Uzi maalumu wa kuwaombea washkaji zetu waliotutoka enzi za utoto

Uzi maalumu wa kuwaombea washkaji zetu waliotutoka enzi za utoto

Anna- school mate wa std 7, nayakumbuka macho yako makubwa ya duara, ulikua mpole na siku zote ulipenda kuniwekea mkono wako begani mwangu iwe tumekaa au tunatembea, ulikua na ndoto ya kua daktari, Homa ya Mapafu ikakatisha ndoto zako, R.I.P Angel.

Aminu- school mate olevel, ulikua mjanja sana, uliipenda biashara na ulisema utakuja kua mfanyabiashara mashuhuri, nakumbuka tulipokua tunajadiliana mambo makubwa kuliko umri wetu, i'm glad i met you, Malaria ikakatisha ndoto zako, Innalillah wainna illah Rajiun.

Issa- Childhood friend, ulinipenda sana, ulisema ungekuja kunioa no matter what, nilikua nachukia ukianza hizo mada, kila mtu mtaani alijua Issa anampenda Culture, tulikua wazee wa kamati kwenye mambo yote yaliyohusu shughuli za watoto na vijana, ulipenda sana muziki na kudance, barabara ile ya Victoria ikakatisha uhai wako, Rest Easy Mwamba.

Deo- daah ukanipigia simu unataka kurudi kwenu ukasalimie wazazi wako, kumbe ndio uliniaga jumla, yale maji ya bahari yakaondoka na roho yako, R.I.P Besty, ulikua huongei lakini ukiwa na mimi unapiga story tunacheka, walikushangaa hadi wakakuzoea. [emoji24]
wapumzike kwa aman wenzetu, tusichoke kuwaombea🙏
 
2012 mshkaj wng straton baada ya furaha ya sisi kumaliza olevel siku ya graduation ulikuwa na pikipiki furaha zilizidi kumbe ile siku ndio ulikuwa mwisho wako uliniambia unachomoka mara moja unaenda road apo kufuata fegi baada ya dk5 nasikia ukunga uku watu wakikimbilia barabarani kumbe ukiingia na pikipiki chini ya semi kichwa kikafumuka na ndoto zako zikaishia hapo hapo nakujuza tuu ulipo baada ya wewe kuondoka matokeo yalikuja umepata Div2 nalikumbuka sana shati lako jeupe jipya ulilovaa ile siku ila ghafla lilikuwa jekundu. Nakukumbaga Sana mpaka leo na nakuombea uendelee kupumzika kwa amani. Amen
usichoke kumuombea mkuu, apumzke kwa aman uko alpo🙏
 
Dua Said, my classmate Mahiwa Sec. Alilazimika kukatwa mguu baada ya kansa kumshambulia, bado haikufaa kwa yeye kuendelea kuishi duniani hatimaye akafariki miezi kadhaa mbele. Bado nakukumbuka sana Mahiwa Boy.

Abby, friend wa ukubwani. Baada ya miaka mingi ya kutoanana nikapokea tarifa ya kifo chako. Ilikuwa ngumu kupokea lakini hakukuwa na namna. R.I.P Swahiba, Nyangao inakumiss.
tusichoke kuwaombea wenzetu🙏
 
Anna- school mate wa std 7, nayakumbuka macho yako makubwa ya duara, ulikua mpole na siku zote ulipenda kuniwekea mkono wako begani mwangu iwe tumekaa au tunatembea, ulikua na ndoto ya kua daktari, Homa ya Mapafu ikakatisha ndoto zako, R.I.P Angel.

Aminu- school mate olevel, ulikua mjanja sana, uliipenda biashara na ulisema utakuja kua mfanyabiashara mashuhuri, nakumbuka tulipokua tunajadiliana mambo makubwa kuliko umri wetu, i'm glad i met you, Malaria ikakatisha ndoto zako, Innalillah wainna illah Rajiun.

Issa- Childhood friend, ulinipenda sana, ulisema ungekuja kunioa no matter what, nilikua nachukia ukianza hizo mada, kila mtu mtaani alijua Issa anampenda Culture, tulikua wazee wa kamati kwenye mambo yote yaliyohusu shughuli za watoto na vijana, ulipenda sana muziki na kudance, barabara ile ya Victoria ikakatisha uhai wako, Rest Easy Mwamba.

Deo- daah ukanipigia simu unataka kurudi kwenu ukasalimie wazazi wako, kumbe ndio uliniaga jumla, yale maji ya bahari yakaondoka na roho yako, R.I.P Besty, ulikua huongei lakini ukiwa na mimi unapiga story tunacheka, walikushangaa hadi wakakuzoea. [emoji24]
Mohamed daa ulikuwa mwanangu nakumbuka mwaka 2005 kuna mjinga mmoja alikuzingua ilikuwa pasaka uka mpa kichapo bahati mbaya alikujerui kwa jiwe tuka kupeleka hospitali ya mkoa tulikuwa na mzee Six tulirudi home usiku mkubwaa ukiwa umeshonwa nyuzi nane!

Shaban Mrutu aka Piko ulikatizwa uhai wako kwa ajali ya kugongwa na gari ukiwa na pikipiki ilikuwa Makambako

Jafet Rutahiwa mzee wa vancuva niliskia ulikutwa umefia geto huko Arusha!

Romana kambona daa namis ile mi utani yako!!
NYUMA YENU MBELE YETU
 
Mwanangu wa dhahabu.....UG,eliasi maugo,Arusha sanawari,nakumiss sana mchizi wangu....nakumbuka nilikua dar napigiwa simu kichaa wako wamempiga shokaa,akaangukia mto sanawari.akafa. Christopha aka krisp bado nakukumbuka mwanagu
 
R.I.P khassim
 
Dah! Uzi wako umenipa kumbukumbu mbili za utotoni hadi leo hazijawahi nitoka kichwani.

Ya kwanza ni primary school. Tulikuwa na michezo ya kuruka sarakasi kwenye milima ya pumba kwenye mashine za kusaga nafaka. Boniface aliruka kwenye rundo moja kumbe lilikua na moto. Hatukua tukijua kuwa pumba huwa tabia ya kuungua kuanzia chini na juu huonekana ziko kawaida. Siku mbili baadae Bony alifia hospital. Taswira yake akiwa ameungua hadi leo haijawahi nitoka kwenye fikra.

'Msiba' wa pili ni primary school pia. Rafiki yetu mmoja, masoud, alipotea tukiwa tunacheza mpira. Wenzetu wa mwisho kumuona walidai alipanda lori la mzee mmoja diwani. Hadi kesho hakuwahi onekana. Tetesi ni kuwa mzee yule alikuwa na michezo ya kutoa kafara. Pumzika kwa amani Masoud.
 
Akida jumbe akida mungu akulinde ulitutoka ghafla ndugu yangu,ndugu zako wa damu bado tupo na cc tunasubiri hatma yetu
 
Back
Top Bottom