Uzi maalum wa kupeana mawazo ya biashara

Uzi maalum wa kupeana mawazo ya biashara

Unataka kulima nini, unataka kulima wapi, eneo/shamba unalo, je shamba limeandaliwa au bado ni pori, unategemea kufanya kilimo cha umwagiliaji au cha mvua?

Walau ukielezea hayo watu wanaweza kukusaidia zaidi.
Okay Mkuu, Shamba Lipo Na Sio Poli Ninachoitaji Kulima Ni Matikiti Maji maeneo Ya Magohe Kule na Kuhusu maji nafikili nitamwGilia Sio Mvua Ipo Hvyo kiongozi
 
Fursa zipo sana .

Wakati huu Wa masika maisha ya watu yanakuwa magumu sana hasa kifedha , kuna ile mikoa inazalisha mahindi , unaingia bush moja na kilo 5 yako unawakopesha hela ili wakulipe mahindi baada ya mavuno ya mahindi , .. Mfano kuna sehemu moja watu wapo tayari kukopeshwa Tsh 20,000/= ili walipe gunia moja LA mahindi mwezi Wa 7 ... So chukua laki5 gawa kwa elfu 20 utakuwa na magunia ya mahindi 25


Kwa mwaka huu bei ya mahindi kwa gunia hapo hapo kijijini ilifika elfu 45 kwa gunia. Na hiyo bei ilikuwa wakati wanavuna mwezi Wa 8,9 hadi October. so ukichukua elfu 45 zidisha kwa gunia 25 unapata Tsh 1,125,000/= hapo mzigo umeuzia hukohuko bush hujaangalia masoko ya mbele...

Pia kuna ishu ya mbolea , yani ukiwa na mtaji wako Wa kueleweka kama M1 nakuendelea unanua mbolea hafu unawakopesha wakulima , mfuko mmoja Wa mbolea utapewa gunia 2.5 wakishavuna. So chukulia ukinunua mifuko ya mbolea (UREA) Mifuko 25 kila mfuko elfu 41,000 kwa huko bush itakugharimu Tsh 1,025,000/= hapo hutolipia tena usafir maana unanunua hapo hapo bush na kukopesha kwa wakulima. Piga hesabu baada ya mavuno utakuwa na magunia 50 km utakopesha kila mfuko kwa gunia 2 tu za mahindi achana na gunia 2.5 walivyozoea , gunia 50 ukaamua kuuza hapo hapo kijini kwa kila gunia elfu 45 utakuwa na kama Tsh 2,250,000/= hapo hujaangalia masoko mengine ya mahindi,, huu tunaita uwekezaji Wa muda mrefu..
 
Hata hivyo kuna hii fursa ya forex lazima tuiangalie kwa urefu na mapana yake. Kifupi forex ni real haina kuzunguka sana kama ilivyo network marketing , ni biashara halali ambayo unaweza kuwekeza kwa kuanzia na sh elfu 50 na kuendelea. Ishu kubwa kwenye forex ni elimu ya kulijua soko linaendaje na nifanyeje kwa wakati huu, wengi sana hiyo elimu hatuna na hatuna budi kuitafuta kwa UDI na uvumba..

Pamoja na hivyo kipindi tunaendelea kuhangaika kutafuta elimu ya kutosha sio vibaya tukawa tunanunua signals kutoka kwa wenzetu ambao wanauelewa mpana juu ya forex na wanatoa signal zinakupa profit kama unazingatia risk management. Kwa kufanya hivi itatusaidia kukuza mitaji yetu huku tukihangaika kupata mafunzo ambayo yatatusaidia tuweze kujitegemea sisi wenyewe.

Kuna watu kibao wanauza signal na zinakuwa nzuri kwa bei ya kimaskini kabisa . wapo Wa $5 hadi $70 kwa mwaka mzima unapokea signals. So km unamtaji wako Wa Tsh 200,000/= ukawa umewekeza na kutumia hizo signals zao kwa kuzingatia risk management kwa siku kulala na elfu50 sawa na $25 ni jambo LA kawaida maisha yanaenda.

Huku unatumia signal za kulipia endelea kuhangaika kutafuta chimbo za kukufundisha uweze kujitegemea katka forex.

Huo ndo ushauri wangu nipo tayari kukosolewa.
 
[emoji121]
SAMAHANI YAKE INASTAHILI KABISA HAPO!!!
Hakuna mfugaji hapo,2018 itapita then ataomba samahani pia.Ukiwa na wazo lifanyie kazi,huu ndio muda wa kuandaa mashamba mtu asianzishe excuse mwakani.Kama mnavyojua sasa hivi Watanzania tumeanza kuwa makauzu kwa watu wasiojituma...
 
Hata hivyo kuna hii fursa ya forex lazima tuiangalie kwa urefu na mapana yake. Kifupi forex ni real haina kuzunguka sana kama ilivyo network marketing , ni biashara halali ambayo unaweza kuwekeza kwa kuanzia na sh elfu 50 na kuendelea. Ishu kubwa kwenye forex ni elimu ya kulijua soko linaendaje na nifanyeje kwa wakati huu, wengi sana hiyo elimu hatuna na hatuna budi kuitafuta kwa UDI na uvumba..

Pamoja na hivyo kipindi tunaendelea kuhangaika kutafuta elimu ya kutosha sio vibaya tukawa tunanunua signals kutoka kwa wenzetu ambao wanauelewa mpana juu ya forex na wanatoa signal zinakupa profit kama unazingatia risk management. Kwa kufanya hivi itatusaidia kukuza mitaji yetu huku tukihangaika kupata mafunzo ambayo yatatusaidia tuweze kujitegemea sisi wenyewe.

Kuna watu kibao wanauza signal na zinakuwa nzuri kwa bei ya kimaskini kabisa . wapo Wa $5 hadi $70 kwa mwaka mzima unapokea signals. So km unamtaji wako Wa Tsh 200,000/= ukawa umewekeza na kutumia hizo signals zao kwa kuzingatia risk management kwa siku kulala na elfu50 sawa na $25 ni jambo LA kawaida maisha yanaenda.

Huku unatumia signal za kulipia endelea kuhangaika kutafuta chimbo za kukufundisha uweze kujitegemea katka forex.

Huo ndo ushauri wangu nipo tayari kukosolewa.
Tupe elimu zaidi mkuu
 
Hata ukiwa na elfu 50 ni mtaji ni vile uwe na nia kufanya ulichokusudia..kuna mtu humu katoa ushuhuda alianza na elfu 50 ..sasa hivi anajenga nyumba

ni kweli mkuu,lakini sio biashara zote zinahitaji uanze na elf 50,au toeni ideas ambazo mtaji huu unaweza kufanya biashara gani????
 
Hata ukiwa na elfu 50 ni mtaji ni vile uwe na nia kufanya ulichokusudia..kuna mtu humu katoa ushuhuda alianza na elfu 50 ..sasa hivi anajenga nyumba
Je una uhakika kuwa anajenga nyumba?tusitafute Fedha rahisi tujitume
 
Nadhani uzi nimzuri. Hapa kuna biashara ya msimu na biashara ambayo ungependa baada ya miaka 3 hadi 5 uko financially stable. Hii ndio nitatolea wazo.

Kuna kilimo cha parachichi kwaajili ya masoko ya nje. Mnaungana kwenye group la watu kama 10 ili muwekeze angalau akari 50 hadi 100. Mna-outsource kazi zote na kampuni then baada ya miaka 3 mnaanza kupata kipato. At year 6, kama mmewekeza eka 100 kwa watu 10, kila mtu anauwezo wa kupata kati ya milion 50 -70 kwa mwaka bila kuhabgaika management na marketing issues. Kwamaelezo zaidi ni PM
 
Je una uhakika kuwa anajenga nyumba?tusitafute Fedha rahisi tujitume
Hakuna fedha rahisi ila ukweli ndio huu kwamba hauhitaji mtaji mkubwa kufanikiwa
anza na ulichonacho ukiwa na nia ya dhati utafanikiwa
 
Back
Top Bottom