Uzi maalum: Aina mbalimbali za wateja wa ajabu ajabu maofisini na madukani

Uzi maalum: Aina mbalimbali za wateja wa ajabu ajabu maofisini na madukani

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Ingawa Wahenga waliwahi kusema kuwa Mteja ni Mfalme au Malkia!

Lakini Baadhi ya wateja maofisini na madukani huwa ni vichomi na vichefuchefu wakubwa!

Ukiachilia mbali baadhi ya watoa huduma kuwa chanzo cha kuchangia ukorofi wa wateja wao!

Zipo tabia mbali mbali za wateja wasumbufu kwa watoa huduma either kwa kujua ama kutokujua!

Tabia hizo za wateja husababisha watoa huduma kukereka, kukosa ari ya kazi au kufukuzwa/ kufunga kazi mapema!

Hapa nimekusogezea baadhi tu ya tabia za wateja zinazokera watoa huduma.
  1. Wateja wanafika ofisini au dukani wakiwa na majibu yao tayari; Wateja wa namna hii humpa tabu sana mtoa huduma kumuelewesha mteja hata wasifikie muafaka mzuri
  2. Wateja wanaojifanya Staff; Hawa ni sampuli ya wateja wanaojifanya ni wadau katika ofisi husika lakini hawajui A wala Z ya namna huduma wanayohitaji inavyotolewa kiasi cha kuzalisha usumbufu.
  3. Wateja wanaokuja kwa mikwara ya vyeo au kazi zao wanazofanya; Hii ni sampuli ya wateja wanaopenda huduma kwa migongo ya taasisi zao, Hufikia hata kuvaa gwanda zao ili imradi tu mtoa huduma aelewe wao ni kina nani, mbaya zaidi humlazimisha hata mtoa huduma asifuate taratibu halali ili wao wapate kwanza.
  4. Wateja wapelelezi; Hawa ni wale wateja wenye kutaka kujua kila kitu hata kama hawafaidiki nacho kwa wakati huo, Pasipo kujali foleni ya watu nyuma hutumia mda mwingi kwa mtoa huduma kuuliza kila kitu na ahadi lukuki, pia hupenda kurekodi rekodi watu kishamba.
  5. Wateja watongozaji; Hii sampuli nayo haivumi lakini imo, ni wateja wenye uwezo mkubwa sana wa kumzoea mtoa huduma kwa mda mfupi, hutumia mgongo wa customers care kupenyeza maombi yao ya ngono!
  6. Wateja wa ukabila na ukada! Hawa ni aina ya wateja ambao kila kitu wanataka kutumia ukabila au uchama ili kumlainisha mtoa huduma
  7. Wateja wapenda magumashi na njia za panya lakini hutaka risiti original; Dizaini hii ya wateja ni wale wanaopenda kupewa huduma kupitia mlango wa nyuma ili kurahisisha lakini hugeuka nongwa punde baada ya kuanza (Umbeya) kusimulia watu mbalimbali vile walivyopatiwa huduma kinyume na utaratibu kiasi cha kuhatarisha kazi za mtoa huduma.
  8. Wateja wendawazimu; Hawa ni wale wateja wanaofokea kila mtu hata kwa jambo dogo, wateja hawa hupenda kutoa mikwara na vitisho wakati mwingine kwa lugha chafu, ilihali wao hawapendi kujibiwa mbovu!
Kama kuna tabia zingine mbovu nimesahau hapo ongezea tuelimishane!
 
Kauli ya kusema "mteja ni mfalme" siku hizi inatumika vibaya sana.

Mi hua namjibu mteja kulingana na anavyohoji. Ukizingua kula kona maana sijakugongea mlango uje ofisini kwangu
 
Mteja namba 5 fafanua ni jinsia zote?
Jinsia zote mkuu! Wapo wa kike na wengine wa kiume! Ukitaka kujua zaidi waulize bodaboda wanavyopata tabu na baadhi ya wateja wa kike
 
Kauli ya kusema "mteja ni mfalme" siku hizi inatumika vibaya sana.

Mi hua namjibu mteja kulingana na anavyohoji. Ukizingua kula kona maana sijakugongea mlango uje ofisini kwangu
Vipi kama ofisi ni ya Umma
 
Vipi kama ofisi ni ua Umma
Kivyovyote vile hata kama ni ofisi ya mtu na nimepewa sheria ya kuwa handle wateja na mi binafsi nakua na principles zangu. Na kwa bahati mbaya ni kwamba sheria zangu nazipa kipaumbele cha kwanza kuliko hizo za muajiri

Sasa inapotokea mteja kaleta noma ambayo iko kinyume na taratibu zangu hua sina excuse, sijali kama kuna sheria ya muajiri inanishauri kuvumilia hali hiyo bila kumuonesha mteja kua nimekasirishwa
 
Kivyovyote vile hata kama ni ofisi ya mtu na nimepewa sheria ya kuwa handle wateja na mi binafsi nakua na principles zangu. Na kwa bahati mbaya ni kwamba sheria zangu nazipa kipaumbele cha kwanza kuliko hizo za muajiri

Sasa inapotokea mteja kaleta noma ambayo iko kinyume na taratibu zangu hua sina excuse, sijali kama kuna sheria ya muajiri inanishauri kuvumilia hali hiyo bila kumuonesha mteja kua nimekasirishwa
Hahah
 
Huwa wanatia hasira sana.....Kuna mmoja alikuja kuchagua viatu alijaribu kila kiatu na vikamtosha,utasikia embu hicho....unamshushia embu hicho unampatia Kama nususaa then ananiambia atakuja siku nyingine mamaaeee nilitaka kumtoa meno
 
Huwa wanatia hasira sana.....Kuna mmoja alikuja kuchagua viatu alijaribu kila kiatu na vikamtosha,utasikia embu hicho....unamshushia embu hicho unampatia Kama nususaa then ananiambia atakuja siku nyingine mamaaeee nilitaka kumtoa meno
Hahahah
 
Kuna watoa huduma nao wanakera Sana, hasa usipokuwa frequent customer utalazimika tu kuonekana mteja msumbufu.
 
Kuna Hawa wateja
Wanaokuja KUKOPA na kuanza na Kujisifia kwako wanavokopeshwaga maduka mengine wanayouza bidhaa ile ile.

Utaskia
"Mi nkiendaga kwa JOHN ananikopaga bila kujiuliza mara mbili,Wee niamini tu ntakurejeshea"

Mteja anatumia mbinu ya kukutishia ili uogope ili umkope kwa lazima asiende duka jingine.

Kiukweli,
Hapo Uvumilivu huwa unanishinda kabisa
 
Kuna Hawa wateja wanaojifanya MUCH KNOW.

Utawaskia wanasema,
"Hii KEBO YA TRONIC Bei elfu 15 unapiga Sana, Kariakoo wanauza buku 5 unatupiga sana Boss"

WANAKERA SANA, wakati iyo Bei hata ununue jumla kontena 10 bado hutauziwa 5,000@pc.
 
Kuna Hawa wateja,
Wamenunua kwako, Unawapa bonus ya nyongeza ya bidhaa nyingine ya nyongeza.

Iyo bidhaa ya nyongeza baada ya mwezi/wiki inasumbua au inapata hitilafu.

Mteja anarudi anafoka anataka kubadilishiwa au kupewa mpya utadhani aliilipia Ela au ilkua under warranty.
 
Kuna wateja,
Wanakuja dukan anatest Kila bidhaa mpaka bidhaa inachakaa au inaharibika ikiwa dukan
 
Kuna mteja anachagua bidhaa, unamwambia Bei Ni laki 1, anasema Haina shida anakwambia funga kabisa.

Anachomoa burungutu la million 2, anazitoa zote ili uzione Kisha anachomoa elfu 30 anakwambia chukua iyo Ela. nyingine mwisho wa mwezi.

Afu anakukufokea upokee izo Ela kwa lazima.[emoji3525]
 
Kuna Hawa wateja
Wanaokuja KUKOPA na kuanza na Kujisifia kwako wanavokopeshwaga maduka mengine wanayouza bidhaa ile ile.

Utaskia
"Mi nkiendaga kwa JOHN ananikopaga bila kujiuliza mara mbili,Wee niamini tu ntakurejeshea"

Mteja anatumia mbinu ya kukutishia ili uogope ili umkope kwa lazima asiende duka jingine.

Kiukweli,
Hapo Uvumilivu huwa unanishinda kabisa
Unatakiwa ujiulize kwanini hajaenda kwa Yuleyule JOHN anakuja kwako JOSEPH
 
Back
Top Bottom