Uzi wa vyakula tu

SUPU YA MAKONGORO

Mahitaji

-Makongoro (miguu ya ng'ombe) kiasi
-Limao 1 kubwa
-Kitunguu swaum
-Tangawizi
-Chumvi
-Pilipili

Matayarisho

Safisha makongoro kisha yatie kwenye pressure cooker au yapike kwenye jiko lolote.

. tia kitunguu swaumu, tangawizi, chumvi,limao na maji kiasi. Baada ya hapo yachemshe mpake yaive na yawe malaini na pia ubakize supu kiasi inaweza kuchukua kama dk 45 au saa 1 hivi.

Baada ya hapo yaipue na upakue supu yako kwenye bakuli katia pilipili kiasi kisha itakuwa tayari kwa kuliwa.

Note:
Ukiwa unanunua makongoro hakikisha unachukuwa yale yasiyokuwa na manyoya na pia
hakikisha usiyachemshe kupitiliza kwani yakiwa malaini sana utashindwa kuyaenjoy.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…