Uwanja wa Chamazi | Kombe la Shirikisho Afrika' Namungo FC Vs Rabita FC

Uwanja wa Chamazi | Kombe la Shirikisho Afrika' Namungo FC Vs Rabita FC

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Namungo FC leo Jumamosi ya November 28, 2020 wanawakaribisha Al Rabita FC kutoka Sudan katika mechi ya mkondo wa kwanza wa raundi ya awali ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

==========

Update;

Namungo FC wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao matatu bila majibu dhidi ya Al Rabita FC, katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali ya kombe la Shirikisho Afrika, mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Chamazi.

FT; Namungo FC 3-0 Al Rabita FC




Screenshot_20201128-192341.jpg
 
39' Gooooooooaaal Gooooooooaaal

Ni yule yule Stephen Sey anaweka chuma cha pili kwa bao maridadi sana daaaah

Namungo FC 2-0 Al Rabita FC
 
45+1'

Muda wowote mpira utakuwa ni mapumziko katika uwanja wa Chamazi

Naaam mpira ni mapumziko ambapo Namungo FC wanatoka wakiwa wametangulia kwa magoli mawili bila majibu

Namungo FC 2-0 Al Rabita FC
 
65' Go gooooal Gooooooooaaal, Kichuya anaandika bao la tatu muda mchache baada ya kuingia akitokea benchi

Namungo FC 3-0 Al Rabita FC
 
74' anatoka Sabilo, na nafasi yake ikichukuliwa na Adam Salamba Namungo FC

Hata hivyo ameumia, ametoka na ameingia Tangalo
 
Hakuna matumaini kwa Rabita FC kurudisha hizi bao, kutokana na washambuliaji wao kushindwa kupenya ukuta wa Namungo FC
 
87' zimesalia dakika 3 kabla ya kumalizika kwa mchezo huu wa kombe la Shirikisho Afrika' Namungo FC wakitakata kwa bao tatu
 
90+2'

Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa kombe la Shirikisho Afrika'

Manyama anapiga ndefu, mpira unarudishwa na mabeki wa Rabita FC

Naaam mpira umekwishaaaa ambapo Namungo FC wakichomoza na ushindi wa bao tatu bila majibu

FT, Namungo FC 3-0 Al Rabita FC
 
Back
Top Bottom