Uzi maalum kwa tuliowahi kuibiwa simu.

Uzi maalum kwa tuliowahi kuibiwa simu.

Bac mkuu ni vitu hvyo dell na Samsung haya matablet makubwa na kwenye pc Kuna vdude vya mantrac cat
 
nipo kwenye daladala naelekea buguruni njia ya vingunguti jamaa kaingiza mkono kaamsha na tecno yangu usiku nashuka manyoya jamaa keshaingia mitaani nilikua frustated na full kutoamini [emoji23][emoji23]
 
sito kuja sahau nilipo ibiwa simu yangu nikiwa nadaka nguo za mtumba, kumbe wahuni walisha niibia kitambo.


washikaji zangu walipo niuliza simu yako ipo wapi? Niliwajibu nimeamua kuiuza ili kuficha aibu ya kuibiwa maana nilikuwa nawachekaga sana wanao ibiwa simu.niliamua kuwadanganya tu maana ilikuwa hakuna namna NANI ANAPENDA KUAIBIKA
 
Inaitwaje, naomba unitajie
Kwenye simu za HTC au Samsung kuna appl imo moja kwa moja kwenye simu inaitwa OEM skin, ni free , ukijisisajili humo waweza itrack simu yako kwani inakujulisha no mpya inayotumika na simu yako. Kwa simu aina nyingine sina hakika sana kama app zake ni free ila waweza ingia google play ukaziangalia zile za free kama zitafaa kwa simu yako.

Embu jaribu hapa.

Click here to visit the Find My Phone website to try to track down your phone. You’ll need to be logged into the same Google account on the computer as you are on your phone. You can also click here to learn more about Find My Phone.
 
nakumbuka kipindi niko chuo siku hiyo pale meeda sinza napata kilaji mida ya sa nne usiku kuna mdada mmoja mzuri pembeni ya meza yangu alikua ameketi peke ake nikamuomba ani join kwenye meza yangu,akaitikia wito bila hiyana tukaendelea kupata kinywaji kwa pamoja na stori mbili tatu. Haikupita hata nusu saa akaja njemba mmoja hivi hata sijui alikotokea akaniambia eti alikua akinitafuta siku nyingi kwanini natoka na demu wake..kabla hata sijamjibu nilikula kelebu moja matata kuja kukaa sawa nimebaki peke angu kwenye meza na simu(s6) niliyokuwa nimeishika mkononi sina,kilikua ni kitendo cha fasta sana kutoka nje hawaonekani kuna bodaboda akaniambia amewaona huyo jamaa na mwanamke wameondoka na bodaboda pale mda sio mrefu nikabaki nimeduwaa tu pale. Baadae nilimueleza meneja wa bar akaniambia huyo jamaa anaitwa 'van dame' ndo huwa anatumia staili hiyo kuibia watu na wengi wameshalizwa
Kama baba angu mdogo vilee??
 
kumbe sometimes huwa mnakiri kuwa nyie ni wadhaifu.... mnadai haki sawa kwa nn
Ndugu yangu ningekuwa nimeenda jeshini ningemfwata eeeh kisa cha kupigwa bisibisi kwa kitu cha laki 4.
 
Back
Top Bottom