Uzalendo Tata

Joined
Jul 26, 2022
Posts
14
Reaction score
10
Tafiti zinaonesha tangu mwaka 2015 na kuendelea kumekuwa na ongezeko la wimbi la watu wanaofanya mambo ambayo kwa watu razini ni ujinga uliokomaa lakini mambo hayo yanachukuliwa kama uzalendo?

Kwa mfano kuna kipindi waziri fulani alikuwa akipima samaki na rula lakini kitendo kile kilitafsiriwa ni uzalendo au lipindi fulani aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar aliwapiga marufuku wabunge kutoingia jinini humo jambo lililotafsiriwa kama ni uzalendo.

Je, jamii ya tanzania inajua maana halisi ya uzalendo?
 
Tafsiri rahisi ya uzalendo ni kuwa na mapenzi na nchi yako, mzalendo ni yule mwenye mapenzi na nchi yake, yaani mfia nchi, aliye tayari kutetea nchi yake au kufanya lolote kwa ajili ya nchi yake.

Kuna tofauti kati ya nchi, serikali na taifa, hao unaowasema wewe si wazalendo kwasababu wana mapenzi na serikali, lakini hawana mapenzi na nchi, wana mapenzi na kiongozi wa nchi au kiongozi wa chama lakini si nchi.

Serikali ni kikundi cha watu watawala walipo madarakani kwa muda fulani, wanaweza kuwepo madarakani kwa muda na kisha huondoka(Kwa hiari au lazima) lakini nchi itaendelea kuwepo, hivyo tunapaswa tuwe na uzalendo (mapenzi kwa nchi) na si kwa serikali, Rais au chama.

Wenye mapenzi na serikali, au Kiongozi fulani, au mapenzi na chama fulani hufanya hivyo kwa masilahi yao binafsi na si kwa masilahi ya nchi.

Mifano ya watu uliowataja hapo hawakuwa na uzalendo na nchi yao bali walikuwa vibaraka wa kiongozi fulani au chama fulani au kundi fulani - kwa maslahi yao binafsi na si kwa masilahi ya nchi.
 

ukipata like 15 kwene huu utoporo wako nishtue nije niangalie wajinga
 
Umefafanua vema. Watu wenye kuegemea kwenye itikadi fulani hawawezi kuelewa. 🇹🇿🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…