Uzi maalum wa kupeana mawazo ya biashara

Mbagala Tz

Member
Joined
Mar 16, 2017
Posts
57
Reaction score
42
Wadau wa Jf

Baada ya hali ya maisha kuwa ngumu kwa wengi wetu nimeona ni vyema nianzishe Uzi huu wa kupeana mawazo chanya ya kibiashara kwa maana humu JF ni sehemu ambayo nondo zote makini huwa zinapatikana

Kwahyo kama una wazo la biashara sio mbaya ukishare na sisi hapa na pia ni vizuri ukiweka na gharama za mtaji na faida itakayopatikana kwa kukisia tu, {yaani kabusiness plan kauongo na kweli} katika uzi huu ili tuweze kujikwamua na hii hali ngumu ya uchumi inayotukabili

Naomba kuwasilisha
 
Watu wana mawazo ya ngono mkuu.

Alizia ngono utajibiwa uzi utajaa kweli kweli.

Watu hawana mawazo ya biashara.


Hata wewe mtoa mada nikikupa wazo la biashara utalikataa, maana ni wale wale.

Watu wanalialia tu hali mbaya wakati fursa zipo nyingi tu!
 
Watu wana mawazo ya ngono mkuu.

Alizia ngono utajibiwa uzi utajaa kweli kweli.

Watu hawana mawazo ya biashara.


Hata wewe mtoa mafa nikikupa wazo la biashara utalikataa, maana ni wale wale.
C kama watu hawana mawazo ya biashara wanayo ila hawataki kushare na wengine hilo ndo tatizo. Unaweza muomba mtu akupe muongozo wa biashara anayoifanya kwa kukusaidia mawili matatu yakuongoze na wewe utakapotaka kuifanya biashara hyo hakika ni ngumu kupata msaada kama huo na hii nadhani inatokana na uchoyo na ubinafsi tu.
 
Hali sasa siyo nzuri kifedha watu wengi wanakosa mitaji. Katika hali hii nawashauri kufanya biashara katika eneo la kilimo na mifugo ambalo unaweza kuanza hata na elfu 50, laki1 na kuendelea. Nunua vifaranga wa kuku wa nyama kama una uwezo wa kupata vyakula (feeds) pesa yako itarudi haraka.
 

kiongozi we huna kabisa shughuli unayojishughulisha nayo?
 
kiongozi we huna kabisa shughuli unayojishughulisha nayo?
Mimi niko kwenye mchakato wa kuanzisha biashara ya nafaka na katika kutafutatafuta taarifa nkakutana na mdsu fulani hivi akanambia hizo yeye ndo biashara zake nkaona hapa sasa ntapata mwanga ila amini nakwambia tangia hapo nmeshamtumia ujumbe kama mara mbili anisaidie taarifa kadhaa kuhusu biashara hyo ila hajawahi kunijibu na ndo maana nkayaandika niliyoandika hapo juu maana nmekutana nayo.
 
Umeongea kwel kabisa ...uzi kama.huu huwez kua na zaid ya page 10 ila nyuzi za mtu katembea na kumpa mimba mama mkwe wake utaona comments 200 na views 10k.
mfano mimi nlitoa thread ya mikoa kwa sasa ambayo ni mizuri kwa ajili ya biashara sijui ipo page moja tu
 
Labda kwako ndo hali sio nzuri, juzi mtu kanunua flat screen curved ya milioni 6 unasema nini bwana
pesa zipo na wenye pesa wapo ila sio kujionyesha ila unaona tu mwenyewe
 
Ndo hivyo tena huwezi kumpangia mtu cha kusoma.
 
Na labda wew unajishughulisha na biashara gani!? Tupeana uzoefu na ujuzi
 
Hivi Nikiwa Na Laki 3 kwenye Kilimo Itanisaidia Nini nikiwa Na Maaan Naitaji Kujua Kwa Laki 3 ni kilimo gani naweza Kufanya Japo kwa Udogo Wake
Unataka kulima nini, unataka kulima wapi, eneo/shamba unalo, je shamba limeandaliwa au bado ni pori, unategemea kufanya kilimo cha umwagiliaji au cha mvua?

Walau ukielezea hayo watu wanaweza kukusaidia zaidi.
 
Mfano kama ishu ya forex kiukweli watu wanapiga hela sasa wengine wenye husda walivyoona hivo wanakuja kila uchao kufungua thread zakusema watu wanapigwa sjui wameliwa kumbe ukweli ni kwamba watu wanapiga hela...sasa watu kama hao na roho hizo hawawez kamwe kumuona mtanzania mwenzake anafanikiwa...roho za kuona mwingine anafanikiwa wamepewa wachache
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…