Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,409
- 13,262
Sisi wapenzi wa mpira tunapoenda kuangalia mpira Uwanja wowote ule kwa malipo maana yake sisi ni wateja inabidi tuheshimiwe kama wafalme kama kauli mbiu inavyosema kuwa mteja ni mfalme.
Nikizungumzia uwanja wa Taifa wa Mkapa ambao ndio uwanja mkubwa na bora kuliko vyote nchini kwakweli huduma zake ni duni sana na ni uwanja mchafu sana kuanzia vyooni hadi kwenye viti. Yaani unaweza kwenda uwanja wa taifa ukiwa msafi ukarudi mchafu kabisa na siyo mahali kwa kuvaa suti kule kama wenzetu Ulaya. Unafika unakuta viti ni vichafu sana yaani hata kufuta vumbi hawawezi wakati wanapokea pesa nyingi katika kila mechi inayofanyika pale. Hizo pesa wanapeleka wapi kama hata usafi hawawezi?
Unaweza kwenda Taifa ukarudi na magonjwa ya kuambukiza kutokana na vyoo kuwa vichafu sana na mfumo wa maji mbovu kabisa bomba nyingi zimenyofolewa na hakuna anayejali.
Ushauri wangu ni kuwa Uwanja wa taifa ubinafsishe kazi ya usafi au hata uwe inafanywa kwa ajira ya muda maalumu wa siku ya mechi tu. Iwepo kampuni ambayo itafanya usafi nan kukarabati bomba na mifumo ya maji kabla ya mechi lakini pia baada ya mapumaziko wakati washabiki wamerudi uwanjani wafanye usafi na kurekebisha pipes kama zimenyofoka na pia wafanye hivyo baada ya mechi wakati washabiki wameondoka mpaka tena mechi ijayo.
Kwa upande wa ndani wanaweza kuitisha hata vijana 200 au 300 kwa siku ya mechi wafute viti vyote kwa ujita wa 10000 kila mmoja na ofa ya kuangalia mpira ili washabiki wakiingia wakute viti visafi ili wasichafuke nguo zao.
Vile vile katika mechi ambazo hazina mashabiki wengi haina haja ya watu kutawanyika sana na kutumia viti ovyo au kuharibu. Wanaweza kuamua kuwa washabiki wakae viti vya orange au mwisho vile vya kati.
Naomba wahusika wazingatie usafi jamani wengine wanaaleji ya vumbi wakiingia wanakuta mavumbi kama yote. Haifai
Nikizungumzia uwanja wa Taifa wa Mkapa ambao ndio uwanja mkubwa na bora kuliko vyote nchini kwakweli huduma zake ni duni sana na ni uwanja mchafu sana kuanzia vyooni hadi kwenye viti. Yaani unaweza kwenda uwanja wa taifa ukiwa msafi ukarudi mchafu kabisa na siyo mahali kwa kuvaa suti kule kama wenzetu Ulaya. Unafika unakuta viti ni vichafu sana yaani hata kufuta vumbi hawawezi wakati wanapokea pesa nyingi katika kila mechi inayofanyika pale. Hizo pesa wanapeleka wapi kama hata usafi hawawezi?
Unaweza kwenda Taifa ukarudi na magonjwa ya kuambukiza kutokana na vyoo kuwa vichafu sana na mfumo wa maji mbovu kabisa bomba nyingi zimenyofolewa na hakuna anayejali.
Ushauri wangu ni kuwa Uwanja wa taifa ubinafsishe kazi ya usafi au hata uwe inafanywa kwa ajira ya muda maalumu wa siku ya mechi tu. Iwepo kampuni ambayo itafanya usafi nan kukarabati bomba na mifumo ya maji kabla ya mechi lakini pia baada ya mapumaziko wakati washabiki wamerudi uwanjani wafanye usafi na kurekebisha pipes kama zimenyofoka na pia wafanye hivyo baada ya mechi wakati washabiki wameondoka mpaka tena mechi ijayo.
Kwa upande wa ndani wanaweza kuitisha hata vijana 200 au 300 kwa siku ya mechi wafute viti vyote kwa ujita wa 10000 kila mmoja na ofa ya kuangalia mpira ili washabiki wakiingia wakute viti visafi ili wasichafuke nguo zao.
Vile vile katika mechi ambazo hazina mashabiki wengi haina haja ya watu kutawanyika sana na kutumia viti ovyo au kuharibu. Wanaweza kuamua kuwa washabiki wakae viti vya orange au mwisho vile vya kati.
Naomba wahusika wazingatie usafi jamani wengine wanaaleji ya vumbi wakiingia wanakuta mavumbi kama yote. Haifai