Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbona CCM wanaimba tutaisoma namba na sisi tumevumilia?Mkuu tukiacha ushabiki je kuna nini cha ziada tumejifunza kwenye Huu wimbo
Mkuu hawa watu wanatamani kutulazimisha watu wote tuimbe nyimbo zaoUnamlinganisha na nani hadi useme uwezo wake ni mdogo? Naona umeandika huu uzi kwa mihemko.
Nyimbo yake ni ile inayosema hawanywi sumu hawajinyongi ccm mbele kwa mbeleWe uko wapi wimbo wako uliotunga tuulinganishe na nyimbo za Roma?
Mkuu hawa watu wanatamani kutulazimisha watu wote tuimbe nyimbo zao za kumsifia MekoUnamlinganisha na nani hadi useme uwezo wake ni mdogo? Naona umeandika huu uzi kwa mihemko.
Mchimba visima anayemkosoa Daktari hajui kutibu.Mimi sio wanamuziki, ila ukweli usemwe
Ukweli au mtazamo wako?
#CommonSenseisnotCommon.
Pandikizi tawi la JF nataka kuwa mpiga zumari wa CCcM kama wewe apo, je wanalipa ngapi huko kwa kazi kama hii ya kwako?
Nitolee wivu wako hao wakina mbaraka waliimba kutokana na nyakati zao, Roma naye anaimba kutokana na nyakati zake usitulazimishe wote tuwe na degree 4
Wewe mwenyewe mbona kuna wajumbe kibao humu wanakuona kama kilaza tu! kutokana na michango yako mingi ya kinafiki na ya kujipendekeza kwa magu!
Mrisho mpoto alishawahi kusema ukisikiliza nyimbo zake mara mbili usipoelewa tambua huna uwezo wa kuzielewaHuyu kijana anauwezo mdogo wa kutunga na kuandika nyimbo kufikisha ujumbe wa aliokusudia. Badala yake amejikita kwenye hisia, mihemko na nadharia. Ila ukikaa na kusikiliza hakuna ujumbe unaoleweka.
Hawa vijana wangejifunza kwa majabali ya muziki waliotangulia akina marijani rajabu na wengine. Nimepata muda wa kusikiliza wimbo wa Roma mkatoliki sijaona cha maana wala meseji za kueleweka zaidi ya upayukaji tu. Nashangaa Kwanini watu wamehamaki wakati ni wimbo wa kawaida tu uliojaa hisia kuliko uhalisia
Mimi nilikuwa mfuasi wa nyimbo za Mr.Sugu, Profesa Jay, Solo thang na Afande Sele kwenye upande wa nyimbo za kufoka foka
Hawa wanamuziki wasasa sio wabunifu ni muda sasa tuwachoke