Habari..
Sisi kuna menu huwa tunaenda kula kwenye mgahawa mmoja wa kihindi, inaletwa hiyo curry na chapati au Naan. Siku moja nikamuuliza chef inavyopikwa akanielekeza sababu tumezoeana sana, na i went to try ikatoka perfect.
Recipe:
Dengu iliyochemshwa kiasi
Nyanya moja.
Kitunguu maji kikubwa
Garlic punye 3 au 4.
Viazi mviringo vikubwa vi3
nyanya paste kijiko cha chakula 1.
Tangawizi mbichi kijiko cha chai 1.
Paprika kijiko cha chai 1
manjano ya unga kijiko cha chai nusu. (kama unapendelea)
Curry powder kijicho cha chai 1 (kama unapendelea)
Nazi 1.
Chumvi kiasi.
Cauliflower kiasi.
Pilipili zile ndefu za kijani 2, ndefu nyekundu 2, na mbuzi moja. (pilipili unaweka kwaajili ya harufu hivyo usizipasue hata kidogo)
Majani ya giligilani au majani ya kitunguu. (option)
Kupika. Process yake ni kama ya kuunga nyama au mchuzi wa aina yeyote.
Kaanga kitunguu kisiwe cha brown, add garlic+Ginger, then add nyanya iliyokatwa katwa koroga ikikaribia kuiva add nyanya paste na viungo vyote vya unga unavyoenda kutumia, add viazi korogo koroga kabla havijaenda kuiva weka dengu yako, weka na cauliflower angalia zisijevurugika. acha viive kidogo weka tui lako la nazi na ka chumvi, pambia kwa juu na pilipili zako ambazo hazijapasuliwa na majani ya vituunguu au majani ya giligilian. Then wapakulie wajilambe na chappat zako.
NB. Cauliflower na viazi lazima zionekane ndio tunazila kama nyama, yaani tonge nyama.