Kwema.
Kwanza, baada ya kujifunga mara nyingi huchelewa kuona siku zake (wengine hupitisha hata zaidi ya miezi mitano), urefu wa kipindi cha kutoona siku hutofautiana baina ya mwanamke na mwanamke.
Hili sio tatizo ila ni namna ya mwili kurudi katika hali yake ya kawaida (normal physiology).
Licha yakua mwanamke kutoona siku zake mara tu baada ya kujifungua sio tatizo hii pia ni NJIA YA UZAZI WA MPANGO kwa njia za asili (natural methods) kwa kitaalam inifahamika kama Lactational Amenorrhea, kwenye kipindi hiki mwanamke anapokua ananyonyesha.
Hivyo basi ili njia hii ya uzazi iweze kufanya kazi kwa kiwango kikubwa mwanamke anatakiwa kufuata taratibu fulani za kitaalam ikiwa ni pamoja na Kumyonyesha mtoto maziwa tu bila kuchanganya na vyakula vingine.
Asante na Karibu.