Uwekezaji wa MO na udhamini wa Azam

Jr king

Member
Joined
Nov 4, 2019
Posts
50
Reaction score
55
Heshima kwenu wakuu.

Moja kwa moja niingine kwenye maada husika, kumekua na mkanganyiko Kati ya uwekezaji uliofanya na Mo pale Simba na udhamini uliofanywa na Azam kwa wanandinga wa jangwani.

Sie wa buhigwe kitu kinachotukanganya ni je? Inamaana Mo ataimiliki simba maisha kwa hiyo 21B? Na yanga amejidhaminisha 41B kwa miaka 10 tu?

Sasa kama ni hivo mbona kama Simba tumepigwa?

Tafadhali wajuzi wa Mambo tuelimisheni hicho kitu.
 
Huu uzi wako ni vyema ukaufuta! Maana mashabiki wa hiyo timu huwa hawapendi umseme Moo wao au yule mvuta bangi ya Kimbiji, Haji Manara!
Siwezi kuufuta mzee wangu kwa kuogopa hawa watu, nina watu mm...hii Simba mnayoiona tumeipigania Sana, hatuwezi kukubali iangukie mikononi mwa mabanyenye kirahisi namna hiyo....narudia nina watu....
 
Siwezi kuufuta mzee wangu kwa kuogopa hawa watu, nina watu mm...hii Simba mnayoiona tumeipigania Sana, hatuwezi kukubali iangukie mikononi mwa mabanyenye kirahisi namna hiyo....narudia nina watu....
Ikiwa mzee kilomon aliyekua Captain wa Timu Tena akitoka mazoezini alikua akienda kubeba matofali kuisaidia mafundi kujenga jengo la Klabu pale msimbazi kavuliwa uanachama na kufukuzwa wewe ninani wa kuhoji mipango ya MO!!
 
Mo ni tapeli hajawekeza chochote. Huwezi kuwekeza bilioni 20 halafu ukitakiwa kuweka ushahidi wa hizo bilioni 20 kuwekezwa Simba unaanza kung’aa macho.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…