Uzi maalum kwa wale ambao walipitia mazito katika maisha yao

jerryempire

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
5,530
Reaction score
9,550
Habari wana jamvi, uzi huu ni maalum kwa wale wanzangu ambao walipitia wakati mgumu kwa jambo moja au lingine kisha kuona mwanga ili iwe kama chachu kwa wenzetu ambao wamekata tamaa ya maisha hali ya kuwa wanauhai

KISA CHANGU
Kwa umri wangu syo mkubwa kabisa ,lakini ni kijana ambae nilikuwa na bado nina ndoto za kufanya mengi katika maisha hasa kusaidia watu.Safari yangu ya kutafuta maisha kwa nguvu zote ilianzia mwaka 2015,baada ya kuhitimu elimu yangu ya astashahada ya utawala.

Baada ya kukaa muda mrefu bila ajira nikaamua kwenda kumtembelea ndugu yangu mkoani kigoma kwa njia ya mabasi ya Saratoga.

Saa 11 asubuhi gari iliondoka pale ubungo naweza kusema kuwa huo ndo ulikuwa mwanzo wa misukosuko, hasa pale tulipofika Tabora tulikuta pori kubwa sana lakini mwanzo kabisa tukakutana na askari wengi sana wakiwa na magari yao, akaingia mmoja na kutuambia kuwa mbele kuna uwezekano mkubwa sana wakuwepo na waasi kwani jana yake walikuwa wanafyatuliana risasi na polisi.

Basi wakaingia askari wawili wakiwa na silaha nzito na magazine za kutosha,ndo mara yangu ya kwanza kuona askari wakibongo wakiwa wanatisha kiasi kile.

Basi wale askari wakatuambia kuwa gari itaondoka kwa kasi kidogo hvyo tufunge mikanda na wenye kuomba sala zao tuombe kabisa,dah nakumbuka siku hyo niliomba mpka maskio yalikuwa yanaongea[emoji28][emoji28][emoji28].

Safari ikaanza huku wale jamaa wakizikoki bunduki mle mle ndani kisha wakalala kwenye ile njia ya katkat ya ndani ya basi huku wakimuamuru dereva aendeshe spidi mpka mwisho,pasipo kusimama kwa jambo lolote.

Dah naweza kusema yule dereva alikuwa vizuri mno kwani gari ilikuwa iliendeshwa moka spidi ya mwisho huku ikitoa alarm ya hatari gari zima tukiwa kimya huku sauti zilizokuwa zinaskika ni yesu na muhammad tu,maana kwa ile spidi ile gari ingegonga hata tufali tu basi ingekuwa mwisho wa maisha yetu.

Gari ilitembea kwa spidi hyo mpka tunamaliza misitu mirefu kama hiyo zaidi ya mi nne,hatimae tukatoka salama,ashukuriwe mungu.Mungu si athumani tukaingia kigoma salama mida ya saa 5 asubuhi.

Lengo la kwenda Mkoa wa kigoma ni kwenda kujifunza tiba mbadala kutoka kwa babu wa rafiki yangu,Nilipokelewa vizuri sana na kwa ukarimu mkubwa sana kutoka kwa watu wale wa kigoma.

Nilijifunza vingi sana kuhusu tiba za asili baada ya miezi 6,alikuja mtu kutoka Congo na kuvutiwa na jinsi nilivyokuwa muelewa kwa haraka katika tiba asili hivyo akanichukua na kunipeleka kwao congo,ili nikajifunze mengi kuhusu tiba asili.

Huko ndiko kulikofanya maisha yangu yabadilike kwa mambo ya ajabu na mateso ambayo leo hii ningekuwa marehemu hakika sitaisahau misitu ya goma,
nitarudi...
 
nawe unaweza kutupia kisa chako ili upate kuwa inspire wengi ambao wamekata tamaa na maisha
 
USIRUDI TENA,HUKUWA NA SABABU YA KUALIKA WATU KAMA UNATAKA KUHADITHIA HADITHI YAKO KWA MAFUNGU,UZI UNGEUPA TU JINA LINALOHISIANA NA HADITHI YAKO
 
Don't stress up yourself, no matter how bad situation it will change
 
sasa haya ndiyo mambo mazito kweli! hahaha kuna jamaa namjua kalala border siku tatu juu ya mti.

akisoma hii stori atashangaa saana.
 
ushanichosha kabla hata stori haijaisha.........
 
muendelezo,
Baada ya kukubali kusafiri nae,safari ilikuwa usiku tofauti na vile ambavyo nilitarajia huku tukitumia gari binafsi la wafanya biashara wa kikongo man,Asubuhi tulikuwa tunamalizia shughuli za pale uhamiaji kwa ajili ya kuingia congo.Safari iliendelea vizuri huku nikionyeshwa maeneo mbali mbali na wenyeji wangu huku nikipewa stori za hapa na pale.
Mwendo wa masaa 4,tukakuta kuna wanajeshi walivyoona tu gari yetu wakarusha nywaya barabarani,nilishtuka sana lakini wenzangu hakuna walio stuka wakanishusha uoga na kunambia kuwa askari wa congo ni tofauti na wa tanzania kwani wao huwa hawasimamishi gari na mkono bali ni kuweka vizuizi bara barani au hata kupiga risasi,na hata ndipo ninapoweza kuthubutu kwa kusema kuwa congo ndo inaongoza kwa rushwa kwani tulitoa rushwa ya dola 200,machoni mwa watu tena bila uoga.Tulikuwa tunaenda kijiji cha kalupash ambacho ni mwendo wa masaa 5 baada ya kuvuka msitu wa goma.Tulianza kuukata msitu wa goma saa 12,asubuhi hakika ulikuwa ni msitu ambao sijawahi kuuona katika maisha yangu.Baada tu ya kuuanza msitu kila mtu akajikuta tu amekuwa kimya pasipokuongea lolote.

MATATIZO YANAANZA
Tukiwa ndani ya msitu baada ya nusu saa tuona kama gogo limelazwa barabarani kwa mbali baada ya kusogea vizuri tukaja kugundua kuwa walikuwa ni watoto wawili ambao walikuwa wamelala barabarani huku wakiwa na bunduki kutuelekezea sisi,alafu kwa nyuma yao kulikuwa na wengine wamewashikia wenzao mkanda wa risasi ambao ulikuwa umeunganishwa kwenye bunduki zao.Dereva baada ya kuwaona akatuambia sasa ba mutu muswali buswala ma mwisho.Hakuna aliyeuliza alimaanisha nini lakini kwa kilichokuwa mbele yetu ote tukawa tumeshaelewa lakini cha ajabu hakuna aliyeswali zaidi ya kuanza kulia.Tulivyowakaribia tu walipiga risasi kama 20 juu wakitutaka tushyke ndani ya gari huku na wengine wakubwa wakiwa wanatoka msituni.Walikuwa ni warefu na wenye miili mieusi ya kutisha mno ambao kimuonekano tu walikuwa wanawakilisha kifo katika maisha basi ote tukashuka kisha mmoja akaingia kwenye gari na kushusha kila kitu.
Baada ya hapo kila mmoja wetu akawa anaitwa mbele na kuuljzwa maswali kwa kilingala kisha anawekwa pembeni,kiupande wangu sikuwa naelewa chochote,ilipofika zamu yangu nilikuwa natetemeka mno kiasi cha mikojo kutaka kunitoka nikaskia wakitaja tanzania kisha wenzao wakawa wanaitikia,kuskia hvyo nikamwambia yule jamaa nisamehe mdogo wangu dah,baada ya kusema hvyo nilipigwa na kitako cha bunduki cha kwenye tumbo kidogo nijinyee kama siyo kuzimia[emoji17][emoji17][emoji17].Kumbe ni kosa kubwa kumuita mtoto au mdogo,askari au muasi yeyote wa congo,baada ya hapo tukaamriwa ote tuvue nguo tulizovaa,tukatii amri ote kwenye costa tukavua ngua hakika tulikuwa tunalia kama watoto wadogo,kisha tukaachwa tuendelee huku tukiwa uchi vile vile baada ya wazee tuliokuwa nao kuwatia huruma,Tuliondoka mbio na gari yetu hali ya kuwa tukiwa uchi wa mnyama huku nafsi yangu ikiwa inajuta mno kwanini nilikubali kwenda
NITAREJEA KUMALIZIA
 
Unazingua nenda kafuturu weka story yote acha kurukaruka
 
Mkuu upoje ndio nini hivi unafanya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…