Uwanja wa Louisville sasa unaitwa Muhammad Ali International Airport kwa heshima yake

Uwanja wa Louisville sasa unaitwa Muhammad Ali International Airport kwa heshima yake

Mohammed Said Mimi si mjuzi wa lugha, unaweza kupitia aya ya kwanza kwenye bandiko namba 15 juu ya maelezo ya Sal Davis.

Hapafu naona umeghabidhika sana bila sababu kumhusu Azarel. Pengine hajarejea kwa sababu Jukwaa hili la historia si maarufu hapa Jf kwa uchangiaji
Plato...
Hata mie si mjuzi hivyo wa lugha hii na nimeeleza kwenye jibu langu
kuwa ikishakuwa lugha si yako ni ya kujifunza hutoweza kukwepa
kukosea.

Na nikamshukuru nikasahihisha.

Lakini sikupendezewa na namna alivyozungumza na mimi hakuwa
muungwana.

Nashangaa kuwa wewe hili hulioni.
Hebu msome upya.

Kaonyesha kukosa adabu ya elimu na hicho ndicho nilichomuasa.
Bahati mbaya unamjibia wewe.

Ama hili la kuwa Jukuwaa la Historia si maarufu sijui uhakika wake
lakini mimi nimefahamika na wengi na nimefanya mijadala mingi
ya kuvutia hapa.

Fanya utafiti kuthibitisha hili.
Kuhusu mstari wa 15 nifahamishe ikiwa pana kosa nitasahihisha.

Umetumia neno ''aya,'' kwangu mimi ''aya,'' ni kitu kingine kabisa.

Kuhusu, ''kughadhibika sana bila sababu,'' hapana sijaghadhibika.
Ningeghadhibika ningeandika fedhuli kama alivyofanya yeye.

Ila nimetaka anifahamu na nimlipe kwa wema wake.

Yeye kanisaidia kusahihisha mswada wa kitabu changu nami
nimehisi nina deni kwake la kumfunza kuwa kuna adabu ya elimu
ili na yeye anufaike kama nilivyonufaika mimi kwa ujuzi wake.
 
Azarel,
"I went to the hotel early morning around 12.30 am."

Ahsante sana ndugu yangu ikiwa kuna makosa mengine nitashukuru kama utanionyesha nipate kusahihisha.
Alama Mohamed Said nadhani hapo ingependeza zaidi ungeandika 06:30 in the morning maana 12:30 ni afternoon hiyo.
 
Alama Mohamed Said nadhani hapo ingependeza zaidi ungeandika 06:30 in the morning maana 12:30 ni afternoon hiyo.
Maalim wangu,
Nimecheka peke yangu kama mwehu hakika huo mbona mchana?

Hatari ya kufikiri Kiswahili huku unaandika Kiingereza na mara
nyingi inapobidi huwa nawapelekea jamaa stori hii ya Sal Davis
na Muhammed Ali wala hakuna aliyenizindua.

Mjukuu wangu kaangalia interview moja nimefanya na South African
Broadcasting Corporation (SABC) miezi michache iliyopita kuadhimisha
ANC Day.

Sasa wakaniomba niende kwenye Maktaba yangu nitoe kitabu cha
Mandela ili inogeshe kipindi.

Wakati natembea kwenda kwenye shabaka la vitabu camera ikawa
inanifuata.

Mjukuu wangu yeye hajapata kuiona nyumba yangu na Kiswahili
chake anababaisha, basi anauliza, ''Is this Babu's home?''

Nimeshangaa.
Home?

Not house?

Mimi ningesema, ''Is this Babu's house?''
Kiingereza kinapokuwa lugha ya pili yapo matatizo.

Mwenye lugha yake hakuona ''house,'' kaona ''home.''

Ahsante Maalim wangu.
 
Mohammed Said Mimi si mjuzi wa lugha, unaweza kupitia aya ya kwanza kwenye bandiko namba 15 juu ya maelezo ya Sal Davis.

Hapafu naona umeghabidhika sana bila sababu kumhusu Azarel. Pengine hajarejea kwa sababu Jukwaa hili la historia si maarufu hapa Jf kwa uchangiaji

Plato...
Msome Maalim Faiza.
Angalia alivyonisahihisha.

Ukimaliza rejea kwa Azarel na fananisha.
 
Braza kwani kuna shida gani kama ungeamua kuandika kiswahili tu lugha ya kizalendo?, maana kiingereza ulichokiandika ni cha hovyo sana mkuu.
 
Back
Top Bottom