Uwiano wa uwakilishi baina ya Zanzibar na Tanganyika

Uwiano wa uwakilishi baina ya Zanzibar na Tanganyika

Wanajamvi, hizo hapo juu ni nukuu chache tu ndani ya kinachodaiwa ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania...! Huu ni ubabaishaji...someone somewhere must be joking or we are being played for fools! Na usanii unazidi kuendelea hapa chini...


Pamoja na mapungufu yaliyomo kuna ndani ya hiyo katiba, kitu kimoja kiko wazi...hakuna popote ndani ya hii katiba anapotambuliwa Rais wa Zanzibar kama Rais wa nchi...! inashangaza nchi kuendeshwa bila hata kufuata hiyo katiba yenyewe...huyo anayeitwa Rais visiwani kwa kweli ni mkuu wa sehemu ndogo tu ya nchi inayojulikana kama Tanzania Zanzibar, yenye idadi ya watu wasiofikia hata asilimia 3% ya Watanzania wote!

The naked truth...Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Mrisho Kikwete anavunja katiba aliyoapa kuilinda na hivo kupelekea Rais wa Tanzania Zanzibar naye ku follow suit. Swali ninalojiuliza ni hili, je tunao wawakilishi bungeni? Where are they?
Mkuu Mag3, wawakilishi wapo kwa bahati mbaya hakuna mwenye kufikiria nchi kwanza, kila mmoja anafikiria jinsi ya kurudi bungeni next time.

Pili, hizi siasa za uchama nazo zimezidi na kudumaza nchi. Mathalani, haiwezekani mbunge wa CCM kusimama na kuhoji au kuunga mkono hoja inayokinzana na sera za chama chake.
Wenzetu wengine duniani mbunge anakuwa mwakilishi wa watu kwanza kabla ya chama.

Pengine hili nalo linaongeza uzito wa kuwa na wagombea binafsi watakaokuwa na mawazo huru bila kufungwa pingu za vyama.

Umekumbusha kitu muhimu sana katika katiba. Baada ya tetesi za mafuta SMZ imekimbilia BLW na kurekebisha katiba yake inayoeleza Zanzibar na eneo lake ikiwa ni mkakati wa kulinda kile kilichosemwa ni mafuta.
Katika kufanya hivyo walijikuta wanakiuka katiba ya JMT kwakiwango cha hali ya juu sana.

Ndio maana tunasema hivi, ili kuondoa sintofahamu na maruwe ruwe haya ZNZ iliyo na uwezo wa kubadilisha mambo mengi bila kuulizwa ina uwezo wa kuamua hatima yake ndani ya muungano bila kutegemea Tanganyika.
 
Mkuu Pasco hili bandiko lako akiliona Jussa Makengeza utapigwa marufuku usikanyage Visiwa vya Karafuu ha ha ha.

Kwa upande wangu, naomba kutofautiana na nyinyi!.

Mfumo wa muungano wetu ni mfumo wa ndoa, Tanganyika ndiye mume amemposa Zanzibar ambaye ni mke! na kujenga familia inaitwa Tanzania!.

Japo ni mume ndiye aliyelipa mahari, mume ndiye mwenye kipato, mume ndiye anayemlisha mkewe na kununua mahitaji yote ya nyumba, na kugharimia gharama zote, hizi ni wajibu wa mume, lakini linapokuja suala la haki, mume na mke wana haki sawa ndani ya nyumba hiyo!, na hata ikitokea ndoa ikavunjika, watagawana mali pasu kwa pasu, japo ni mume ndiye aliyenunua kila kitu na mke alikuwa golikipa tuu!.

Ila ukiona mke anapewa kila kitu halafu bado anaanza kufanya visa na vitimbi, ili utoe talaka, ujue keshapata bwana anayemdanga, kama na wewe ukiona umemchoka usisubiri kuchoshwa na visa, mpe talaka yake muachane kwa amani na usalama, lakini kama bado unampenda, hata afanye visa vipi, talaka hutoi na sana sana utamuadabisha tuu!.

Tena mke huyu ni mtukutu wala hakumbuki fadhila!, ile December 1963, aliolewa na Mwarabu!, si unawajua tena Waarabu na ile michezo yao ya kwenda kinyume!, mke yakamshinda, tarehe 12 Januari 1964 akaasi ndoa ya Mwarabu akatoroka kwenye nyumba ya ndoa kwa kusaidiwa na yule Mganda Okello, mke huyo alijileta mwenyewe kwa Dume la Mbegu, Tanganyika, na kuomba ndoa ya mkeka ili kumzua Mume Mwarabu asimrudie maana hata talaka hakupewa!, Tanganyika hakufanya ajizi, akamposa na kumuoa chap chap!, tangu wakati huo kamfanyia mengi tuu sasa leo ndio vinajotokeza hivyo vibwana vinataka kumdanganyia peremende, eti ohh "nitakupendezesha kama Dubai", omba talaka nitakuoa mimi! na ahadi chungu tele!, hivyo hujakoma tuu?!.

Tanzania bado inampenda mke, hata alete chokochoko kupitia vitimbakwiri vya mwarabu, talaka hatoi!, ila mke huyu atashikishwa adabu na kunyoroshwa mpaka atanyooka na kutulia kwenye ndoa!.

P.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Pasco hili bandiko lako akiliona Jussa Makengeza utapigwa marufuku usikanyage Visiwa vya Karafuu ha ha ha.
Mkuu Ngongo, zamani nilikuwa kila nikienda Zenj, hukaa na Jussa for over a cup of tea, huyo ndio mridhi wa Maalim Seif, ila tangu chokochoka zimeanza, nimekuwa simtafuti tena, ili kibinti cha Mzelendo, tunaonana!.
P.
 
Mkuu FJM usisahau tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya ni nusu kwa nusu !.WaTanganyika wako kimya wanakubaliana na upuuuzi !.


Ngongo,

Matokeo ya hii sensa yatasadia sana kujadili Muungano. Kwa kuanzia, tuweke wabunge wa viti maalum pembeni;

Tanganyika kuna majimbo 182, kwa maana hiyo kwa population ya 43,625,434 ni kwamba kila mbunge, on average, atakuwa anawakilisha watu 239,700. Zanzibar na population ya 1,303,568, wana majimbo 50. Hivyo, on average, kila mbunge wa Zanzibar atakuwa anawakilisha watu 26,071!

(Mbunge kama Mnyika anawakilisha majimbo 15 huko Zanzibar!)

Gharama zote za bunge anabeba Tanganyika ambaye anapunjwa kwenye 'representation. Lakini bado watu wanalalamika Zanzibar inanyonywa!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mimi binafsi nawashangaa sana waTanganyika kwanini siku zote wanapata kigugumizi katika kudai Serikali yao ya Tanganyika na kuufanya muungano uwe wa kuchangia kwa kila Serikali.

Lakin vile vile haingii akilini hata siku moja wajumbe wa Tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya huko Tanzania kuwa na wajumbe pasu kwa pasu ukizingatia Znz ina wati 1.2 milion na wenzao majirani zao zaidi ya 47 milioni.

Lakin kwa idadi ya waZnz na uchumi wao inajionyesha wazi wakiachwa pekee yao wana nafasi kubwa sana kiuchumi kutokana na idadi yao kuwa ndogo. hata mimi pamoja na umasikini wangu nina uwezo wa kuwapa milo mitatu kwa siku kwa mwezi mzima. lakin majirani zao mmmh?

kama kutakuwa kuchangia muuungano kuwekwe kutokana na uwiano wa Idadi za watu na hicho kijikite hata misaada na mikopo pia? kwani Znz wanadhulimiwa sana katika hayo.

lakin la mwisho kwanini waTanganyika mnakuwa na kigugumizi sana katika kuujadili na hata kusema bayana nini mtazamo wenu kuhusu huo mvungano wenu. WaZnz wapo wazi wanataka muungano wa mkataba na kama hilo haliwezekani basi kila mtu achukue chake.


LET TANGANYIKA COME and mvungano ufe.
 
Mkuu Mag3, wawakilishi wapo kwa bahati mbaya hakuna mwenye kufikiria nchi kwanza, kila mmoja anafikiria jinsi ya kurudi bungeni next time.

Pili, hizi siasa za uchama nazo zimezidi na kudumaza nchi. Mathalani, haiwezekani mbunge wa CCM kusimama na kuhoji au kuunga mkono hoja inayokinzana na sera za chama chake.
Wenzetu wengine duniani mbunge anakuwa mwakilishi wa watu kwanza kabla ya chama.

Pengine hili nalo linaongeza uzito wa kuwa na wagombea binafsi watakaokuwa na mawazo huru bila kufungwa pingu za vyama.

Umekumbusha kitu muhimu sana katika katiba. Baada ya tetesi za mafuta SMZ imekimbilia BLW na kurekebisha katiba yake inayoeleza Zanzibar na eneo lake ikiwa ni mkakati wa kulinda kile kilichosemwa ni mafuta.
Katika kufanya hivyo walijikuta wanakiuka katiba ya JMT kwakiwango cha hali ya juu sana.

Ndio maana tunasema hivi, ili kuondoa sintofahamu na maruwe ruwe haya ZNZ iliyo na uwezo wa kubadilisha mambo mengi bila kuulizwa ina uwezo wa kuamua hatima yake ndani ya muungano bila kutegemea Tanganyika.

Waarabu tuna usemi KAULI YA VITENDO NI BORA SANA KULIKO KAULI YA MANENO. Kwa hilo utaona waZnz wameonyesha kila dalili za kudai haki zao ndani ya muungano na wapo tayari kwa lolote. Lakin ndugu zao kutoka bara ni wanafiki wakubwa bendera kufuata upepo. Jisahihisheni kwalo na kuwa wawazi na ku speak out kama wafanyavyo waZnz.
 
Waarabu tuna usemi KAULI YA VITENDO NI BORA SANA KULIKO KAULI YA MANENO. Kwa hilo utaona waZnz wameonyesha kila dalili za kudai haki zao ndani ya muungano na wapo tayari kwa lolote. Lakin ndugu zao kutoka bara ni wanafiki wakubwa bendera kufuata upepo. Jisahihisheni kwalo na kuwa wawazi na ku speak out kama wafanyavyo waZnz.
Kama asemavyo seif, matatizo ya muungano ni nafasi za ubalozi! is that what you mean.
Sisi tulishasema mkitaka hewala, hamtaki ondokeni. Kitu kimoja mfahamu mkiwa na Tanganyika hamna mamlaka kamili mtaidshi katika kivuli cha Tanganyika. Mtakuwa na bendera, wimbo wa taifa n.k. lakini mwisho wa yote mtakuwa chini ya kivuli cha Tanganyika, matake msitake. Hiyo ni lazima itatokea
 
Mtakuwa na bendera, wimbo wa taifa n.k. lakini mwisho wa yote mtakuwa chini ya kivuli cha Tanganyika, matake msitake. Hiyo ni lazima itatokea
Na wao bila aibu wanatamba eti "tuna bendera yetu na wimbo wetu" huku wakiendelea kulalama "eti tunapumuliwa!" Kama hamtaki kupumuliwa si muondoke? Kujipitishapitisha ya nini? Watu wazima mnafunga safari, mnavuka bahari hadi Dodoma...kutafuta nini kama si kupumuliwa! Ona sasa, mwishowe mnaanza kupumuliana wenyewe kwa wenyewe! Ama ndio tuelewe nini...mnazuga sio? Wazanzibari bwana, watu wa ajabu kabisa!
 
Duh hizi comments napenda Barubaru na wala urojo wote wazisome kwa umakini kisha wachukue hatua.

Na wao bila aibu wanatamba eti "tuna bendera yetu na wimbo wetu" huku wakiendelea kulalama "eti tunapumuliwa!" Kama hamtaki kupumuliwa si muondoke? Kujipitishapitisha ya nini? Watu wazima mnafunga safari, mnavuka bahari hadi Dodoma...kutafuta nini kama si kupumuliwa! Ona sasa, mwishowe mnaanza kupumuliana wenyewe kwa wenyewe! Ama ndio tuelewe nini...mnazuga sio? Wazanzibari bwana, watu wa ajabu kabisa!
 
Last edited by a moderator:
Duh hizi comments napenda Barubaru na wala urojo wote wazisome kwa umakini kisha wachukue hatua.

Siku zote nasema BORA waZNZ wanaolalamika kuliko waTanganyika ambao WANANUNG'UNIKA. kwani tunaamini hakuna dhambi kubwa kuliko ya mtu anayenung'unika.

Pole sana Ngongo

 
Back
Top Bottom