe, aonekane kwake kuelimika ama kuwa na kipato siyo kujikweza na mambo kama hayo. anyway labda niambie vizuri kwenye pm nione kama naweza kumshauri kwa uzuri zaid.

kwa wanawake siyo kwamba nawachukia ila mtanisamehe sana mm mapungufu ya kike huwa nayapiga vita sana kwani naamini mwanamke hodari na jasiri huzima mapungufu ya mwanaume na ndivyo ilivyo.
 
Last edited by a moderator:
Mtambuzi,nilichokua namueleza gfsonwin ni mtazamo wangu na msimamo wangu katika hatari aliyoifanya chini ya mwamvuli wa uvumilivu.Nauthamini sana uvumilivu na kuna mambo ya kufanyia uvumilivu,lakini sio kama alilofanya yeye.Ni kweli mtu yoyote anaweza kuwa mtu mpya pale atakapoishi na mvumilivu,lakini hilo linategemea ni mambo gani anatendewa huyo anaevumilia,mengine unaweza kuwa unadhani unavumilia kumbe hujiamini,unahofia utaanzaje ukiwa mwenyewe,hata kama unafanyiwa mambo ya hatari!
 
Last edited by a moderator:
Aspirin ulichosema ni kweli kabisa. Kuna kipindi penzi linaisha tunalazimisha kwa kujiita wavumilivu.

Aingii akilini nyumba ndogo initukane saloon (kwanza ningeua aisee) na kuja kulala kitandani kwangu na kuvaa kitenge changu juu. Hapana.... Ndio kusamehe kupo (si saba mara sabini though) na kunategemea mazingira kama yata niconvince kuwa ni worth kusamehe...ila kuvumilia ni BIG NO

Maisha yenyewe mafupi; who is he kunifanya nilie mwaka, miwili, mitatu...? hata kama angekuwa ni the last man standing hapa duniani.


Nimewahi kusamehe lakini sijawahi kuwa mvumilivu. Na baba nanii anajua kuwa niko principled. Mfano siwezi kujua kuwa jamaa ana nyumba nyingine anaudumia afu mimi nikubali kukaa eti navumilia atajirudi. Ni kukosa kujiamini kuwa bila fulani maisha yamesimama.


 

Ni kweli dada yangu, na kila mtu naamini anatamani kuwa na uvumilivu, tatizo linakuja pale Mtu anapokosa uvumilivu wa kuvumilia. Mfano mzuri ni mimi mwenyewe, I real wish I could have uvumilivu, lakini tatizo ndio hapo ni vipi kuuvumilia uvumilivu.
 
Umeona Eiyer. Ukiwa na dada anayevumilia hivi ndio unasikia makaka wameenda kumtoa dada yao kwenye ndoa.. maana ni kama amekuwa brain washed. Haya mambo yalikuwa zamani na ni ilikuwa ukimuuliza mtu kwa nini uchapi lapa anakwambia ni sababu za kiuchumi... labda yatima hana pa kwenda hivyo kuondoka na kukaa ni sawa.

Ila kweli karne hii ya 21 kama bado kuna mwanamke mvumilivu tena aliye well informed, mwenye elimu na kazi yake... siwezi kuelewa hata atoe maelezo gani

Kuna vya kuvumilia kama mume katimuliwa kazi, kaugua... lakini na akili zake timamu anakueletea vimada ndani na vimada wanafikia kukukashfu BIG NO. Kwanza hata huyo mwanaume unaweza kuwa unampa wakati mgumu kwani anataka umpishe aanza maisha upya na ampendae. Ni ung'ang'anizi. Labda kama kweli kuna kurogana.


 
kaazi kweli kweli,i wish ningekuwa mvumilivu labda nisingekuwa na record breaking ya strings of relationships...lol:A S cry:,nakuwa na huyu asubuhi jioni nilishamuacha...lol
 
Eiyer nimekuelewa, lakini katika maoni yangu nilisema uvumilivu unalipa pale unapoambatana na imani isiyotetereka......... Kwa watu wenye imani isiyotikiswa na wala hawatetereki wanapopata changamoto mara nyingi hupata matokeo mazuri.
Kumbuka kwamba sisi kama wanaadamu huwa tunajaribiwa na kufikia mahali tukajiona tumenyang'anywa kila tunachokitegemea. tunafika mahali tukajiona tuko watupu kiasi kwamba tunaweza kujiuliza kwa nini iwe mimi........ hapo ndipo tunapokuwa na uchaguzi wa aidha kumtegemea Mungu au kutafuta suluhu kwenye ushirikina.......... mara nyingi ushawishi wa kukimbilia kwenye ushirikina huwa na nguvu sana, ambapo matokeo yake hayawi mazuri, lakini kama imani yako itasimama imara ukimtegemea Mungu, hakika atakulinda na kama ni kufa basi itakuwa ni kwa mapenzi yake maana hatukuumbwa ili tuishi milele........
Na ndio pale unaposhuhudia Mume anahangaika na vimada mpaka anapata Ukimwi lakini mke akabaki salama na kuwaacha watu midomo wazi..................
 
Last edited by a moderator:

ndugu yangu nyumba kubwa aisee wala huyu dada hajakosa kujiamini hata kidogo unless kama sijamuelewa vizuri. binafsi uvumilivu wa aina hii mimi sina lakin ukweli ni kwamba kama ni mcha Mungu basi ametuonyesha kuwa Mungu huwa anajibu maombi. Pia sisi wengine huwa tunaamini kila jambo jema hufanyika kwa mapenzi ya Mungu hivyo haukua mpangoo wa MUNGU kwa huyu dada gf kuondoka.

tutasema sana lakin Mungu akitaka ubaki nakuhakikishia utabaki na wala hili halitakkuwa na mpinzani. nampa tu pole kwa magumu haya kweli ana Mungu.
 
Last edited by a moderator:
nyumba kubwa kuvumilia kwangu hakukusababishwa na kutokuwa na kipato wala kazi wala mahali pa kwenda wala kutokujiamini ama woga. nilijiamini sana kuwa mimi ndiye mke sahihi no ways. tena bahati nzuri wazazi wangu wapo hai hadi leo and wako vizuri sana kiuchumi.labda nikwambie sababu na hizi kwenu ziwe za kijinga ama nini kwangu they remained to be critical reasons
-sikupenda kuwa na mahusiano zaid hata kama angetokea mwanaume gani
- sikupenda watoto wangu hasa ambaye alikuwa wa mume wangu ambaye nilimchukua kwa mama yake niliye mwaminisha anakuja kuish na baba yake halafu nije nimuharibu kisaikolojia kwa kumuishisha maisha ya kuish na mtu baki manake kumbuka baba yake ndiye aliye tuunganisha.
-mimi huwa siku zote sikubali kushindwa katika kila nilitakalo ambalo najua ni haki yangu, so imani yangu kwa Mungu ilinikataza na sikuona sababu.
-pia hakunaga maisha yasiyokuwa na changa moto and to me ni sawa ndio maana huwaga nasemaga hapa jamvini kazi ipo pale unapotumika kama ubao kwa wenzio.
-kubwa kuliko yote ni kwamba sikuwah kumchukia mume wangu hadi nifike mahali pa kuona simuhitaj tena.
kwangu mimi kimada kuvaa kitenge changu kulala chumbani kwangu ni mambo mabaya sana lakini sikuona kama yana impact kama hayo niliyoyaonyesha hapo juu.
 
Last edited by a moderator:
Kwenye ndoa kunatakiwa heshima sio uvumilivu vipi uvumilie kama mke wako au mme wako anaenda nje ya ndoa.

Bado uvumilivu unachukua nafasi kama alivyosema gfsonwin, kikubwa hapa kama mumeo/mkeo anatoka nje unatakiwa ujiulize sababu ni nini kabla ya kuchukua hatua hivyo uvumilivu unaanza ndipo maamuzi ya hekima na busara yanafuata. Pasipo na uvumilivu hata maamuzi yanayofanyika pindi mambo ya ndoa yanapokwenda kombo yanakuwa si mazuri kwani kuna kukurupuka.
 
Last edited by a moderator:
Mimi bishanga abashaija nikiwa na akili timamu bila kushurutishwa na wana jamvi,hasa gfsonwin,nakuchukua wewe The secretary uwe mke wangu,katika tabu na raha,hata ukini cheat na Eiyer nitavumilia tu.
Huo ndo uvumilivu,bishanga anaku cheat we umo tu,gfsonwin uko tayari mzee akufanzie na Kaunga kisha uvumilie tu?
 
Last edited by a moderator:

Girl! Thats why i do say i love u! Ur coments, and posts shows and tells how strong ur! Ur my heroine cuz u live heroic and u encourage others! To some extent I saw myself in ths post of urs bt i wasnt strong enough to wait up to the finishing line....u inspire me! Be blesed my dada.
 
Du gfsonwin kwanza pole na hongera pia; mshukuru pia Mungu wako ambaye amekupa hicho kipaji cha uvumilivu na mwisho akaendelea kuwa mwaminifu kwa kukureward (kumrudisha mumeo ndani).

Mimi Mungu hajanijlia kipaji hicho, na nafikiri alijua l am better off this way. Ambavyo kanijalia na kunipa nguvu ya kumilia nitavumilia; ambavyo sina stamina navyo sijilazimishi navyo. I wouldn't wanna be you, pamoja na kwamba nakuadmire.
 

thanks Sabry001 but it wasn't me it was God.
 
Last edited by a moderator:

ma dearest Kaunga nakushukuru sana ila ukweli it was God not me, sijui kwanini niliweza lakin najua Mungu ndiye aliyefanya. Sifa nampa yeye tu. Siwez kumshauri mtu afanye kama mimi ingawa nitampa options nyingi achague anayoitaka ila huu ushuhuda niliona niuandike just to teach others kwamba maisha yana mambo tofauti sana in reality and ukiwa jasiri na moyo mkuu hakuna gumu lolote utakaloshindwa. Be blessed ma dear.
 
Last edited by a moderator:
Bishanga usisahau kwamba kuna mambo mengine huna jibu lake yaani solution comes at the scene. and to it is like that. manake nikuulize hivi wewe Bishanga waweza kumsamehe mkeo anapocheat?
 
Last edited by a moderator:
Bishanga, keshacheatiwa na ANA kavumilia ije kuwa Kaunga? Au una maana Kaizer? Huyo mbona ......... sisemi, nisije nikaongopa nikasababisha maungamo bure!
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…