Uzi wa vyakula tu

Nakubaliana na wewe. Ugumu upo kwa familia zetu hizi una mke mna watoto sita, ndugu zako na ndugu wa mkeo jumla mpo kumi na tatu ndani uwezekano wa kumudu kula hivi ni mdogo
Upo sahihi kabisa mkuu.Tatizo kubwa ambalo linatusumbua waafrika ni umasikini wetu wa akili wa kuwekeza nguvu zetu,akili zetu,maarifa yetu pamoja na ujanja wetu katika kupata watoto wengi badala ya kuwekeza katika kupata utajiri.
 
Hapa Arusha kuna mboga wanaita mnafu ni tamu sana ikiandaliwa vizuri nimekuja kuijulia Arusha
Unaitwa Mnavu, hii ni mboga ya watu wenye asili ya tanga(wazigua) Mnavu mbali na utamu wake, lakini tena huongeza damu kwa watu wenye matatizo ya kupungukiwa na damu na hata maafisa wa afya huwashauri wananchi kutumia mboga ya mnavu ili kuinarisha MFUMO wa damu yao mwilini.
 
Uupate uliopikwa kwa tui la nazi... Mama! 👌😝 Kando yako bonge la ugali wa moto na glass yako ya juice ya ukwaju, baridiiiii! 🤣 🤣 🤣
 
Mnafu na Saladi Ndo mboga zangu kuzipata Dar ni Changamoto

Mnafu ukiutia utumbo na nazi ni hatari sana

Kuna kuku mnafu nayo ni balaa tupu
Boonge moja la mboga mnafu nimeipenda halafu haikifu unaweza kuila kila siku kwa mtindo wa kubadili namna ya kuipika
 
Ndio ndio. Hapa Arusha wanalima sana na ni maarufu hii mboga, ni tamu hakika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…