Uwanja wa Taifa watolewa nyasi bandia na kuwekwa nyasi halisi

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
Mwonekano wa Uwanja wa Mpira wa Taifa Jijini Dar es Salaam Ukipandwa nyasi mpya na si za bandia.

Hivi zipi nzuri? Maana mimi nilidhani hizi bandia ndo nyasi nzuri maana ni vigumu uwanja kuchimbika mashimo mashimo na muda wote uwanja unakuwa umenyooka.

 
Halisi zinahitaji uangalifu kwenye matunzo.
 
Kiongozi kushindwa kutunza nyasi huo ni ujinga wa hali ya juu, wanapata pesa nyingi sana, gharama ya kisima cha maji na kuwalipa watu wawili kwa ajiri ya kuhudumia nyasi za uwanja sio kitu TFF au wizara ya michezo wanaweza kushindwa, ziwe nyasi bandia au halisi, wakishindwa kuzitunza viongozi wafungwe jela.
 
Nazo wanaweka wachina ama?!! Maana nchi hii haiishi vituko, kuna siku nilimwona mtu anaomba msaada ili awasaidie watu fulani kutoa funza miguuni mwao. Nafikiri aliyetuloga tayari kafa kwani mambo mengine tujiongeze jamani
 
Matunzo gharama nyasi za bandia ,nyasi za kawaida unamwagilia maji taka mbolea tosha kabisa ,hapo wanakwepa gharama ukizingatia uwanja wenyewe unavyodekeshwa kutumiwa pesa zitatoka wapi ,
 
Nyasi kwa kawaida Zina muda wakutumiwa na kuchakaa hivyo ungolewa na kupandwa upya ataa zile za mifugo au wanyama porini kuna wakati wanachoma moto ili ziote upya
 
Uwanja Wa taifa au Uhuru !!??
Ni uwanja wa taifa na sio Uhuru.
Uwanja wa Uhuru ni ule wa zamani mali ya Jeshi la Wananchi. Shamba la Bibi.
Uwanja wa taifa ni huu mpya unaobena watu 65,000.
 
Kabla ya game ya Everton walipanda na kureform mpango wa maji. Sasa tuseme wanau-review huo mpango wa kabla ya game ya everton au ni picha za zamani?
 
Uwanja wa taifa haijawahi kuwa na nyasi bandia

Pili nyasi bandia hazifai kabisa labda kwa viwanja vidogo kama wa karume

Ni kawaida kwa viwanja kukarabatiwa na kuoteshwa nyasi zingine
 
Matunzo gharama nyasi za bandia ,nyasi za kawaida unamwagilia maji taka mbolea tosha kabisa ,hapo wanakwepa gharama ukizingatia uwanja wenyewe unavyodekeshwa kutumiwa pesa zitatoka wapi ,
Mtoa mada kavurugwa uwanja wa taifa haujawahi kuwa na nyasi bandia, uhuru ndio kuna nyasi bandia
 
Huyu mtoa mada mbona kama hajui mambo ? Huo uwanja nyasi hali kwani ujaona wanaupiga maji ? Waache wazungu wakarabati ila hela yao watakuja kucompesate kivingine.
 
ulikuwa na nyasi halisi mkuu,uwanja huo haujawahi kuwa na nyasi bandia
 
Umenikumbusha.

Last weeks nilikuwa Iringa, nikaingia kwenye kibanda umiza kimoja kucheki game watu wakawa wanabishana sana suala la Nyasi za National Stadium.
Wengi wanadhani uwanja wa Taifa una nyasi bandia "Artificial Turf".

Ule uwanja tangu ujengwe haukuwahi kuwekwa nyasi bandi Mkuu. Kinachofanyika sasa ni kubadilisha breed ya grass pale chi.

Hapo awali zilikuwa zikitumika "Empire Zoysia Grass" na sasa zinapanda "Bermuda Grass". Hizi zote ni Natural Grasses.
 
Siyo nyasi bandia bali wanatoa nyasi za muda mfupi na kuweka za muda mrefu kwani zilizopo ubora wake umekwisha hivyo kuondoa tatizo hilo la kubadili nyasi kila baada ya muda mfupi ni gharama na hasara kwa taifa hivyo ni bora zipandwe za muda mrefu, nyasi bandia zipo uwanja wa uhuru.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyasi za uwanja huo zilikua halisi, lakini huwa kuna kautaratibu kila baada ya muda flani unabadili nyasi....kama emirates wanavyofanya kila ligi ikiisha nyasi zinatolewa wanapanda mpya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…