Uzi maalumu wa kupeana mawazo na kutafuta washirika wa biashara

Uzi maalumu wa kupeana mawazo na kutafuta washirika wa biashara

HS CODE

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2019
Posts
1,784
Reaction score
4,376
Nimegundua Jf hata ukianza mada kwa kusalimia, wajumbe hawajibu, bali wanaenda moja kwa moja kwenye kuchangia, hivyo kwa leo, sitosalimia.

Kwa wengi hali ni ngumu, iwe walioajiriwa au walioko mitaani, hata hivyo hata wenye unafuu wa maisha, haimaanishi wamesha maliza utafutaji wa pesa.

Inawezekana kwa sasa unayopesa mkononi, lakini hujui ni biashara gani ufanye, au kuna mchongo unausikilizia lakini hujui ukitiki pesa utakayopata uifanyie nini, kubwa kuliko yote kuna watu humu wana mawazo ya biashara lakini wanakosa watu makini wakushirikiana nao.

Uzi huu ni wa kupeana mawazo ya biashara zinazoweza kufanyika bila kujali zinahitaji mtaji wa kiasi gani, hata kama sisi bado hatujaanza kuzifanya au tulifanya zikafeli lakini tunaona upo uwezekano wa watu kuingiza njuruku. Inawezekana pia tukautumia kutafuta watu wanaovutiwa na mawazo yetu na wako tayari kushirikiana kwenye safari ya mafanikio. Mimi naanza na mawazo yafuatayo:

Wazo la kwanza
Kuna wale wenzangu wamesoma masomo ya sayansi, na tunajua kabisa masomo ya sayansi kuna changamoto kwenye practicals kwanini msomi asifungue center kwa ajili ya practicals tu, Ili madogo wasaidike, huku anaingiza pesa. Najua vile vifaa ni gharama lakini kila penye nia pana njia.

Wazo la pili
Zanzibar ni kisiwa chenye mahitaji mengi kutoka nje ya nchi, lakini vingi vinavyohitajika bara vinapatikana kwa wingi. Kuanzia bidhaa za shambani kama, mazao ya nafaka, mifugo mpaka za viwandani. Kwanini tusubiri mpaka waagize nchi za mbali?

Wazo la tatu
Watu wanazaa sana, na kutokana na changamoto za utafutaji wanakosa muda wakuwalea Watoto wao, kwanini msomi usiwaze namna ya kutatua changamoto hii, kwa kuanzisha daycare, unatafuta mdada ambaye utamlipa kulingana na unachopata Ili awatunze watoto na wewe unapata mia mbili mia tatu kuliko kuzurura na bahasha na umecharara?

Hebu ongezea na wewe.
Asante.

NB: Nimepata inspiresheni ya kuandika uzi huu, kutokana na michango ya mwanachama griti thinka Daudi1, kama utasaidia kutatua changamoto za watu, sifa zote apewe yeye. Ukisababisha changamoto lawama zote nipeni mimi.

Moderator, naomba msiuhamishe jukwaa huu uzi, ubaki hapa hapa.
 
Issue ya zanzibar ni kweli bidhaa nyingi zinatoka arabuni kuliko hapa Tanganyika, so fulsa hiyo ni nzuri sana ila na hawa ndg zetu wameremaha sana kupenda products za kiarabu.
 
Issue ya zanzibar ni kweli bidhaa nyingi zinatoka arabuni kuliko hapa Tanganyika, so fulsa hiyo ni nzuri sana ila na hawa ndg zetu wameremaha sana kupenda products za kiarabu.

Au wamelemaa kwa sababu sisi na wao hakuna anayewaza kupeleka bidhaa huko.

Nahofia pia usikute japo nchi ni moja, lakini kukawa na mlolongo wa kodi na ushuru unaokwamisha. Ngoja wataalamu waje kutufahamisha.
 
Sekta Ya Madini,
Kwa uzoefu mdogo niliokuwa nao katika sekta hii pana naamini kama tukitengeneza timu yenye moyo wa kipambanaji haswa, bila ya umimi na ujuaji tukasshirikana kwa manaufaa yetu binafsi na nchi kwa ujumla tunaweza kupata matokeo makubwa katika muda mchache na vijana wakaishi maisha ya ndoto zao ndani ya nchi yetu nzuri ya Tanzania,
Kwa sasa madini yanayohitajika sana Duniani ni,Lithium,Nikel,Kopa
 
Au wamelemaa kwa sababu sisi na wao hakuna anayewaza kupeleka bidhaa huko.

Nahofia pia usikute japo nchi ni moja, lakini kukawa na mlolongo wa kodi na ushuru unaokwamisha. Ngoja wataalamu waje kutufahamisha.
Yap kwa upande wa ushuru hilo halikwepeki na ukweli ni kuwa products kutoka bara inatakiwa uwe na makaratasi yote ya biashara vinginevyo uwe na ngoja niwasiliane na flani.

Znz ni nchi nyingine kabisa hasa kwa watanganyika dhidi ya wazanzibari!.
 
Utastaajabu fursa nyingi utapewa ni za kununua na kuuza, vipi za kutengeneza wenyewe na kuuziana?.

itakuwa vyema zije nyingi za kutengeneza.

Ni kweli kabisa Mkuu, uko sahihi sana.
 
Sekta Ya Madini,
Kwa uzoefu mdogo niliokuwa nao katika sekta hii pana naamini kama tukitengeneza timu yenye moyo wa kipambanaji haswa, bila ya umimi na ujuaji tukasshirikana kwa manaufaa yetu binafsi na nchi kwa ujumla tunaweza kupata matokeo makubwa katika muda mchache na vijana wakaishi maisha ya ndoto zao ndani ya nchi yetu nzuri ya Tanzania,
Kwa sasa madini yanayohitajika sana Duniani ni,Lithium,Nikel,Kopa

Asante sana Mkuu, ni kipi hasa unaaamini wewe na wengine tunaweza kukifanya kwa vitendo ili tupige hatua?

Je unahitaji timu ya watu wenye mtazamo unaofanana ili mfanye kitu, unafikiria namna ya kupata rasilimali fedha, vibali n.k?
 
Yap kwa upande wa ushuru hilo halikwepeki na ukweli ni kuwa products kutoka bara inatakiwa uwe na makaratasi yote ya biashara vinginevyo uwe na ngoja niwasiliane na flani.

Znz ni nchi nyingine kabisa hasa kwa watanganyika dhidi ya wazanzibari!.

Duh! Huu ni ukweli mchungu. Kuna kitu inabidi Serikali na wadau wakifanye.
 
Nilitamani mada ingebaki kule kule jukwaa la hoja mchanganyiko, naona huku kumejificha sana kwa watu kuja kutafuta fursa.
 
Nilitamani mada ingebaki kule kule jukwaa la hoja mchanganyiko, naona huku kumejificha sana kwa watu kuja kutafuta fursa.
Pasi kumuomba Moderator auache kule wanauamisha tu, wao hawajali kama uzi una fulsa au NO.

Hata ule uzi uliousoma una lengo la kuwafungua vijana waliolala wakisubiri serikali but mods wameubeba na kupeleka sijui wapi huko, that's why wachangiaji ni wale wale walionza as here!.
 
Nilitamani mada ingebaki kule kule jukwaa la hoja mchanganyiko, naona huku kumejificha sana kwa watu kuja kutafuta fursa.
Kuna tatizo kubwa katika hii nchi,ulipoanza kuweka bandiko lako hili muhimu ulitoa na Angalizo kuwa Uzi huu usiamishwe ili kupata wachangiaji wengi zaidi,cha ajabu Uzi umehamishwa pasipo kujali umuhimu wa mada husika kwa wakati wa sasa na wakati ujao,
Nafikiri kama Uzi huu ungehusu mambo ya Ushoga na Usagaji labda mambo yangekuwa mazuri zaidi,
Taifa letu linapitia kipindi kigumu cha watu wanaoweza kufikiri kuliko kipindi chochote kile tangu tupate Uhuru,mambo ya msingi hayapewi kipaumbele,mambo ya upuuzi ndio yanapewa nafasi katika majukwaa kama haya,redio na tv,
Hakuna nchi tamu na nyepesi kutoboa km Tanzania,uwezo wa kufikiri katika mambo yanayohusu Utajiri na Ukwasi ni mdogo sana kwa Watanzania wengi,
Fursa zilizopo ni kubwa kuliko akili za watu wengi,ukituliza akili na kuwa mvumilivu Bilioni 1 ni suala kawaida tu katika nchi hii!
 
Pasi kumuomba Moderator auache kule wanauamisha tu, wao hawajali kama uzi una fulsa au NO.

Hata ule uzi uliousoma una lengo la kuwafungua vijana waliolala wakisubiri serikali but mods wameubeba na kupeleka sijui wapi huko, that's why wachangiaji ni wale wale walionza as here!.

Duh! Ni kweli Mkuu. Huku naona wengi hawapendi kupoteza muda kupafika. Kuna nyuzi nyingi zingeweza kuwajenga watu ila ziko maeneo yasiyofikiwa na wengi.
 
Back
Top Bottom