Uzi maalumu wa kufarijiana kwa wale wote wanaopita kwenye hali ngumu za kimaisha

Uzi maalumu wa kufarijiana kwa wale wote wanaopita kwenye hali ngumu za kimaisha

Pole wote mnaouguliwa, poleni wote mliofilisika komaeni ipo siku mtainuka tu,
poleni mliodanganywa kimapenzi kisha mkaachwa poleni ila mjikaze mtapata wenzi wengine walio wema kwenu,

poleni wote ambao mabosi wenu wanawanyanyapaa kazini jipeni moyo na kujipanga jinsi ya kupata mtaji wa kujiajiri,

poleni wahitimu wote ambao kwa muda mrefu hamna ajira au mmepata ajira ambayo kipato chake ni kidogo sana kiasi kwamba ukipata pa kutokea utakimbia bila kugeuka nyuma.

Poleni mliofiwa,
poleni mliotumbuliwa siku si nyingi mtapata kazi nyingine.

Poleni sana.
Mkuu umegusa hadi matatizo yangu ha ha ha ha

Kila siku lazim nickilize wimbo wa prof ft harmonize-yataisha
 
Pole mkuu. Ukipata muda share
kuna kipindi nilipataga misukosuko
nilitamani Dunia ipasuke...ilifikia kipindi nilitamani hata nigongwe na gari au kitu kibaya kinipate ili nife but haikuwa hivyo...
ni vile unapita wakati mgumu hata ndugu/rafiki na mpenz wanakukimbia ni hatari sanaaa
tangu hapo sikutaka tena kuamini/kuwategemea watu......
nilijiapiza na Mungu wangu na kuweka ahadi na Mungu wangu
from now nakula mema ya Nchi japo sijafikia but atlest now...naona mwanga mkubwa wa maisha yangu tofauti na kipindi cha Nyuma...
Kuna wakati now nadhani bado nipo ndotoni coz siamini kama ndiyo Mimi ambaye watu walinicheka na kunidhihaki....
hata walionitenga Leo ndiyo wakwanza kuninyenyekea...
nilichojifunza
wakati mwingine Mungu anaruhusu upitie magumu ili akufikishe kwenye kusuidio na sehemu aliyokuandalia...
lait kama wale niliowategemea wangefanya kama nilivyodhani au lait kama baba asingenitelekeza pengine leo "NISINGEKUWA MTU MAALUMU" katika Dunia yetu. ....

Natamani Kushare Nanyi story abt My life
 
Wale wenye shida ya hela ya haraka pia tunahitaji faraja? Kama ndio naomba na mimi mnifariji.
 
Kukata tamaa ni umaskini ukatae.
Kabla hujataka kufarijiwa jiulize ni wangapi wanahitaji faraja yako hali wewe umekata tamaa.?
Nilishawahi kukata tamaa nilivyokua mjamzito. Kama kujiua isingekua dhambi ningeshapotea kwenye ulimwengu huu. Mama yangu nae alikua sababu ya mimi kutojiua. Miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito nilipata tabu sana. Machozi kila siku. Kila nikiamka nawaza kutoa ujauzito au nizae niwe single mom dunia ije kunihukumu. Lakini Mungu ni mwema sana. Nilisema kama ambavyo napata mawazo ya kuwa mama wa huyu kiumbe basi na Mungu hatoniacha.
Sasa hivi hata nipitie gumu kiasi gani hata kulia nimeacha nikiwaza kuna binadamu anaishi kwa sababu mimi nilimleta duniani.
Ninachomaanisha hata upite magumu kiasi gani kuna watu bado wanaamini katika wewe hivyo usikate tamaa. Chukulia kama kipindi cha mpito yote yatarudi kama mwanzo mapito yako yakiisha.
 
Kila mtu anapitia magumu yake

Saiz nipo kweny mwendokas la kutoka kimara to kivukoni na tumejaa pomoni kweny gari na wote nahis tunaenda kazin ila ukiuliza mishahara utakuta wetu ni chini ya laki tatu na apo una kadigirii kichwan
 
Back
Top Bottom