Uzi maalum wa nyau wetu majumbani

Uzi maalum wa nyau wetu majumbani

Paka wanafundishika sana mkuu ingia youtube zipo video kibao paka wanafundishwa jinsi ya kutumia choo cha kukaa ili kukidhi haja zao na wanaelewa na inakua ndo sehemu ya maisha yao kila siku anaposikia kutoa haja anaenda chooni anaflash kisha anasepa.Uwezo wao kwenye kuelewa mambo kwa haraka uko tofauti na wanyama wengine kama mbwa ila paka unaweza kumfundisha kwa vitendo na akakuelewa. kuhusu chakula ndivyo walivyoumbwa sasa unataka ashinde njaa masaa matano kwa tumbo lile si unataka ashinde mitaani sasa awe shume? hiyo ni nature yao kila baada ya muda fulani wanahitaji kula, mfumo wao wa chakula uko tofauti na wengine elewa hivyo mkuu.
Wala siwaelewi, japo nafuga paka na ninaye mkongwe na anajua akiskia sauti ya mfuko anajua ni menyu time, ila sio km ananipenda lah hasha anapenda chake kiwepo, na bado nasimamia palepale paka hafundishiki, nimekaa naye miaka 9 haelewi kitu. He is just broken
 
.
Three%20cuties.._heart_eyes__heart_eyes_%20Double%20tap%20if%20you%20love%20these%20cuties..%...jpeg
 
Wala siwaelewi, japo nafuga paka na ninaye mkongwe na anajua akiskia sauti ya mfuko anajua ni menyu time, ila sio km ananipenda lah hasha anapenda chake kiwepo, na bado nasimamia palepale paka hafundishiki, nimekaa naye miaka 9 haelewi kitu. He is just broken

Unaweza ukawa umekaa nae hata miaka 15 ila kama haujaonyesha nia ya kumfundisha aelewe nini sahihi cha kufanya basi sahau mkuu utamuona kama mzigo tu. Labda haujajua tu njia gani za kumfundisha akuelewe na atii kila unapotaka afanye ulilomfundisha. Paka hafundishi kwa maneno anafundishwa kwa vitendo na lazima awe sehemu ya tukio unalotaka afanye anachopaswa kufanya ndo atakuelewa japo itachukua hata wiki mbili kuanza kuelewa vyema na kuhifadhi kwenye kumbukumbu zake. kuhusu kula sio paka tu hata mbwa nao wameumbwa na asili ya kula kula tu sasa kama amehisi kuna kitu cha kula kinanukia kwa nini asiombe apewe? kumbuka wana uwezo mkubwa pia wa kunusa.
 
Na sisi masela tunaokaa ghetto tunacomment wapi?
Maana paka hawezi kukaa ghetto atakufa njaa
 
Back
Top Bottom