Uzi wa mafundi (umeme,ujenzi,bomba) na wenye nyumba

v0il0r

Member
Joined
Jan 23, 2018
Posts
24
Reaction score
26
Uzi wa mafundi wa majumbani kama umeme, ujenzi, bomba na n.k + wenye nyumba lengo nikupata msaada au kutoa ushauri au unataka fundi Kwa wenye nyumba

Mfano: wewe una hitaji fundi wa umeme labda pasi, jiko, tv, short-circuit, n.k au ujenzi unaweza pata fundi contacts zake, au ukaomba ushauri

*Binafsi ni fundi umeme kama utahitaji msaada wa kifaa kama pasi, oven, micro-wave, fridge, n.k (Dar -kibamba, nicheki pm)

Karibu mafundi na wenye nyumba.
 
Kama upo Kibamba hapo ni mtaani kwangu kuna kazi soon ntakupa pale Gogoni ya wiring.
 
Mafundi wengi wa Kibongo mnajenga kwa mazoea pia hamuendi na manadiliko ya Dunia kiteknolojia.
Pia Fundi utambue UFUNDI NI SANAA siyo unajenga Chemba za Choo zimekaa kama sambusa, zimechomoka juuuu ka mlima Meru, zina joint kuubwa kati ya mfuniko na chemba utadhan uwazi wa Bonde la Uffa.
Mnaharibu sana nyumba za watu kimuonekano nyie viumbe. Rudin shule msome na Mpunguze ubishi mnapopewa ushauri wenye mantiki
 
Tumekupata mkuu
 
Sitaki hata kuwasikia, jinsi mlivyoninyosha pumbavu zenu hahaha
 
Sema unakuwa haujapata mtu mwenye kipaji na ufundi siyo fundi anafanya ili apate pesa.
Mafundi bomba wengi kazi zao mbovu. Na vipimo vyao wengi wanatudanganya. Kama umejenga nyumba yako chukua tape measure kapime uangalie ikiwa bathroom yako wemefuata standard ya hivi vipimo








Tuje kwenye chemba wamekomaa na chemba za kizamani za kujengea ambazo huwa zinatema harufu na mazalia ya mende na zinachukua nafasi kubwa wakati siku hizi kuna chemba za kisasa zinaitwa rodding eye drainage system. Faida yake;

(1) Mfumo huu unampa mwenye nyumba eneo kubwa la kufanya shughuli zake

(2) Hauingizi wala kufuga mende

(3) Unaongeza zaidi mvuto na mwonekano wa nyumba

(4) Unadumu kwa muda mrefu

(5) Haurudishi harufu





HAPA KABLA YA KUWEKA PAVING BLOCKS



HAPA BAADA YA KUWEKA PAVING BLOCKS


👆Piga picha hapo ingekuwa zimewekwa chemba za kujengea zingekuwa ngapi na hako kanjia usingeweza kupita kwa uhuru au kupitisha vitu👇

 

Attachments

  • 1682681087303.png
    288 KB · Views: 27

Hii system nimependa mkuu soon nataka nifanye drainage kwa hyo nije nimuambie fundi wangu kuwa nataka rodding eye drainage siyo….na kama haelewi hii system ntafanyaje hili anielewe
 
Nahitaji waya wa umeme mita 15 2.5mm na 1.5mm
Nichek 0692911361 Dsm
 
Fundi rangi nipo hapa pia.karibuni kwenye page yangu ya Instagram mjionee kazi za kisasa .
@finishing za kisasa 2257.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…