Nafikiri benchi la ufundi la simba lina kitu cha kujifunza kwa kipigo kile, mashindano ya caf hauwezi kwenda ugenini ukafunguka kutaka kucheza hovyo hovyo ni makosa makubwa sana hasa ukikutana na timu kubwa, mfano
1. Jana TP Mazembe wamecheza na CS Constantine ya Algeria ambayo kule kwao kwenye msimamo wa ligi ni ya nne huku TP Mazembe inaongoza ligi Congo DRC na pia ndiyo klabu bora Afrika kwa ranking za sasa kuliko klabu yoyote, pamoja na hayo walijitahidi kucheza defensive footaball ila wakapigwa 3-0,
2. Mwezi september tu hapo hao AS-Vita walikutana na Al-Masry huku Masry ikiwa imetoka kuitoa Simba kwenye Confederation cup kwa droo ya 2-2 taifa na 0-0 kule Egypt ila pale Kinshasa walipokea kipigo cha 4-0 kama wamesimama
3. Final zote mbili ile ya champions league na confederation cup zimeisha kwa 3-1kwa 3-0
Yaani Raja casablanca alishinda 3-0 home, lakini akapigwa 3-1 pale Congo na Vita. Raja kabeba ndoo
Al Ahly alishinda 3-1 home, akapigwa 3-0 pale Tunisia na Esperance. Esperance kabeba ndoo.
4. Mechi za confederation cup zinazoendelea currently Zamalek kaipiga Coton Tchad 7-0 pale Egypt, ila nae kachezea 2-0 pale N' Djamena Chad.
Nyumbani ni nyumbani na ugenini ni ugenini tu
Nini kifanyike
Simba kwenye hatua hii au hata wakifanikiwa kuvuta mechi zote za ugenini kuanzia hiyo ya Al Ahly wahakikishe wanacheza deep defensive football huko wakifanya counter attack tena kwa speed.
Waache ubishi kutaka possesive footbal la sivyo yatawakuta mabaya zaidi
Sent using
Jamii Forums mobile app