Uzazi wa mpango ni suluhu ya matatizo mengi ikiwemo umachinga uliokithiri

Uzazi wa mpango ni suluhu ya matatizo mengi ikiwemo umachinga uliokithiri

Tanzania tuna tatizo la kuchagua ajira Tuna ardhi ya kutosha watu hawataki kulima na kufuga
Ajira hamn mtu anachagua aisee! Mitaji ndio ishu huko kulima ambako hujui unamuuzia nani nalo ni swala jingine!

Unalima kwa nguvu ukifika sokoni mmakuta wakulima mmejazana mazao hayana faida! Kama ni mali kuoza unauza kwa hasara tu ili kiishe.

Nani atafurahia kilimo cha aina hio? Raha ya kulima upeleke mazao sehemu husika ukabidhiwe chako mapema uendelee na mishe zingine! Peleka mazao ghalani gunia zako 10 unalipwa cash yako yenye faida nzuri unatembea.

Hiki kilimo cha kuanza kuviziana masokoni na madalali hakina maana wala tija! Uteseke kulima halafu ukifika sokoni dalali anataka ale 40% ya faida wewe uliyeteseka uambulie 60%! Hapo bado hujadhulumiwa!

System ya kilimo ki bongobongo haiko stable wenzetu wa Kenya wamejitahidi ku brand produce zao duniani wanauza direct ulaya huko! Wanakuja kulangua kwetu kwa bei nafuu wao wanauza kwa super profits ulaya!

Wamewezaje kushawishi wazungu wanunue bidhaa zao sisi tunashindwa nini ku standardize kilimo chetu kiwe cha kibiashara? Arable land ipo ila watu hawana time na kilimo sababu kinazalisha hasara kwa watu wasio na mitaji! Serikali inachoweza ni kutumia billion 27 kujenga AC za mtaani dodoma eti hali ya hewa ku maintain!

Mara elfu uwe mchuuzi wa mazao ila sio kilimo bongo kama huna mtaji wa maana!
 
ili uwe na watoto wenye future nzuri lazma nawe uwe na future nzuri kwanza!......nakusalimia sana mkuuu
Yeah ukitaka kuamini hilo angalia familia ya Jakaya Mrisho Kikwete na familia ya Muhidin Ngurumo.

Unategemea Khalfan anaweza kuwa mmachinga? Au vijana wote waliozaliwa nje ya ndoa kama mtoto wa Odama yule anaweza kuwa machinga eti sababu anamaliza chuo mwaka 2030? Baba ana utajiri na connection wakati wewe unasoma kwa mkopo umalize degree yako kwa tabu urudi kuzagaa mtaani mwenzio sahizi anasoma shule ya ada 10M kwa mwaka na akimaliza katika chuo hicho hicho ulichomaliza wewe yeye haendi kuzagaa mtaani maana cha kufanya kipo tayari anachagua tu kama ajira au biashara! Mzee analima mapapai for fun sababu kazeeka analima kama hobby tu ya wazee ila mapapai yake ana export yale haendi kupatana na madalali ilala boma au kariakoo shimoni sasa we kurupuka ulime mapapai uone kitakachokupata.

Mhidin Ngurumo yuko majalala licha ya kuwa mpiga tumba na gitaa maarufu tu ila familia yake na watoto lazma waishie kuwa masakara tu na si kwa kupenda ila aliyetoboa sana unaweza kuta ni dereva wa serikalini huko! Wengine unga unga mwana sababu mzee pia hakuwa na finances za maana!
 
Ajira hamn mtu anachagua aisee! Mitaji ndio ishu huko kulima ambako hujui unamuuzia nani nalo ni swala jingine!

Unalima kwa nguvu ukifika sokoni mmakuta wakulima mmejazana mazao hayana faida! Kama ni mali kuoza unauza kwa hasara tu ili kiishe.

Nani atafurahia kilimo cha aina hio? Raha ya kulima upeleke mazao sehemu husika ukabidhiwe chako mapema uendelee na mishe zingine! Peleka mazao ghalani gunia zako 10 unalipwa cash yako yenye faida nzuri unatembea.

Hiki kilimo cha kuanza kuviziana masokoni na madalali hakina maana wala tija! Uteseke kulima halafu ukifika sokoni dalali anataka ale 40% ya faida wewe uliyeteseka uambulie 60%! Hapo bado hujadhulumiwa!

System ya kilimo ki bongobongo haiko stable wenzetu wa Kenya wamejitahidi ku brand produce zao duniani wanauza direct ulaya huko! Wanakuja kulangua kwetu kwa bei nafuu wao wanauza kwa super profits ulaya!

Wamewezaje kushawishi wazungu wanunue bidhaa zao sisi tunashindwa nini ku standardize kilimo chetu kiwe cha kibiashara? Arable land ipo ila watu hawana time na kilimo sababu kinazalisha hasara kwa watu wasio na mitaji! Serikali inachoweza ni kutumia billion 27 kujenga AC za mtaani dodoma eti hali ya hewa ku maintain!

Mara elfu uwe mchuuzi wa mazao ila sio kilimo bongo kama huna mtaji wa maana!
Kilimo ni janga. Ni maneno tu, kilimo kwanza, siasa ni kilimo, uti wa mgongo, cha kufa na kupona nk. Ajabu kauli zote hizi hazilengi tatizo kuu la kilimo, bei ya mazao na masoko. Mpe mtu auze kokote kwenye bei nzuri. Vunja huu wizi unaitwa ushirika. Mtu alime kahawa au chai na auze kwa amtakae. Alime mahindi auze kwa amtakae na anakotaka. Mti akilima maharage na akitaka kuuza South, akauze. Hapo ndiyo kilimo kitakuwa, watu ndipo watakimbilia kulima. Hapo ndiyo matajiri wenye mitaji watalima.
 
Japan na Korea ni nchi tofauti sana na sisi kiuchumi, hizo ni nchi za viwanda adimu sisi ni nchi ya kilimo. Hizi ni nchi ambazo chumi zake zinazalisha bidhaa adimu (zinazozalishwa na nchi chache) kwa ajili ya soko la dunia nzima (magari, electronics, mashine, nguo n.k).

Uchumi wetu sisi ni uchumi ambao ni kwa ajili yetu huku ndani zaidi na utabaki hivyo kwa muda mrefu sana kwa sababu bidhaa tunazozalisha ambazo ni za kilimo na ndio sekta kubwa kuliko zote sio bidhaa tofauti au adimu sana na za majirani zetu wote wanaoutuzungaka na bara zima kwa ujumla.
Nchi kama DRC Congo ikija kuamka ina uwezo wa kulisha bara zima la Africa na sisi tukakosa mahali pa kuuzia mazao yetu kabisa

Hivyo hata tukiweza kuendeleza kilimo na ufugaji kwa kiwango cha kisasa cha juu kabisa bado soko letu kubwa tutagemea la huku ndani na lazima ipo siku litazidiwa, likizidiwa sekta itapunguza ukuaji wake na ajira nyingi zitatoweka hivyo tutarudi kule tulipotoka kwenye tatizo la ajira. Kwa hiyo wakati tunakomaa kupata uchumi imara lazima pia tupambane na ongezeko holela la watu kwa sababu aina ya uchumi wetu.
Serikali ikiwa na mipango na sera za kiuchumi itatumudu hata mara nne ya ifadi tulivyo sasa.

Japan ni ndogo sana ukilinganisha na sisi, lakini ina watu zaidi ya 120m. Korea Kusini tunalingana idadi ya watu lakini kwa ukubwa inaingia kama mara tisa kwetu. Lakini wao wanaishi vizuri kuliko wao. Na hizi nchi, Japan na Korea idadi kubwa sana ya watu ni wazee ambao hawazalishi bali wanatumi. Sisi average ya umri ni kama miaka 18 hivi, bado nguvu nyingi sana.

Serikali ni ya kulaumiwa kwa asilimia 100. Hatujafika idadi ya kuanza kupanga uzazi, ni uzembe tu.
 
Kuna mahali nimesema watoto wauwae?
Hiyo misemo ya kila mtoto anakuja na sahani yake ni potofu, haina ukweli wowote wala nafasi katika dunia ya leo. Watoto wanatikiwa wakute sahani zao zilizoandaliwa tayari na wanaowazaa.
Katika Quran mwenyezi mungu anasema.msiue watoto wenu kwa kuhofia RIZIKI.
Yeye ndiye anayetoa RIZIKI
 
Siyo kweli...

Wamachinga hata nchi zilizendelea wapo...
Mfumo ndiyo mbovu...
 
umewaza kama RC dsm na RAIS wake,kuona kwamba wamachina ni uchafu jiji na si watafutaji wa maisha.
 
Wengi wanachukulia poa aina ya familia mtu anayotoka katika suala la kutoboa. Ila ukweli ni kwamba kama hutoki kwenye famili yenye ukwasi na koneksheni nyingi ni vigumu sana kutoboa na kufika mbali .Ni rahisi zaidi kuelekea kwenye umachinga na mama ntilie usipotoka familia bora.

Wachache wanaotoboa kutoka familia duni ni kwa jasho, machozi, damu na hata kujikomba sana kwa wenye nazo.Ni muhimu sana kuangalia watoto tunaowazaa tutawapa maisha ya aina gani watoboe na wataishia wapi inatokana kwa kiasi kikubwa na mchango wa wazazi.
Yeah ukitaka kuamini hilo angalia familia ya Jakaya Mrisho Kikwete na familia ya Muhidin Ngurumo.

Unategemea Khalfan anaweza kuwa mmachinga? Au vijana wote waliozaliwa nje ya ndoa kama mtoto wa Odama yule anaweza kuwa machinga eti sababu anamaliza chuo mwaka 2030? Baba ana utajiri na connection wakati wewe unasoma kwa mkopo umalize degree yako kwa tabu urudi kuzagaa mtaani mwenzio sahizi anasoma shule ya ada 10M kwa mwaka na akimaliza katika chuo hicho hicho ulichomaliza wewe yeye haendi kuzagaa mtaani maana cha kufanya kipo tayari anachagua tu kama ajira au biashara! Mzee analima mapapai for fun sababu kazeeka analima kama hobby tu ya wazee ila mapapai yake ana export yale haendi kupatana na madalali ilala boma au kariakoo shimoni sasa we kurupuka ulime mapapai uone kitakachokupata.

Mhidin Ngurumo yuko majalala licha ya kuwa mpiga tumba na gitaa maarufu tu ila familia yake na watoto lazma waishie kuwa masakara tu na si kwa kupenda ila aliyetoboa sana unaweza kuta ni dereva wa serikalini huko! Wengine unga unga mwana sababu mzee pia hakuwa na finances za maana!
 
Binadamu yoyote tofauti na wanyama ili aweze kukua vizuri, apate maendeleo na astawi anahitaji msaada, uangalizi na muongozo wa muda mrefu wa wazazi, familia, ndugu, marafiki, majirani na Serikali.

Anahitaji apatiwe chakula bora, mavazi bora, makazi, na elimu bora tangu akiwa mdogo hadi angalau miaka 18. Akimaliza masomo yake anahitaji apewe mazingira mazuri/awezeshwe kujipatia kipato kupitia kazi za hadhi nzuri "decent jobs". Wenye jukumu hili ni Familia yake na Serikali. Wanaposhindwa kutimiza jukumu hilo ndipo tunaona taifa likizalisha vijana lukuki ambao ni wamachinga, wauza pipi na maji barabarani, bodaboda na mama ntilie wanaopikia kuni katikati ya majiji.

Lawama nyingi zinaelekezwa serikalini kunapoteka matatizo yanayohusu kufuata utaratibu kwa makundi haya lakini ni vyema tujikite katika chanzo cha tatizo ambacho ni 1.sera za kiuchumi zilizoshindwa kufungua sekta za uchumi mkubwa wa viwanda, kilimo na huduma 2.Kupuuza uzazi wa mpango kwa raia wengi. Ni lazima sote tukubali zama za kuzaa rundo la watoto ambao hujui hatma yao watakapofikisha miaka 20 zimepitwa na wakati.Hizi na zama za kuwa na watoto ukiwa na mpango kichwani wa jinsi gani watoto hao hawataishia kuwa makabwela wanaotanga tanga.
😍
 
Wengi wanachukulia poa aina ya familia mtu anayotoka katika suala la kutoboa. Ila ukweli ni kwamba kama hutoki kwenye famili yenye ukwasi na koneksheni nyingi ni vigumu sana kutoboa na kufika mbali .Ni rahisi zaidi kuelekea kwenye umachinga na mama ntilie usipotoka familia bora.

Wachache wanaotoboa kutoka familia duni ni kwa jasho, machozi, damu na hata kujikomba sana kwa wenye nazo.Ni muhimu sana kuangalia watoto tunaowazaa tutawapa maisha ya aina gani watoboe na wataishia wapi inatokana kwa kiasi kikubwa na mchango wa wazazi.
UKWELI MTUPU 😍
 
An optimum Productive Population...

Sio vema mtu ufyatue watoto ukitegemea jamii ikusaidie kulea (ni vema uwe responsible)
Sio vema kwa taifa kushindwa kutumia nguvukazi kwa kushindwa kuwawezesha / kuwapa fursa nguvukazi hio kupata kipato.

Watu ni rasilimali (ingawa wakizidi ni tatizo) ila watu hao lazima wawe productive. (Kuna kipindi China watu walizidi ilibidi waweke idadi ya watoto) ingawa wingi wao kwa sasa watu wanaotolea macho sababu ni soko kubwa vilevile..

Tanzania bado haijajaa; Ingawa ni obligation ya mzazi kuwa na familia kadri ya uwezo wake.... Tatizo la Umachinga / Masikini litamalizwa na Machinga / Masikini wenyewe....

 
Mwakani 2022 ni SENSA ya WATU na MAKAZI.....

Lengo lake ni kuijua idadi yetu na kuweka vipaumbele vya maendeleo....

Ikiwa serikali inahitaji kuweka mikakati MADHUBUTI... Cha ajabu anatokea mwananchi tena humu mijini.......kutokea pande za USWAZI analegalega kuiweka mipango ya kifamilia kwa kusema kila mtoto anakuja na RIZIKI YAKE......


"HEAVEN OR HELL by Meek Mill & Jada Kiss"
 
Umeongea jambo la maana sana mkuu binafsi nimekuelewa

Tusiangalie tumeangukia wapi,bali tulipojikwaa

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Kwenye Utawala Wangu Zaeni Hakuna Kupanga Uzazi
Waziri Wa Afya Umenisikia Vizuri Najua Hupendi
Sasa Hivi Elimu Ni Bure, Hata China Na India Zimeendelea Kwa Kuwa Na Watu Wengi Sana

Ngojeni Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Mwingine Ndiyo Mpange Uzazi

By Jiwe
 
Kama wewe ni maskini, fukara au mfanyakazi wa ngazi ya chini ukizaa watoto 5 kuna uwezekano mkubwa watatu wakaishia kuwa wamachinga na waendesha bodaboda na hao wawili ndio wakapata kazi au kufanya biashara ya maana. Uamuzi ni wako.
Tatizo lako naona unachukulia hii issue kama kucheza kamari; "ukizaa watano, watatu wawe machinga na bodaboda, na wengine ndio wafanikiwe"

Unaweza zaa mmoja huyo huyo akawa bodaboda, au ukazaa wawili wote wakawa bodaboda na machinga, pale ambapo ajira zinatoka kwa kuajuana uta-guarantee vipi uhakika wa mwanao kuipata hata kama ana elimu?

Narudia tena, uzazi wa mpango sio kigezo/uhakika wa kupata ajira kwa kijana wa kitanzania asie na connection.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kuna watu walimuamini na wakafyatua kweri kweri!
Kwenye Utawala Wangu Zaeni Hakuna Kupanga Uzazi
Waziri Wa Afya Umenisikia Vizuri Najua Hupendi
Sasa Hivi Elimu Ni Bure, Hata China Na India Zimeendelea Kwa Kuwa Na Watu Wengi Sana

Ngojeni Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Mwingine Ndiyo Mpange Uzazi

By Jiwe
 
Back
Top Bottom