Uzee umekuja ghafla kwenye maisha yangu

Uzee umekuja ghafla kwenye maisha yangu

zipumbovu

Member
Joined
Nov 27, 2023
Posts
22
Reaction score
344
Habari wakuu natumaini muko vizuri.

Maisha yangu yanaendelea kunishangaza kila siku kuhusu nyakati zangu, Nimekuwa nikiishi kama kijana mdogo wa kawaida lakini kumbe jamii hainioni kuwa ni kijana mdogo bali inaniona ni Mtu anaefukuzia uzee.

Nilizoea kupewa shkamoo na watoto wadogo lakini sasa napewa shkamoo na vijana wakubwa tuu ambao Mimi nilihisi pengine tuko sawa. Mwanzo walikuwa ni vijana wakubwa wachache lakini saizi ni vijana wengi sana wakubwa wananipa shkamoo, wengine wananiita baba kabisa.

Siku Moja ndio nilishangaa kabisa pale nilipotaka kujipatia kamchepuko majibu yake yakaniacho hoi "kalisema lakini wewe mbona kama baba yangu tuu "

Uzee umepiga hodi kwenye maisha yangu na Bado hata sikujipanga vizuri kuupokea.

NB: MWENZAKO AKINYOLEWA ZAKO TIA MAJI
 
Habari wakuu natumaini muko vizuri.

Maisha yangu yanaendelea kunishangaza kila siku kuhusu nyakati zangu, Nimekuwa nikiishi kama kijana mdogo wa kawaida lakini kumbe jamii hainioni kuwa ni kijana mdogo bali inaniona ni Mtu anae fukuzia uzee.

Nilizoea kupewa shkamoo na watoto wadogo lakini sasa napewa shkamoo na vijana wakubwa tuu ambao Mimi nilihisi pengine tuko sawa. Mwanzo walikuwa ni vijana wakubwa wachache lakini saizi ni vijana wengi sana wakubwa wananipa shkamoo, wengine wananiita baba kabisa.
Siku Moja ndio nilishangaa kabisa pale nilipotaka kujipatia kamchepuko majibu yake yakaniacho hoi "kalisema lakini wewe mbona kama baba yangu tuu "

Uzee umepiga hodi kwenye maisha yangu na Bado hata sikujipanga vizuri kuupokea.

NB: MWENZAKO AKINYOLEWA ZAKO TIA MAJI
Tuanze na umri wako halisi kwanza,
Umefika 40?
 
Nilianzwa kuitwa babu nikiwa na miaka 27 h, ivi mpaka leo sijui ni sura au haiba ( personality) yangu tuu.
Sasa nina umri aliokuwa nao Michael Jackson lakini mtu anaweza dhani ni sawa na baba yake.
Uzee haukwepeki ila nilitaka mchepuko mdogo mdogo nanunua Ubungo External au Sinza na Kimboka Bar Buguruni 😁
 
Waliosoma huu uzi huku wakionea aibu cm zao kama mimi tujuane. Ila pia umeajua kuandika kwa Uandishi wa kisanaa. Nitashangaa kama wewe ni pure mathematician.

Mungu akubariki lango hili la leo umetukamata kwa uwazi na Kweli.

Ila ninachokushauri ishi maisha kama mtoto uzee utakimbia mbio za Hosean Bolt. 🙌🙏
 
Back
Top Bottom