Uwekezaji wa Serikali ya Rais kwenye Sekta ya Kilimo wazaa matunda. Tanzania yaipiku Nigeria na kuwa Mzalishaji namba 2 wa Mahindi Afrika

Kwenye kilimo NAMI naungana na serikali vijana tuhakikishe Samia akiondoka ofisini 2030 pia tuwe na aseti za mamilioni zilizotokana na kilimo.
Nani kakuambia anaondoka 2030 kwani si ndio atakuwa anamaliza muhula wake wa kwanza?
 
Kweli mmedhamiria ila bado sana
Inatakiwa tulime cash crops kwa wingi sana
Serikali ipambane ili tuuze sana nje
Team wizara ya kilimo wako vizuri sana kwenye kazi zao
Ndio lengo la Serikali Kupitia ajenga 1030.

Mipango iliyopo ni Mingi na ya maana sana ,kama itatekelezwa basi hakuna wa kutusogelea hapa Africa.
 
Yes ,huo mwaka target ni Kilimo kichagie 10% ya GDP

Ngano tujitosheleze Kwa 80%

Tufite habari za kuagiza Mafuta ya kula

Na mazao ya Kilimo yawe sehemu kuu ya exports ya Nchi.

Tuache kuagiza mbegu na mbolea Nje ya Nchi.
Kwenye kujiendeeleza naunga mkono πŸ’―
Yaani wao ndio watuombe msaada wa chakula
 
Naunga mkono hoja. Ni mda sana niliwahi sikia BBC Tanzania ni ya3 kwa uzalishaji maharage barani Africa ikiongozwa na Kigoma,Kagera,na kilimanjaro. Leo sijui tutakuwa wangapi maana Mikoa mingi inalima sana magarage ikiwemo Mby, Njombe,Songwe, Iringa.
Hii nchi haina njaa hasa zikiwepo logistic nzuri za kusambaza chakula. Kongole watanzania kwa kukifuata kilimo. Tusisahau sekta kama ya Parachichi inakuwa kwa kasi sana. Ipo sikuTZ itakuwa ya 1.
 
Kilimo Kitamu Asikuambie Mtu
 
Ngoja nifuatilie data
 
Kilimo Kitamu Asikuambie Mtu
Nimeona formation Moja ya mahindi unaweza pata gunia Hadi 60 Kwa acre ila ni mwendo wa mbolea tuu yaani 2:2:2:2 sawa na mifuko 8 Kwa ekari.

Na Mpango wa Kujaribu formation ya mifuko 6 yaani 2:2:2 walau nipate 34-40 bags per acre.Awali nilikuwa natumia 2:1:1 /acre naambulia gunia kati ya 30-34 kulingana na timing na Hali ya hewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…