Uzazi wa mpango ni lazima

Uzazi wa mpango ni lazima

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo Rais wetu Mheshimiwa Samia katutangazia matokeo ya sensa ya watu na makazi.

Ukiitazama vizuri idadi ya watu inavyoongezeka (61 million) na ukuaji wa uchumi ni wazi sasa tunatakiwa kuzalisha zaidi bidhaa mbali mbali kuliko kuzalisha watoto ambao watakuja kuangukia katika lindi la umaskini.

Tuzae watoto ambao tutakuwa na uwezo wa kuwatunza na kuwajengea misingi bora ya elimu.

Ni vyema familia zikapanga uzazi wa mpango ambao utaendana na uwezo wa uchumi na malezi bora.

Ongezeko la idadi ya watu bila ya ukuaji wa uchumi, maendeleo ya sayansi na teknolojia, matokeo yake ni kutengeneza kizazi cha madereva wa boda boda, wauza bar, machinga na wapiga debe.

Naomba kuwasilisha kwa mjadala wenye afya.
 
Shida tuliyonayo upo uvamizi mpya wa kiimani unaopingana na sayansi ya afya na bulldozer wameongezeka ambao wanahimiza ongezeko huru la kuzaliana na kusahau juhudi za uzalishaji bidhaa.

Huduma nafasi za ajira na mifumo ya kisasa kuhudumia, kwa maana ya ukusanyaji taarifa, uchakataji taarifa, utoaji elimu unaoendana na mabadiliko haya pamoja na ukuaji wa uchumi.
 
Hesabu yenye kukaribia ukweli inaweza kupatikana kupitia watendaji wa vijiji/ mitaa na kata.

Hii sensa ya siku/wiki moja ikiwa Pamoja na utamaduni wa kumaliza haraka bila uhakiki yaweza kuwa na mapungufu yake.

Hata hivyo, ndiyo takwimu rasmi ya serikali kwa sasa, lazima itumike.
 
Hesabu yenye kukaribia ukweli inaweza kupatikana kupitia watendaji wa vijiji/mitaa na kata.
Hii sensa ya siku/wiki moja ikiwa Pamoja na utamaduni wa kumaliza haraka bila uhakiki yaweza kuwa na mapungufu yake.
Hata hivyo, ndiyo takwimu rasmi ya serikali kwa sasa, lazima itumike.
Kwa mtazamo wako hesabu ndogo au kubwa?
 
TheStoryTimeFacts [emoji310]
Habari [emoji112]
Naitwa Erry Mars ni msimuliaji wa Historia,makala na simulizi
Nathamini sana mchango wako ndugu [emoji120],Naomba support yako nisaidie ku SUBSCRIBE na kugusa KENGELE kwenye channel yangu.[emoji120]
Link Bonyeza Hapa[emoji116]



Asante sana [emoji120]

Oyaa usini-quote kwny mambo ya kikumar.
 
Vipofu hatuoni nyota Babu😂
Zuberi na Zubeda wamepishana miezi Michache..... Afrika eeeh
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo Rais wetu Mheshimiwa Samia katutangazia matokeo ya sensa ya watu na makazi.

Ukiitazama vizuri idadi ya watu inavyoongezeka (61 million) na ukuaji wa uchumi ni wazi sasa tunatakiwa kuzalisha zaidi bidhaa mbali mbali kuliko kuzalisha watoto ambao watakuja kuangukia katika lindi la umaskini.

Tuzae watoto ambao tutakuwa na uwezo wa kuwatunza na kuwajengea misingi bora ya elimu.

Ni vyema familia zikapanga uzazi wa mpango ambao utaendana na uwezo wa uchumi na malezi bora.

Ongezeko la idadi ya watu bila ya ukuaji wa uchumi,maendeleo ya science & technology matokeo yake ni kengeneza kizazi ya madereva wa boda boda,wauza bar,machinga na wapiga debe.

Naomba kuwasilisha kwa mjadala wenye afya.
Kati ya vitu vya msingi ambavyo nilitegemea Mh. Rais angechana live pale pale uwanjani ni hilo la ongezeko la watu lisilowiana na uchumi na kufuta rasmi kauli ya fyatueni Serikali italea. Hakufanya hivyo; fursa nyingine adhimu imepotea bure.
 
Kati ya vitu vya msingi ambavyo nilitegemea Mh. Rais angechana live pale pale uwanjani ni hilo la ongezeko la watu lisilowiana na uchumi na kufuta rasmi kauli ya fyatueni Serikali italea. Hakufanya hivyo; fursa nyingine adhimu imepotea bure.
Waislam hatuna huo ushenzi, sisi ni kuzaana tu Kila mtu anakuja na shani yake
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Leo Rais wetu Mheshimiwa Samia katutangazia matokeo ya sensa ya watu na makazi.

Ukiitazama vizuri idadi ya watu inavyoongezeka (61 million) na ukuaji wa uchumi ni wazi sasa tunatakiwa kuzalisha zaidi bidhaa mbali mbali kuliko kuzalisha watoto ambao watakuja kuangukia katika lindi la umaskini.

Tuzae watoto ambao tutakuwa na uwezo wa kuwatunza na kuwajengea misingi bora ya elimu.

Ni vyema familia zikapanga uzazi wa mpango ambao utaendana na uwezo wa uchumi na malezi bora.

Ongezeko la idadi ya watu bila ya ukuaji wa uchumi,maendeleo ya science & technology matokeo yake ni kengeneza kizazi ya madereva wa boda boda,wauza bar,machinga na wapiga debe.

Naomba kuwasilisha kwa mjadala wenye afya.
Kimsingi ni kwamba Tanzania Hakuna ajira kabisa
 
Watanzania wataenda kuwa kama Wanigeria, kila kona ya dunia wapo wanasaka fursa. Nyumbani njaa.
 
Kati ya vitu vya msingi ambavyo nilitegemea Mh. Rais angechana live pale pale uwanjani ni hilo la ongezeko la watu lisilowiana na uchumi na kufuta rasmi kauli ya fyatueni Serikali italea. Hakufanya hivyo; fursa nyingine adhimu imepotea bure.
Bora alivyonyamaza kimya
 
Ukiitazama vizuri idadi ya watu inavyoongezeka (61 million) na ukuaji wa uchumi ni wazi sasa tunatakiwa kuzalisha zaidi bidhaa mbali mbali kuliko kuzalisha watoto ambao watakuja kuangukia katika lindi la umaskini.
Nadharia potofu.
Vipi ungehimiza watu kufanya kazi kuongeza pato, na viongozi kutotapanya mali za nchi hii ili ziwafaidie wananchi wake isingeeleweka?

Utajiri wote huu ndani ya nchi iliyobarikiwa kila kitu isipokuwa akili kichwani mwa viongozi wake, unalia na idadi ya watu 60 milioni?
 
Ushamba wa kuzaa kama sifa upo huku tu nchi zinazo jitambua ukizaa wengi mwisho 2 tu na uwezo wa maisha wanao huku mtu anazaa kama analipwa mshahara mwisho wa siku wanakimbia familia zao au wanaacha watoto wajilee.
 
Nadharia potofu.
Vipi ungehimiza watu kufanya kazi kuongeza pato, na viongozi kutotapanya mali za nchi hii ili ziwafaidie wananchi wake isingeeleweka?

Utajiri wote huu ndani ya nchi iliyobarikiwa kila kitu isipokuwa akili kichwani mwa viongozi wake, unalia na idadi ya watu 60 milioni?

Mama Lishe unazaa watoto wanne kipato chako cha kudunduliza halafu unataka Serekali ikujengee matundu ya choo.

Ukweli mchungu tuanzishe familia ambazo tunaweza kuzihudumia vizuri wenyewe badala ya kila kitu kukimbilia msaada wa Serekali.

Last week nilikuwa Dar nikabaki kushangaa jinsi usafiri wa Mwendokasi ulivyozidiwa na idadi ya watu.Kifupi nilishuhudia msongamano mkubwa wa watu sijapata kuona.Ukienda katika vituo vya afya hali ni hiyo hiyo,ukuchungulia sekta ya Elimu kila mwaka madarasa yanajengwa madawati hayatoshi darasa moja wanafunzi 100 badala ya wanafunzi 45.

Kila Niki Tazama Tanganyika nabaki na mshangao
 
Mama Lishe unazaa watoto wanne kipato chako cha kudunduliza halafu unataka Serekali ikujengee matundu ya choo.

Ukweli mchungu tuanzishe familia ambazo tunaweza kuzihudumia vizuri wenyewe badala ya kila kitu kukimbilia msaada wa Serekali.

Last week nilikuwa Dar nikabaki kushangaa jinsi usafiri wa Mwendokasi ulivyozidiwa na idadi ya watu.Kifupi nilishuhudia msongamano mkubwa wa watu sijapata kuona.Ukienda katika vituo vya afya hali ni hiyo hiyo,ukuchungulia sekta ya Elimu kila mwaka madarasa yanajengwa madawati hayatoshi darasa moja wanafunzi 100 badala ya wanafunzi 45.

Kila Niki Tazama Tanganyika nabaki na mshangao
Wapi hapo ulishangaa watu kujazana mwendokasi [emoji23][emoji23]
Mwendokasi za mbagala nazionea huruma mana zitajaza sanaaaaa

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Kwa mtazamo wako hesabu ndogo au kubwa?
Kuna uwezekano ni kubwa baadhi ya maeneo.
Kulingana na teknolojia ya mawasiliano, dunia imekuwa kama Kijiji na nchi zimekuwa kama mitaa, hakuna sababu ya kufanya sensa za projection (hesabu ni tatizo kwa watu wetu, wanaweza kuandika namba yoyote bila kujua impact yake).
Inawezekana kabisa kusajili watu kwa asilimia kubwa hivyo kupata ukweli hata kama kazi hiyo itafanywa mwaka mzima kupitia ofisi za serikali.
Watumishi wale wale wa serikali watoe taarifa, kuanzia shina, mtaa/Kijiji, kata na wilaya (hapa uhakiki waweza kufanyika mara kwa mara).
Changamoto ni elimu za kukariri, kuanzia zamani.
NIDA yenyewe yaweza kutumika kujua idadi ya watu.
 
Back
Top Bottom