Elimu bora na sahihi hufungua akili, siyo kuifunga. Epuka fikra kwamba kupata vyeti pekee ni mafanikio; badala yake, tumia elimu kama zana ya kupata maisha unayotaka. Kisha, tumia maarifa yako kuongeza thamani yako kwa jamii, na epuka kuridhika na kubweteka na kile unachokijua.