Uwezekano wa Magufuli kuongoza nchi kwa kipindi cha pili haupo

Uwezekano wa Magufuli kuongoza nchi kwa kipindi cha pili haupo

Yupo vipindi vyote, akikaribia kumaliza kipindi cha mwisho wewe mwenyewe utarudi kuomba katiba ibadirike aongeze kipindi kingine cha tatu
 
Kuna wakati akili za mizimu nda akili sahihi zaidi kutumika kwa wakati huo, ukijifanya sober muda mwingine unapotea kijasiri bila mwenyewe kujua kama unapotea. Wacha movie iendelee
 
For what I know ,move ya lowasa ni strategic, Rostam is behind all the plan
 
Baabba Mmungu tunakuomba...
Hawa waattu ni wamelaaniwa na kuamua kumtumikia shetani...
Katika Jiinnaa la Yyessu Wasshhiindwe!.
P
Baaaabbababa "Mungu" wetu wa Tanzania, Africa na dunia kwa ujumla, bila kusahau Chatototo yetu, tunaomba uturudishie Ben, Azory, uruhusu demokrasia, uruhusu bunge live, ukemee utekaji, utupe nyongeza zetu makazini , Lisu asipigwe risasi tena. Hawa watu wanaokupinga washindwe kwa jina la Yesu ukisha warudisha hao niliowataja.
Kwa jina la Yesu AMEEN!
 
Nimepata mwanga kuhusu baadhi ya wanasiasa wa ccm wasiotarajiwa kujitokeza hadharani kuegemea upande mmoja kwenye sakata hili la waraka wa wastaafu wakati wengine wametulia wanatazama tu!
 
Wanaojua mzizi wa haya yanayoendelea ni wachache sana.

Hamjiulizi kwanini jiwe mpaka sasa kigugumizi? Hujuma anazofanyiwa ni reaction ya kitendo cha jiwe kujipeleka kwenye kambi ya Lowassa.

Hope hilo swali huwaulizi washambuliaji wa Uzi huu ambao hata wewe unaona wazo kuwa wako hapa siyo kwa madhumuni kushiriki mjadala kwa hoja bali kushambulia na kutisha!
 
Niliwahi kusema kuwa kile kitendo cha kumrudisha Lowassa chamani na kumrudisha Rostam Aziz nchini ni cha kuangalia kwa jicho la tatu!!!

Nimepata kumsikiliza Mzee mmoja mstaafu wa nchi hii akizungumza kwenye jukwaani moja la uongozi nje ya nchi. Aliwalaumu sana viongozi wa Afrika kwa ubinafsi uliopitiliza! Ndio haya ya kuwavuta na kuwakumbatia baadhi ya watu kwa maslahi binafsi ya kisiasa badala ya maslahi ya nchi.
 
Umemalizana na Acacia? karibu tena kwenye siasa halisi, eti yule mtu wetu wanampigia tena chapuo kwanini humshauri akachunge ng'ombe kama alivyoahidi.
Vitu vingine ni ndoto tuu za mchana, unaamua usichangie ili tuu kuheshimu mawazo ya watu. Utaratibu wa CCM kuhusu the incumbent president unajulikana, who would dare do anything?. Kinana, Makamba,Membe, Nape na January they are history!, they are things of the past, kama yalivyo ...ya jana, hayanuki!. Hakuna mtu CCM alikuwa na nguvu na wafuasi kama Lowassa, alipoondoka, aliondoka peke yake na watu wake wachache na hakukimega chama, hivyo wengine wote they are almost nothing.
P
 
Na Anderson Ndambo.

Kuna mambo yanahitaji jicho la Tatu kuyaona na pengine kuyaamini. Tabia mojawapo ya siasa ni kubadilika badilika kulingana na majira na wakati kutokana na sababu za wakati husika, lakini kwa Tanzania mabadiliko haya yamekuwa na kasi kubwa mno, hicho si kitu cha kawaida, kama ambavyo Magufuli mwenyewe hakutegemea kuukwaa Urais wa Tanzania kwa kuchaguliwa kuwa mgombea wa ccm, vilevile mazingira kama yale yanaweza kubadilisha hali ya mambo na matokeo yakawa tofauti na tunavyodhani kuelekea 2020.

Rais Jakaya Kikwete aliingia madarakani kutokana na kuimarika kwa kundi lenye nguvu lililokuwa likiongozwa na Lowassa ndani ya ccm, na kwa wakati huo ndio lilikuwa kundi lenye nguvu ndani ya chama hicho (ccm) lililoweza kudhihirika na kuweza kutoa ushawishi na kulazimisha Kikwete kuingia madarakani na kundi hilo likamkaanga vikali, Salim na kumtowesha kabisa kwenye ulingo wa siasa za kitaifa ndani ya ccm na nchi kwa ujumla. Kundi hili lilianza kujijenga tangu wakati Nyerere akiwa madarakani na kimsingi lilikomaa sana wakati wa Mkapa kiasi kwamba Mkapa akashindwa kulidhibiti.

Mwaka 2015, kundi hili lilifikia hatua ya mwisho na ya juu kabisa ya kupasuka kwakwe, baada ya Kikwete ambae ni sehemu ya zao la kundi hilo kujichomoa na kumsaliti king mwenzie (Lowassa) na kutengeneza kundi jipya ndani ya ccm. Kutokana na nguvu ya Lowassa wakati ule ccm ambayo ilitokana na kundi lake la asili, kundi la Kikwete lilikuwa na wakati mgumu sana, kwasababu lilikuwa halina ukubwa na ushawishi mkubwa kama kundi ambalo kikwete amelisaliti isipokuwa tu kutokana na Ushawishi wake Kikwete kama Rais na mjumbe mzoefu alie asi na baadhi ya wajumbe wake na wote tunafahamu shughuli waliokuwa nayo walipo mkata Lowassa.

Sasa Magufuli amezaliwa kutokana na Kundi kubwa ndani ya ccm kuvunjika kwa kusalitiana na kwa bahati mbaya sana, makundi haya yote yalijikuta yako tena kwenye uwanja mmoja (ulingo wa siasa (ccm), na katikati yupo Magufuli. Kundi la Kikwete kwa sasa lina nguvu kubwa kutokana uwekezaji mkubwa wa kikwete ndani ya serikali na ccm, lakini kundi la Lowassa ni kubwa kutokana na uzito wa wajumbe wake ndani ya ccm na ushawishi wao kwa Rais magufuli. Vita inapamba moto. Na makundi yote haya mawili kwanza hayakubaliani, lakini kubwa zaidi haya mkubali Magufuli kwasababu mwenendo wa magufjli una athari zinazo fanana kwa makundi yote na timu yake. Kundi la lowassa linatumia fursa tu, na tusisahau Ndoto ya Lowassa kuongoza nchi haijafa.

Rais magufuli anadhani yuko salama, kwasababu kuna vita ya ziada kwa makundi haya mawili, anadhani kuliimarisha kundi la Lowassa kutamsaidia yeye kupita kiulaini 2020 kwasababu ya mvutano mkali utakaozidi kuimarika baina ya makundi haya mawili ambayo tayari vita hiyo imeanza kujidhihirisha hadharani baada ya matamshi ya Bashe yenye dhana ya kisasi dhidi ya watu wa kundi la Kikwete. Kitendo hiki kimemshawishi sana magufuli kwamba ataweza kuvuka kiulaini sana. Na hili linaonesha kupata mafanikio kwasababu kundi la lowassa sio tu linapewa nyadhifa sasa na magufuli bali, limeanza kuinunua vita ya magufuli na wakina musiba wanaanza kutoweka kiana.

Kinachokwenda kutokea..

1. Kwanza tuelewe, makundi haya yote yana ushawishi mkubwa ndani ya ccm kuliko magufuli mwenyewe.

2. Makundi haya yana ushawishi mkubwa ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama kuliko magufuli mwenyewe.

3. Magufuli sio tu, hana ushawishi mkubwa kwenye vyombo vya usalama kuliko mahasimu wake, Bali hata ndani ya ccm na hata kwenye nchi (Taifa) maana watu wamemchoka kabisa, kweli Raia tumemchoka kabisa.

4. Magufuli amenza kuunda chama chake kipya ndani ya ccm (ccm mpya), inayobebwa na kundi la watu ambao hawana ushawishi wowote ndani ya ccm, hawana uzoefu wa kutosha wa kuongoza nchi, hawana mizizi mirefu ndani ya siasa za ccm, kimsingi watu hawa ni wanasiasa kwenye taswira ya magufuli (magufulisim).

Sasa, mwisho wa kukomaa kwa vita hii kubwa ya mafahari wawili, itapelekea nchi kuwa kwenye hali mbaya zaidi kiuchumi, kisiasa na kijamii. Jamii itazidi kuyajua maovu mengi yaliofichwa dhidi ya ccm, bila kujali ni ccm asilia au mpya au nani, na kimsingi jamii itakuwa imejaa chuki kubwa dhidi ya ccm yote, bila kujali huyu anatoka kundi gani, kwasababu wote hawa nje ya ccm wanajulakana kama ni ccm tu. Magufuli hatokuwa kwenye nafasi ya kufanya mambo mapya, kwasababu ya mtifuano huu na mtifuano huu ndio utakao chukua nafasi kubwa zaidi kuelekea 2020 kwenye masikio ya watu na si magfuli, kimsingi magufuli atakpjikuta anafika 2020 akiwa anachukiwa kuliko mwanzo.

Itakapofikia hapo, wakati wa kufanya maamuzi ya nani anapaswa kuivusha ccm, itategemea mshindi wa kati ya makundi haya mawili, lile la Kikwete na lile la Lowassa, na kimsingi, vyombo vya dola na usalama vitakuwa kwenye nafasi kubwa ya ushawishi ndani ya nchi na ccm yenyewe kuliko wakati wowote ule, na jamii itakuwa ikiamini zaidi kwa wapinzani, hapa ndipo maamuzi ya ama magufuli au mwingine ndani ya ccm atapaswa kuwekwa kama mgombea yanaweza sio tu kufanyika na ccm wenyewe, pengine Jeshi la nchi, na kwa vyovyote vile, jeshi la nchii kwa sisi wachambuzi wa mambo haliwezi kumruhusu magufuli kuendelea na awamu ya pili. Chakuzingatia tu, wakati huo (2020) kuna uwezekano baadhi ya watu hatutakuwa nao, kimwili au kisiasa, akiwemo Magufuli mwenyewe. Hapa ndipo namuona Lowassa akiibuka tena.

Watu wanaosema, ccm imekuwa ikifikia hatua kubwa ya mpasuko, na huweza kujinasua upya, wanasahau wakati huo, kulikuwa na kundi moja, na baadae likaongezeka hili la pili ambalo limejengeka kwenye msingi wa visasi, na sasa tuna makundi mawili yenye nguvu yasiokuwa tayari kupatana na kukaa meza moja, kitu ambacho hakijawai kutokea huko nyuma.

Hichi kinacho onekana Lowassa na Rostam kumuunga mkono Magufuli si kitu cha kufuraia sana, usishangae 2020 mgombe wa ccm akawa Edward Lowassa na sio Magufuli tunae dhani ndie. Mwelekeo wa mambo wa sasa unabadilika kwa kasi kubwa sana, na kuna kila dalili za ccm kufikia tamati, ijapokuwa kweye mazingira tata sana. Lowassa ni mzuri sana kwenye kuficha na kulinda hadhi yake yeye binafsi. Mwaka 2015 kuna utafiti ulionesha ndie amgombea pekee aliekuwa na ushawishi mkubwa kuliko wanasiasa wengine kwa tofauti ya asilimia 11 akifuatiwa na Dr. Slaa. Huu ni ushawishi binafsi bila chama. Na kimsingi anajua jinsi ya kuwatumia wengine, na ana watu wenye weledi mkubwa kwenye kumlinda tofauti na magufuli anaetetewa na vichaa kama musiba.

Naendelea kutoa ushauri kwa vijana wa ccm, kujaribu kuchagua upande sahihi mapema na sio kukesha kupyauka, leo unamtukana huyu, kesho unamtukana yule, mwisho unajikuta unatakiwa kumsifia mtu uliemtukana jana, utasimamaje? Vijana muwe wenye hekima sana, na pengine mjitaidi kunyamaza kimya, unaedhani ana nguvu leo, kesho unaweza kumkuta ni laini kama siagi......kuni zinawaka moto sana....

A. Ndambo

Umechambua vema ila umeweka chumvi hadi kusahau Mpendwa wetu lowasa(kulingana na clip ya harusi ya mwanae) ni mgonjwa, naamini hataweza kugombea tena bali atampa saport magu.
 
Nimepata kumsikiliza Mzee mmoja mstaafu wa nchi hii akizungumza kwenye jukwaani moja la uongozi nje ya nchi. Aliwalaumu sana viongozi wa Afrika kwa ubinafsi uliopitiliza! Ndio haya ya kuwavuta na kuwakumbatia baadhi ya watu kwa maslahi binafsi ya kisiasa badala ya maslahi ya nchi.
Nimepata kumsikiliza Mzee mmoja mstaafu wa nchi hii akizungumza kwenye jukwaani moja la uongozi nje ya nchi. Aliwalaumu sana viongozi wa Afrika kwa ubinafsi uliopitiliza! Ndio haya ya kuwavuta na kuwakumbatia baadhi ya watu kwa maslahi binafsi ya kisiasa badala ya maslahi ya nchi.
Unachokisema kiongozi ni dhahiri kipo. Watu hawajui kuwa viongozi kama Lowassa na Rostam wana historia yenye ukakasi kidogo kama tulivyoaminishwa na wahusika. Wao kubadilika ghafla na kuwa wazuri,ni jambo la kushtua. Kuna mengi yapo njiani. Tukae hapa hapa "stendi"yatatukuta!!!👊🏿👊🏿👊🏿
 
Duh! Wewe ndio umechemka kabisa kumleta Ngoyai kwenye equation. Mtu ambaye yuko 'ICU' anawezaje kweli kugombea Urais?
Labda hujaona clipp yake ya hivi karibuni... Ngoyai keshajichokea. The best for him now ni kujiandaa kiroho kwa safari inayofuata...
Hoja yako haina mashiko.Hatakuwa wa kwanza.
Aliyekua rais wa Algeria amegombea misimu miwili akiwa mgonjwa taabani.
 
Chakuzingatia tu, wakati huo (2020) kuna uwezekano baadhi ya watu hatutakuwa nao, kimwili au kisiasa, akiwemo Magufuli mwenyewe


Hiyo imenitisha!! kah!
 
Mkuu hizo ni ndoto za Alinacha za mchana kweupe rais ataongoza awamu ya 2 na kwa atakayofanya tutatammani tumuongeze mda tutampa miaka mingine 20 jmla iwe 20 rais gani ukiacha nyerere alifanya mambo makubwa kama haya?? Alofanya Magufuri??
Kafanya nini kikubwa sana ambacho kimetowa matunda kwa taifa?inaonekana wewe ni mshabiki Wa chama tu au umri wako Mdogo au uwezo wako Wa hisoria ya nchi huijui vizuri wewe tafadhali usiwabeze marais waliopita unamsifia huyo kwa vile amekuta waliomtangulia wamemsafishia njia mfano Mdogo kwenye udhibiti Wa bandari ingekuwa hajakuta tayari imeshatengenezwa system kubwa ya TANCIS angedhibitije kwa system ya zamani ya Asycuda +unakumbuka mtwara kusafiri kwa basi ilikuwa ngumu?je unajuwa bwawa la lihasi lilijengwa awamu ipi?unajuwa Tanzania barabara zilikuwa chache na mikoa michache?unajuwa nyerere aliacha megawati ngapi za umeme? Na rais huyu amekuta nchi ina mgwatts ngapi?usiwabeze waliopita wewe kwanza huenda wewe umesoma shule za kata ambazo nijuhudi za marais waliopita tuulize sisi tuliokuwepo awamu zote za nchi hii usinge sifiya uongizi Wa nyerere tumevaa kaptula zenye viraka viraka tumetembea peku shule nzima hakuna mwanafunzi anayevaa viatu 'kama upenda kusifu sifu lakini usimdhau baba au mlezi aliyekule mpaka ukapata digree uliyonayo
 
Huwa nacheka sana kila napomaliza kusoma habari za wanoandika Mh.Membe kugombea, pengine kupita na kama hizi za mtoa hoja..Mimi kwa kuitazama siasa ya Tanzania nilibaini kuwa CCM inapokuwa na migogoro tayari vyama vya upinzani huwa havina nguvu na matayarisho kwa ajili ya uchaguzi isipokuwa tu ujanja aliofanya Mh.Mbowe 2015 japo kuna watu walimbeza bila kujua nini maana ya Tactics. Mimi kitu nachokiona hapa katika kuelekea uchaguzi wananchi wapo njia panda katika mfumo wa kujiuliza nani atapitishwa..automatically wanakuwa wanajiandaa kuipigia kura CCM maana atakayepita kura ya maoni wanamchukulia kuwa ana uwezo na hakuna jinsi ya kumzuia..hivyo basi kwa kuwa kura ni siri watu humpigia kura mgombea urais CCM. Sababu kuu ni kwamba amepita ndani ya CCM huyu ni mwamba, pili wasiwasi kuwa vyama vingine vya siasa havijaonesha kuwa vina mwamba kwa ajili ya uchaguzi ujao au mwamba wao ameyumbishwa kisiasa.
Hoja ya eti kuna mpasuko wenye kundi la JK na kundi la Lowassa hii hutokana mtazamo wa siasa tu ndani ya CCM ambao mwisho wa siku halmashauri kuu humaliza hii hali na wanachama wa CCM hufikia makubaliano (rejea chaguzi zote tangu1995).
Watu wanajichanganya wanashindwa kubaini kuwa kama Mh.Magufuli hana kundi lenye nguvu basi ana watu watiifu wenye weledi na wanaoelewa nini maana ya kuwa mwenyekiti wa chama..pengine wapo katika kila kundi ila wanaamini katika mfumo wa CCM kupata mtu sahihi,yani wakiona huku kachukua fomu mtu fulani basi wakati wa kumpata mgombea wanajikuta wote wanaona bora huyu asiye na kundi kubwa ili nasi kundi letu tubaki salama.Makundi haya hutokana na tofauti za kiitikadi na huwa hayawezi kuwa na nguvu kuliko CCM.
Mimi binafsi naona nafasi ya Mh.Magufuli bado ni kubwa kugombea 2020 labda kama atakataa mwenyewe maana kuongoza Taifa hili yataka "Moyo wa Ujasiri na Uvumilivu".
 
Back
Top Bottom